Rais Samia: Inapotokea mwanamke ananyanyaswa ni wazi mfumo wake wa uwakilishi unaingia dosari

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Ni ukweli usiopingika, mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa, na mustakabali wa Taifa ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi, inapotokea mwanamke ananyanyaswa ni wazi mfumo wake wa uwakilishi unaingia dosari - Samia

Ziangalieni familia zenye mizozo ambako wanawake wanafanyiwa sivyo, family inakuwa haiko 'stable' na hata makuzi ya watoto yanaathirika

Hata sehemu za kazi unaweza kumuona mwanamke mwenzio kaingia kazini asubuhi uso haukunjuki vizuri ukimuambia moja anakujibu tatu ukimuita chemba ukimuuliza tatizo limetoka nyumbani, kwahiyo unayanyaswaji unafanya wanawake wasi-perform vizuri

Afadhali wanaume akikereka huko ana njia zingine za kupita akafurahi na akarudi kazini ametulia, lakini sisi hatuna, ni nyumbani kazini, kazini nyumbani, so handle with care sisi ni assets muhimu

Endapo sisi kama jamii tutafanikiwa kubadili mazoea na firka potofu ama zilizopitwa na wakati naamini kwa kiasi kikubwa tutatokomeza mila na desturi kandamizi kwa mwanamke na watoto.

Historia inaonesha na kuthibitisha nafasi ya Mwanamke ni kujenga umoja, amani na mshikamano katika jamii. Ikitikoea Mwanamke ametengwa na kunyanyaswa hata ushiriki wake katika hayo utakuwa hafifu na hatimaye kufanya ufanisi wake kupungua.
 
Mama haya yakina mama atuachie wenyewe tunyooshane....."HAKI SAWA" twende haki sawa... nao wakiona vipi waingie chocho maisha yaendelee au sio, mbona hata sisi wanaume tunanyanyaswa sana na hawa viumbe?

Shida ipo hapa, kutaka kupingana na elimu ya uumbaji iliyosema Mwanamke ni kiumbe dhaifu na kutaka kushupaza shingo kudai HAKI SAWA, twendeni tu JINO KWA JINO.... mje mbebe zege, muwe madereva wa malori, makondakta, mabaharia, mapilot, wagema ulanzi, mafundi, majambazi, magaidi, masheikh, wachungaji nk tutaona mwisho wake.
 
Akitekwa na akili ya jinsia atakuwa kituko, na kama tatizo ni upeo wa kielimu kwa hio hana command of authority hivyo akawa tegemezi wa wasaidizi kwa kila kitu kila wakati kila mahali atakwama sana. Aache waziri wa jinsia na watoto ayasemee hayo. Yeys atimize wajibu ili aonekane mtu credible.

Tunajua umuhimu wa mwanamke na ndio walezi na wazazi wetu. Yeye achape kazi tu.
 
Naunga mkono hoja na kuongezea kuwa Wanaume wanaopigwa na wanawake na kabali juu na vitofali pia watazamwe na kupaziwa sauti.

Nina ushuhuda wa mwanamke kumpiga jirani wake mwanaume kiasi cha kumuumiza jicho vibaya na kukaa ndani mwezi. Mwanaume huyo alienda polisi kushitaki akaja na askari na defender juu. Lakini yule mwanamke hawakumpeleka polisi...! Yule mwanaume alihama nyumba hile.
 
Mama haya yakina mama atuachie wenyewe tunyooshane....."HAKI SAWA" twende haki sawa... nao wakiona vipi waingie chocho maisha yaendelee au sio, mbona hata sisi wanaume tunanyanyaswa sana na hawa viumbe?....
Mkuu hujawahi kutana na mwanamke jambazi?
Au hujawahi ona mwanamke pastor?
Hebu nenda pale Mikocheni B kwa mama Rwakatare ukasali hapo uone muziki wa Wachungaji wanawake wanaomiliki mpaka bastora.
 
Mama haya yakina mama atuachie wenyewe tunyooshane....."HAKI SAWA" twende haki sawa... nao wakiona vipi waingie chocho maisha yaendelee au sio, mbona hata sisi wanaume tunanyanyaswa sana na hawa viumbe?

Shida ipo hapa, kutaka kupingana na elimu ya uumbaji iliyosema Mwanamke ni kiumbe dhaifu na kutaka kushupaza shingo kudai HAKI SAWA, twendeni tu JINO KWA JINO.... mje mbebe zege, muwe madereva wa malori, makondakta, mabaharia, mapilot, wagema ulanzi, mafundi, majambazi, magaidi, masheikh, wachungaji nk tutaona mwisho wake.
Hakuna mtu mbaya kama mwanamke kama angepewa uwezo sawa na mwanaume kwa nguvu au zaidi?
Wanaume wasingepumua
 
Back
Top Bottom