Rais Samia: Fedha ambazo zingegharamia Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zigawanywe sawa

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,050
4,903
Dodoma!

Akizungumza Leo katika kongamano la Muungano jijini Dodoma, Makamu wa Raisi Dr . Philip Mpango amesema Raisi Samia Suluhu Hassan ameelekeza Fedha zilizotakiwa kutumika katika shughuli za maadhimisho ya miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zigawanywe pande hizo mbili (Tanganyika na Zanzibar) ili zikafanye shughuli za maendeleo!

Dk. Philip Mpango ametumia takribani dakika 20 kuhutubia wanakongamano na Kisha kuondoka ili aendelee na shughuli zake za Kila siku za kulijenga taifa!

IMG_4248-768x905.jpg

TAREHE 26 Aprili, 1964 Mataifa mawili haya ya Jamuhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar yalioungana na kuunda Taifa jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo badae ikabadilishwa na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo kila mwaka ifikapo Aprili 26, tunakumbuka siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo mwaka huu Muungano huu unatimiza miaka 57, huku ukiwa ni Muungano wa mfano na imara katika Bara la Afrika na ulimwenguni pote.
 
Ila kama Serikali haina mpango wa kuadhimisha Sherehe za Muungano, kwanini wanatenga bajeti yake kila mwaka?

Kwanini fedha hizo in a first place zisipangiwe shughuli za maendeleo badala ya kuja kuzibadilishia gia angani ilhali kuna vifungu vingi tu vya muhimu vinakosa bajeti katika wakati wa kupanga.
 
Salaam

Makamu wa Rais Mteule, Dkt. Philip Isdor Mpango, amesmea kuwa, Rais Samia kaagiza fedha zilizotengwa kugharamia Sherehe za Muungano, amezibadilishia matumizi na kuagiza zigawanywe sawa kwa bara na Visiwani.

Pia kasema kila upande utajiamulia matumizi ya fedha hizo.
 
Mama kaanza vizuri; baadhi ya mambo yaliyofanya JPM awe kwenye mioyo ya watu ni maamuzi kama haya.

Sherehe za Uhuru na Muungano ni sherehe muhimu sana katika historia ya nchi yetu, na ni muhimu zitengewe budget.

Lakini matumizi ya hizo pesa inabidi yafanye kitu cha maana kitakachosaidia watu wengi badala ya kuliwa na wale wajanja wajanja wa mujini kwa kukodi vihema, vicocktail, kuweka mafuta mashangingi, n.k.
 
Na bado lazima mwanakwerekwe kuwe kama chato
Tulijua tu kwa kuapishwa mama samia kuwa Rais wa JMT wenye chuki na maendeleo ya Zanzibar watanyoosha vidole tu, hawa ndio wanafiki ambao siku zote huitazama Zanzibar kwa udogo wake lakini siku zote hawako tayari kuiacha Zanzibar isimame kwa miguu yake pamoja na kwamba Tanganyika iliungana na nchi ya Zanzibar kwa hiyari zake.
 
Labda niulize kuwa pesa za gharama za Muungano huwa zinatoka wapi au kwa utaratibu gani.

Pili, je Zanzibar kuna pesa ambayo wanachangia kwenye Muungano kusema sasa warudishiwe sehemu?

Kinyume na hapo Tanganyika haipaswi iendelee kuifadhili Zanzibar. Otherwise tuambiwe kuwa nao Zanzibar kuna pesa huwa wanachangia huku kwetu.

Mh Rais asitake sasa kuwa nyonya wabara kwa jasho lao kupafaidisha kwao. Haya ndo madhara ya kuwa na Rais kutoka Zanzibar. Kama kuna sehemu anaona Zanzibar wananyonywa aseme wazi na hiyo mianya izibwe.

Lakini siyo sisi huku tupigike halafu jamaa wawe wanakula tende na urojo tu mwisho wa siku wapate pesa zetu.
 
Back
Top Bottom