Rais Samia, ili kuondokana na huu uchafu, harakisha Katiba Mpya

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,489
40,999
Katiba pendekezwa ya Warioba, ilisema kuwa mawaziri wasiwe wabunge ili Rais awe na uwanja mpana wa kuwapata wasaidizi kwenye nafasi za uwaziri.

Siku za nyuma, wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere, kabla ya mabadiliko ya katiba, mawaziri hawakuwa wabunge.

Leo katiba yetu hii mbovu inamlazimisha Rais kuteua mawaziri kutoka kwenye kundi la wabunge ambao wengi wao uwezo wao ni duni, lakini wanaupata ubunge kwa sababu wana pesa za kuhonga wapiga kura, hata kama pesa zenyewe, kwa baadhi yao, ndiyo hizo walizoziiba au wakati mwingine kukwepa kodi, ingawa wapo wanaotumia pesa zao safi walizozichuma kwa jasho lao, halafu wanaenda kuzitumia kuwahonga wapiga kura.

Mtu aliyeupata ubunge kwa kuhonga wapiga kura, au kuwahonga wasimamizi ili mpinzani wake aondolewe na yeye apite bila kupingwa, akiteuliwa kuwa Waziri, ataweza kuwa ni waziri mwenye maadili?

Serikalini wamejaa viongozi ambao mapito yao yamejaa uchafu tele, halafu tunategemea tupate manukato ya kuvutia.

Waziri Mkuu, mbunge ambaye hakupata hata kura moja.

Waziri wa Fedha, Nishati, Habari, n.k; wote wabunge wa kupachikwa.

Watu wasio na maadili tunataka wasimamie maadili. Haya maajabu yapo Tanzania pekee.
 
Nani wakutunga hiyo Katiba na nani wakusimamia hiyo katiba?

Kwani Katiba ya sasa haikatazi watu kuiba na huu uchafu wanaofanya?
.
 
  • Thanks
Reactions: TPP
Tusiisukumie Katiba Mpya kila mzigo, muhimu wahusika wafuate sheria hizi zilizopo kwenye ofisi zao, kulea ujinga kwa kisingizio cha kusubiri Katiba Mpya ni kujiangamiza wenyewe.
 
Katiba haitazuia watu kuiba. Waambieni watu ukweli
Hata katiba ya sasa hairuhusu kuiba
 
  • Thanks
Reactions: TPP
Serikalini wamejaa viongozi ambao mapito yao yamejaa uchafu tele, halafu tunategemea tupate manukato ya kuvutia.

Waziri Mkuu, mbunge ambaye hakupata hata kura moja.

Waziri wa Fedha, Nishati, Habari, n.k; wote wabunge wa kupachikwa.

Watu wasio na maadili tunataka wasimamie maadili. Haya maajabu yapo Tanzania pekee.
Warumi 3:23
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
 
Unaamini Katiba Mpya itapatikana?
Watanzania hasa wana CCM wasafi tuamue moja kuendelea na uchafu huu mwaka nenda mwaka rudi ama tuamue kuachana nao kwa kuwa na katiba mpya?

Kumbuka ujio wa katiba mpya ni kuizima rasmi CCM, jambo ambalo hawa hawa wanaolalamikiwa si waadilifu ndiyo hawa hawa wana nguvu kubwa ndani ya CCM.

Naiona safari ndefu yenye mashimo, giza na mimba njiani.
 
Waziri wa Fedha, Nishati, Habari, n.k; wote wabunge wa kupachikwa.
"Uongozi wako wa zamani utaratibu ukweli wako mpya" Methali ya kisomali.

Hii Methali imenipa nguvu Toka nisipate Jana kati.
 
Tusiisukumie Katiba Mpya kila mzigo, muhimu wahusika wafuate sheria hizi zilizopo kwenye ofisi zao, kulea ujinga kwa kisingizio cha kusubiri Katiba Mpya ni kujiangamiza wenyewe.
Unapokuwa na katiba ambayo inambana kuwa waziri lazima awe mbunge, hata pale anapoona ndani ya Bunge wamejaa wachafu watupu, bado atalazimika atafute wa afadhali ndani ya kundi la hao wachafu.

Katiba mpya itampa uhuru wa kumtafuta yeyote anayefaa toka mahali popote, nje ya Bunge.
 
Katiba haitazuia watu kuiba. Waambieni watu ukweli
Hata katiba ya sasa hairuhusu kuiba
Katiba hauzui watu kuiba, ni kweli. Lakini katiba inamlazimusha Rais kuteua mawaziri miongoni mwa wabunge. Je, kama wabunge wote wakiwa na kasoro, wengine uwezo mdogo, wengine wevi, wengine maadili ya maisha ni zero, unadhani Rais atafanya nini, zaidi ya kuwateua walio wa afadhali badala ya kuwapata wazuri wasio na mashaka?
 
Katiba hauzui watu kuiba, ni kweli. Lakini katiba inamlazimusha Rais kuteua mawaziri miongoni mwa wabunge. Je, kama wabunge wote wakiwa na kasoro, wengine uwezo mdogo, wengine wevi, wengine maadili ya maisha ni zero, unadhani Rais atafanya nini, zaidi ya kuwateua walio wa afadhali badala ya kuwapata wazuri wasio na mashaka?
Wanaoiba ni mawaziri tu? Watumishi wa halmashauri ukiacha DED sio wateuliwa wa raisi, lakini Kuna wizi kuliko kawaida
 
Katiba pendekezwa ya Warioba, ilisema kuwa mawaziri wasiwe wabunge ili Rais awe na uwanja mpana wa kuwapata wasaidizi kwenye nafasi za uwaziri.

Siku za nyuma, wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere, kabla ya mabadiliko ya katiba, mawaziri hawakuwa wabunge.

Leo katiba yetu hii mbovu inamlazimisha Rais kuteua mawaziri kutoka kwenye kundi la wabunge ambao wengi wao uwezo wao ni duni, lakini wanaupata ubunge kwa sababu wana pesa za kuhonga wapiga kura, hata kama pesa zenyewe, kwa baadhi yao, ndiyo hizo walizoziiba au wakati mwingine kukwepa kodi, ingawa wapo wanaotumia pesa zao safi walizozichuma kwa jasho lao, halafu wanaenda kuzitumia kuwahonga wapiga kura.

Mtu aliyeupata ubunge kwa kuhonga wapiga kura, au kuwahonga wasimamizi ili mpinzani wake aondolewe na yeye apite bila kupingwa, akiteuliwa kuwa Waziri, ataweza kuwa ni waziri mwenye maadili?

Serikalini wamejaa viongozi ambao mapito yao yamejaa uchafu tele, halafu tunategemea tupate manukato ya kuvutia.

Waziri Mkuu, mbunge ambaye hakupata hata kura moja.

Waziri wa Fedha, Nishati, Habari, n.k; wote wabunge wa kupachikwa.

Watu wasio na maadili tunataka wasimamie maadili. Haya maajabu yapo Tanzania pekee.
madiwani wanapatikana kwa rushwa, wabunge wanapatikana kwa rushwa, mawaziri wanapatikana kwa ushirikina, rais akianza kuteua anatafuta kwanza makada wa chama chake walioshindwa udiwani na ubunge.....kisha tutegemee maajabu?
 
Wanaoiba ni mawaziri tu? Watumishi wa halmashauri ukiacha DED sio wateuliwa wa raisi, lakini Kuna wizi kuliko kawaida
Tukiwa na DED mwenye uwezo, weledi na mwenye uadilifu, atawasimamia walio chini yake kuhakikisha wizi hautokei.
 
Hizo ni ndoto. Unafikiri maded wote zaidi ya 120 hawana uwezo?
Kama Halmashauri ina upotevu wa fedha za umma, DED hana uwezo. Kama angekuwa na uwezo, walioiba fedha ya umma angewatambua kabla ya CAG na kuwachukulia hatua.
 
Back
Top Bottom