Rais Samia, huu wizi wa Tsh Bil. 3.4 kwa Mwaka wa wabunge 19 utaufumbia macho?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,702
71,013
Kama mbunge halali analipwa zaidi ya shilingi milioni 13.8 kwa mwezi basi wale wabunge 19 wa Ndugai ambao hawana chama chochote kilicho waidhinisha kuingia bungeni bali kwa ubabe na kiburi cha Ndugai huku akilindwa na marehemu Magufuli watakuwa wanalipwa takribani bilioni 3.4 kwa mwaka bila kuhesabu posho za vikao.

Pesa hizo za umma ni wizi mkubwa wa wazi kabisa ila wenye baraka za bunge na rais aliyepita. Je, nawe una bariki wizi kama huo? Au Utaufumbia macho kwa vile hao ni wabunge wanawake na kinachofanyika ni kuikomoa Chadema?

Angalia usiingie kwenye kapu la lawama kama za mtangulizi wako aliyekuwa na kiburi cha uzima.

Wizi huu unatofauti gani na watumishi hewa? Nguvu ya kukemea mengine utaipata wapi kama mengine utayafunika wakati kila mwenye akili anayaona?

Wewe sio yule!
 
Ni wivu tu miaka yote lilipokuwa kundi kubwa ndani ya bunge nini walichochangia ktk maendeleo ya nchi hii. Bunge gani la watu 300 lilileta changes. Mwisho niambie kama Mbowe angekuwa Bungeni ungesema ni wizi? Badala ya kumuomba rais nenda mahakamani kupambana na maovu.
 
Hatari Sana kufukua fukua makaburi, mengine unayapotezea tuu Maisha yasonge Kama makosa yalishafanywa na yeye akiwa kwenye system
 
Ni wivu tu mika yote lilipokuwa kundi kubwa ndani ya mbunge nini walichochangia ktk maendeleo ya nchi hii. Bunge gani la watu 300 lililetachanges. Mwisho niambie kama Mbowe angekuwa Bungeni ungesema ni wizi? Badala ya kumuomba rais nenda mahakamani kupambana na maovu.
I never urgue with a fool, people mighty not notice the difference. Nenda FB kajadili upoloto wako na watoto wenzio
 
Mara baada ya waziri mkuu msitaafu Edward Lowasa kujiunga na kuinunua Chadema ili awe mgombea urais mwaka 2015 , kitu cha kwanza kabisa alipokabidhiwa tu chama alipiga marufuku siasa za kiharakati na kushauri siasa hizo hazina tija kwa sasa. Edward Lowasa alionya kuwa Chadema lazima igraduate kutoka chama cha kiharakati hadi kuwa chama cha siasa sasa.

Edward Lowasa alifafanua madhara ya chama kubaki cha kiharakati muda wote kuwa ni pamoja na kupinga maendeleo yote ya nchi ,kuombea mabaya nchi ,kushirikiana na mabeberu ili kuiibia nchi ,pamoja na kushangilia kila lililobaya kwa taifa ili kumfurahisha tu anayefadhili hizo harakati zako. Matokeo ya harakati hizi ni chama kuchukiwa na wazalendo na kupoteza ushawishi kwa wananchi.
Hakika Lowasa aliona mbali. Leo brand ya chadema imeharibiwa vibaya, chama kilichojizolea umarufu kwa kutetea wanyonge leo kinataka machinga na mama ntilie wafukuzwe mitaani!!! Leo ni furaha kubwa kwa Chadema ndege kukamatwa na wazungu!!!

Pia tangu tarehe 17 mwezi march Tanzania imekumbwa na simanzi isiyo na kifani mara baada ya kutangazwa kwa kifo cha rais Magufuli.

Mamilioni ya watanzania wameangua kilio kila kona kwamba sasa mwokozi wao ameondoka, cha kushitusha ni kwamba wananchi wa hali ya chini kabisa ndiyo wanaoongoza kwa kilio kinyume na tulivyokuwa tumeaminishwa kwamba Magufuli alikuwa ananyonga wanyonge!

Kitendo cha hayati rais Magufuli kuagwa na mamilioni ya watanzania huku wakiangua vilio njia nzima na kutandika kanga zao chini ili mwili upite imeenda kinyume kabisa na wasaliti wa nchi hii akina Tundu Lisu na genge lake.

Kwa jinsi msiba huu unavyoenda naamini utakuwa darasa tosha kwa wasaliti wa nchi hii akina Tundu Lisu ,Godbless Lema, Chahali, Ngurumo, Mange Kimambi na wengine wengi, sasa wataelewa kumbe watanzania siyo vilaza.

Wataelewa kumbe watanzania wanajua yupi anapigania haki zao kwa vitendo na ni yupi ni mpiga makelele nyuma ya keyboard.

Kwa mapenzi haya yanayoonyeshwa na Watanzania kwenye msiba huu ni lofa tu atakayeendelea kuamini kwamba eti Tundu Lisu aliibiwa kura kwenye uchaguzi mkuu uliopita.

Wito wangu kwa wasaliti wa nchi hii wanaoshangilia msiba kwamba sasa Magufuli ameondoka watarudi Tanzania na kuanza tena kutumika kuiba rasilimali za nchi hii kama walivyokuwa wanafanya huko nyuma wajue tu kwamba wanapoteza muda.

Watanzania siyo vilaza ,wanajua fika Tundu Lisu aliwatisha kwamba watashitakiwa MIGA ikiwa watabadili sheria za madini.

Tundu Lisu aelewe kuwa hawezi kuwa rais wa Tanzania kwa kushinda Twitter akikejeli kila lililojema kuhusu nchi yetu,
Tundu Lisu kupitia msiba huu atakuwa ameelewa na kupata darasa kwamba ukitaka kupendwa na Watanzania tumikia watanzania na siyo kutumikia Acacia
 
Samia anapenda “wapinzani” wawepo Bungeni. Alishawahi kusikika akisema wapinzani walikuwa wanawachachafya CCM enzi hizo na yeye alijiunga siasa ili akawabane mawaziri.

Nina imani Samia hawezi kuwafanya kitu hao akina mama 19. CHADEMA kama vipi si wachague 19 wengine kama haiwatambui wale waliopo ili mbivu na mbichi ziwe wazi na tuone Bunge litaact vipi?
 
Acha unafiki wee mwanasaccos, badala ya kumuuliza Mbowe kwanini kamati haitaki Kukutana ili itoe majibu ya rufaa Kama wamefukuzwa au hapana unakimbilia kwa watu wa CCM kwani ndo wanaoitisha hiyo kamati kuu ya Chadema?
Nyumbu hovyo kabisa.
 
Wamezulumiwa nini? Haya ni maoni yangu kama mtanzania mlipa kodi, Chadema imehusikaje hapo wakati wao walishamaliza kazi yao through vikao?
Mliwaambia Kama hawajaridhika na maamuzi ya kikao wakate rufaa, wakakata rufaa Sasa mbona mmekaa kimya hamjibu rufaa yao? Au itasikilzwa 2025 Mkishamaliza kula ruzuku?
Nyumbu hovyo kabisa.
 
Zile dola milioni 400+ mlilipwa?? tuanzie hapa kwanza, vipi 1.5trl ile??
Kichwa chako ni dispenser ya mate hakina kazi nyingine
 
Wamezulumiwa nini? Haya ni maoni yangu kama mtanzania mlipa kodi, Chadema imehusikaje hapo wakati wao walishamaliza kazi yao through vikao?
Yaani huyo mjane achana nae kabisa, akilala CHADEMA akiamuka Mbowe.
Mpaka anasahau kuomboleza.
 
wale wabunge 19 wa Ndugai ambao hawana chama chochote kilicho waidhinisha kuingia bungeni bali kwa ubabe na kiburi cha Ndugai huku akilindwa na marehemu Maguful
Lililobaki ni kumwomba CORONA asimsahau huyu.

Akitusaidia kwa kazi hiyo atakuwa ametusaidia sana Tanzania kama alivyofanya wiki kadhaa zilizopita.
 
I never urgue with a fool, people mighty not notice the difference. Nenda FB kajadili upoloto wako na watoto wenzio
......., but you are already a fool! Unawezaje kuita malipo ya bunge kwamba ni wizi? Kama una shida ya kimfumo pursue it legally. sasa wewe unaleta thrd ikiwa na hukumu! Rubbish!
 
Kwahiyo ulichoandika hapa kinahalalisha kuwepo bungeni watu wasiowakilisha chama chochote cha siasa?
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom