Rais Samia: Hatutaruhusu utoroshwaji madini kuendelea. Zifanyike doria kuwabaini wahusika

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Rais Samia Suluhu Hassan amesema ifikapo 2025, Serikali inalenga Sekta ya Madini iweze kuchangia 10% ya Pato la Taifa. Ameeleza hayo katika Hafla ya Utiaji Saini Mikataba baina ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini.

Amesema, "Tunasikia Madini yamepenya huku na huku, jitihada zinafanyika kuzuia hali hiyo. Waliotumwa kusimamia utoroshwaji madini badala ya wao kuwa chanzo, warudi walinde Rasilimali yetu"

Ameongeza, "Hali ya utoroshwaji haikubaliki na hatutaruhusu Uhujumu huu kuendelea. Zifanyike doria za mara kwa mara ili wahusika wajulikane"
 
Rais amekiri madini yetu kutoroshwa lakini ameamua kuwaacha watoroshaji waendelee kubaki ofisini walinde madini yetu, huu kama sio udhaifu ni nini?

Huu utoroshwaji kweli upo au ni siasa tu?
 
Tulia kama ulivyo utulivu wenyewe. Rais halazimiki kupokea ushauri wowote au mawazo ya mtu yeyote yule aongozapo. Hii humuweka huru na maamuzi yenye maslahi mapana ya taifa.
 
Biteko jiandae
Nani mwenye jukumu la kulinda mali ya umma wa Watanzania, ni waziri wa sekta husika au vyombo vya ulinzi likiwamo jeshi la police?

Ingekuwa masuala ya sera za madini ingekuwa na mantiki Dotto kulikwa kichwa, otherwise wizara ya madini nao wawe na jeshi usu kama ilivyo wizara ya maliasili na utalii ili kwenye kila mgodi mdogo au mkubwa kuwe na askari walio chini ya mamlaka ya wizara ya madini ili unapoendelea utoroshwaji basi waziri apigwe chini.

So far, kwa kazi aliyofanya Doto kuhakikisha masoko ya madini yako kila mkoa na/au Wilaya yenye kuchimba madini, hiyo ni achievement kubwa sana.

Na kama madini yanapitishwa mpaka airports, au mipaka mingine, kula nako Doto anatakiwa awe airports zote au mipaka ya kawaida?

Ila kwa kuwa Madam President anazidi kuwasoma wasaidizi wake na kama anaona kuna mtu ana uwezo mkubwa wa kusimamia wizara ya madini basi apewe wizara. Kwani waingereza wanasema they all "serve her pleasure"

Kila la heri kwenye mkataba huu, japo naomba kujuzwa tuna asilimia 16 kama kwenye Tembo Corporation (Kabanga Nickel) au 16% za Twiga Corporation.

Kila la heri Madam President SSH
 
Kumbe wanafahamu kuwa madini yanatoroshwa, lakini eti wanaoyatorosha hawafahamiki!

Sasa wamejuaje kuwa yanatoroshwa to begin with?

Na doria anayoitangaza rais ina maana hao watoroshaji ambao hawafahamiki hawajamsikia?

Kiufupi ni wazi kabisa kuwa chini ya ccm haitawezekana kumaliza ufisadi wa rasilimali za Taifa hili. Watu wanabembelezana tuu.

Tungekuwa tunajikita kwenye uwajibishwaji wa mafisadi, haya yasingeendelea kutokea. Sasa rais anazungumzia doria kwamba ndiyo solution. Lakini kuwatafuta na kuwakamata watoroshaji pamoja na wale wanaowawezesha kuyatorosha hakupo. Hao watakaofanya doria hawatasaidia lolote. Uwajibikaji ndiyo msingi. Yani “accountability”
 
Vyombo vya dola kazi wanayoweza ni kupambana na CHADEMA na kufungua mashtaka ya uongo.
Tunakumbuka shuka kumekucha.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema ifikapo 2025, Serikali inalenga Sekta ya Madini iweze kuchangia 10% ya Pato la Taifa. Ameeleza hayo katika Hafla ya Utiaji Saini Mikataba baina ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini...
Fukuza watu kazi,hizi Kauli "hatutaruhusu"hazina maana,inajurikana kabisa kutorosha madini ni kosa,anayefanya inabidi aadhibiwe vikali.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema ifikapo 2025, Serikali inalenga Sekta ya Madini iweze kuchangia 10% ya Pato la Taifa. Ameeleza hayo katika Hafla ya Utiaji Saini Mikataba baina ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini.

Amesema, "Tunasikia Madini yamepenya huku na huku, jitihada zinafanyika kuzuia hali hiyo. Waliotumwa kusimamia utoroshwaji madini badala ya wao kuwa chanzo, warudi walinde Rasilimali yetu"

Ameongeza, "Hali ya utoroshwaji haikubaliki na hatutaruhusu Uhujumu huu kuendelea. Zifanyike doria za mara kwa mara ili wahusika wajulikane"
Utoroshwaji madini mie ndo naweza zuia kwa sababu najua mbinu zao!! Babu yangu alikuwa mwizi wa madini nilimsaidia mnoo!...na bado wantumia mbinu hizohizo sasa Mama Samia wewe si unanijua niite nifanye kazi hiyo!

nitumie hata E-mail nije nikufanyie kazo hiyo ni dakika sifuri tu nakuleta taarifa kamili!.....ukitaka kuendelea na kazi niite tufanye kazi
 
Utoroshwaji madini mie ndo naweza zuia kwa sababu najua mbinu zao!! Babu yangu alikuwa mwizi wa madini nilimsaidia mnoo!...na bado wantumia mbinu hizohizo sasa Mama Samia wewe si unanijua niite nifanye kazi hiyo!

nitumie hata E-mail nije nikufanyie kazo hiyo ni dakika sifuri tu nakuleta taarifa kamili!.....ukitaka kuendelea na kazi niite tufanye kazi
Nashauri serikali ianze na huyo baba yako, ulete ushahidi achukiliwe hatua za kisheria ndo upewe kazi ya kudhibiti hao watoroshaji.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema ifikapo 2025, Serikali inalenga Sekta ya Madini iweze kuchangia 10% ya Pato la Taifa. Ameeleza hayo katika Hafla ya Utiaji Saini Mikataba baina ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini.

Amesema, "Tunasikia Madini yamepenya huku na huku, jitihada zinafanyika kuzuia hali hiyo. Waliotumwa kusimamia utoroshwaji madini badala ya wao kuwa chanzo, warudi walinde Rasilimali yetu"

Ameongeza, "Hali ya utoroshwaji haikubaliki na hatutaruhusu Uhujumu huu kuendelea. Zifanyike doria za mara kwa mara ili wahusika wajulikane"
Madini hapana, tembo ndio!!
 
Nashauri serikali ianze na huyo baba yako, ulete ushahidi achukiliwe hatua za kisheria ndo upewe kazi ya kudhibiti hao watoroshaji.
Msomege kwa uelewa!........ mie sikusema ivo!! usinirishe maneno!! tumia akili kunijibu siyo unakurupuka tuu!!
 
Back
Top Bottom