Rais Samia, gharama za maisha zinazidi kupanda juu. Penye njaa na mateso hapawezi kuwa na amani

Wimbo

JF-Expert Member
Oct 23, 2012
783
524
Mama Mpendwa Shalom

Mwenendo uliopo mpaka sasa, japo tunakupongeza kila kona kwamba unaupiga mwingi mambo ni magumu.

Hawa walioko vijijini ambao ndo hasa wapiga kura wako hawajui habari ya Ukraine na Putin wao, wanachokihitaji wapate maisha ahueni, wakati nchi nyingi zilizoathirika kama sisi zinajipanga kutenga ruzuku ya kugharamia mfumuko wa bei ya mafuta sisi tunaibandika ilivyo na hata wabunge wengine wanalalama ati Waziri ameondoa tozo.

Mama mahali penye njaa na mateso hapawezi kuwa na amani. Ongezeko zaidi ya ya asilimia 50% ya diesel toka umeshika madaraka hata kama linasababishwa na external forces lazima njia mbadala za kulegeza nati litafutwe.

Najua unao washauri wengi Wazuri Wa uchumi na siasa lakini nikuombe Mama yetu iangalie Tanzania, kiangalie Chama chetu CCM wengine wanaweza kukushauri kwa maslahi binafsi watu wengi wakaumia.

Huyo mama unayemtetea kila siku anayeuza mbogamboga alikuwa analipa tsh 500 kupanda bajaji Jana bei imepanda nauli Tsh 1000/- tumemrudisha nyuma sana. Usifurahie akina mama hao na madira yao wapiga iyenaiyena "mama anaupiga mwingi" wengine wanafiki tu na wengi wao hawajui machungu ya mama Wa kijijini ambaye bado anaishi kwa Jembe la mkono.

Punguza gharama za uendeshaji wa serikali yako tenga ruzuku ya mbolea na mafuta na kupigania bei za mazao ya wakulima wetu wanyonge, pambana reli zikamilike haraka ili kupunguza matumizi ya fedha za kigeni zinazonunua mafuta, kile kitengo cha kukusanya dhahabu zetu ili kuwa na reserve itakayotusaidia kubalance currency yetu kiangalie vizuri.

Lakini usiache kuwa mhubiri kwa hao wanaojikusanyia huku wengine wakilala na njaa, wambie maisha hayazidi miaka 120 na hakuna atakayeondoka na kitu.

Tunapoadhimisha nia tukufu za waasisi Wa Nchi yetu tujiweke kwenye mzani tujipime baada yetu yepi yataubeba uwepo wetu.

Umewahi kusema nafasi hii umeruzukiwa na Mungu. Ni kweli wewe kama wewe usingeshinda uchaguzi ule, ( huu no mtazamo wangu) kama ndivyo Mungu aliandaa kusudi jema kwako na kwa Nchi yetu Msikilize Yeye.

Amekuweka ili uivushe Tza ng'ambo ya mafanikio usisahau usipofanya maagizo yake Mungu ni mkali mno.
 
Kwa dalili za uchumi wa dunia unavyoporomoka ni wazi kabisa tunakoelekea ni kubaya kama sio mwisho wa maisha basi ni dalili za mwisho wa dunia.

Yanayotokea huko majuu ya kwamba sasa hata mtu akitaka kununu nyanya za Tanzania anunue kwa kutumia shiling ya Tanzania, sio dalili nzuri, mafuta ya petrol ya kutoka Urusi kwa sasa yapo bei chee, ila uyanunue kwa kutumia hela ya Urusi hawataki tena upumbavu wa kutumia dola.
 
1649310655885.png
 
WAKUBWA WA DUNIA KUNA KITU WANAKISET SIO BURE, UKUTE HATA HIYO VITA NI SEHEMU YA MPANGO HUO
 
Kila Nchi iuze na kununua kwa kutumia pesa za Nchi yake! Thamani ya pesa itokane na Mali asili za Nchi husika. Dunia iachane na Dola!! Dola ya marekani itumiwe na Marekani tu!
 
Tatizo kila Mmoja anataka kumtawala mwenzake
Ni suala la kuamua kuigomea Marekani. Wazungu wa ulaya ni Kama watumwa wa Marekani kwa Sasa! Wanaiabudu Marekani kwa kuona Marekani ndiye mlinzi wao dhidi ya kitisho bandia Cha Urusi!!

Kimsingi Urusi si tishio la ulaya Kama usipoiwekea mazingira ya kuhatarisha usalama wake!

Marekani ndio anapenda kuweka mazingira ya kuhatarisha usalama wa Urusi Ili kuwafanya wazungu waendelee kumhitaji!!
 
Tuliwekeza kwenye siasa badala ya miundombinu ya vitu kama mafuta sasa tunataabika
Na hiki ndo kinaigharimu nchi hii hadi leo, kujikita kwenye masiasa siasa tu na uswahili swahili. Nyerere alifanya miscalculation kuondoa lugha na mfumo wa kiingereza na kuleta uswahili na siasa, leo tungekuwa tumeipiga Kenya gap la maana tunachuana na nchi kama Nigeria na SA kwenye uchumi mkubwa.
 
Mama Mpendwa Shalom

Mwenendo uliopo mpaka sasa, japo tunakupongeza kila kona kwamba unaupiga mwingi mambo ni magumu.

Hawa walioko vijijini ambao ndo hasa wapiga kura wako hawajui habari ya Ukraine na Putin wao, wanachokihitaji wapate maisha ahueni, wakati nchi nyingi zilizoathirika kama sisi zinajipanga kutenga ruzuku ya kugharamia mfumuko wa bei ya mafuta sisi tunaibandika ilivyo na hata wabunge wengine wanalalama ati Waziri ameondoa tozo.

Mama mahali penye njaa na mateso hapawezi kuwa na amani. Ongezeko zaidi ya ya asilimia 50% ya diesel toka umeshika madaraka hata kama linasababishwa na external forces lazima njia mbadala za kulegeza nati litafutwe.

Najua unao washauri wengi Wazuri Wa uchumi na siasa lakini nikuombe Mama yetu iangalie Tanzania, kiangalie Chama chetu CCM wengine wanaweza kukushauri kwa maslahi binafsi watu wengi wakaumia.

Huyo mama unayemtetea kila siku anayeuza mbogamboga alikuwa analipa tsh 500 kupanda bajaji Jana bei imepanda nauli Tsh 1000/- tumemrudisha nyuma sana. Usifurahie akina mama hao na madira yao wapiga iyenaiyena "mama anaupiga mwingi" wengine wanafiki tu na wengi wao hawajui machungu ya mama Wa kijijini ambaye bado anaishi kwa Jembe la mkono.

Punguza gharama za uendeshaji wa serikali yako tenga ruzuku ya mbolea na mafuta na kupigania bei za mazao ya wakulima wetu wanyonge, pambana reli zikamilike haraka ili kupunguza matumizi ya fedha za kigeni zinazonunua mafuta, kile kitengo cha kukusanya dhahabu zetu ili kuwa na reserve itakayotusaidia kubalance currency yetu kiangalie vizuri.

Lakini usiache kuwa mhubiri kwa hao wanaojikusanyia huku wengine wakilala na njaa, wambie maisha hayazidi miaka 120 na hakuna atakayeondoka na kitu.

Tunapoadhimisha nia tukufu za waasisi Wa Nchi yetu tujiweke kwenye mzani tujipime baada yetu yepi yataubeba uwepo wetu.

Umewahi kusema nafasi hii umeruzukiwa na Mungu. Ni kweli wewe kama wewe usingeshinda uchaguzi ule, ( huu no mtazamo wangu) kama ndivyo Mungu aliandaa kusudi jema kwako na kwa Nchi yetu Msikilize Yeye.

Amekuweka ili uivushe Tza ng'ambo ya mafanikio usisahau usipofanya maagizo yake Mungu ni mkali mno.
ndugu yangu tangu lini ccm akamjali mtanzania? Wote wapo kwa maslahi yao na familia zao na vizazi vyao.
 
Back
Top Bottom