robinson crusoe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2020
- 740
- 1,214
Mimi ni mwalimu wa miaka mingi. Nina mates wangu wengi ktk taaluma ya ualimu mikoa mingi ya nchi hii. Hii siyo mara ya kwanza kuwa na ujenzi wa madarasa, tatizo ni ubora duni unaotokana na wizi wa watendaji wakuu wilayani na halmashauri. Wizi mkubwa ni wa Sementi, mbao na mabati kiasi kwamba sakafu hugeuka vumbi ktk kipindi cha mwaka mmoja tu!
Sasa wizi umeanza, Ninapowasiliana na waalimu wenzangu ktk mikoa 10 ambayo nina mawasiliano nao; Kigoma, Mwanza, Mara, Singida, Lindi, Morogoro, Manyara, Singida, simiyu na Katavi wote wanaeleza kupigiwa simu na maafisa elimu na tayari pesa zimeliwa wakisema pia zinahitajika na wakuu wa wilaya. Mkoa wa kigoma wameanzisha mtindo wa kuziba pengo kwa kuwatumia wanafunzi kama vibarua wa ujenzi huo hadi kuponda kokoto na kukoroga zege.
Mwanza wao wanadai nguvu ya wananchi itumike ili kuunga mkono msaada wa serikali. Kwa mtindo huu rais usitegemee lolote la maana. Huku wilayani huna wasimamizi, ni wezi tu!
Sasa wizi umeanza, Ninapowasiliana na waalimu wenzangu ktk mikoa 10 ambayo nina mawasiliano nao; Kigoma, Mwanza, Mara, Singida, Lindi, Morogoro, Manyara, Singida, simiyu na Katavi wote wanaeleza kupigiwa simu na maafisa elimu na tayari pesa zimeliwa wakisema pia zinahitajika na wakuu wa wilaya. Mkoa wa kigoma wameanzisha mtindo wa kuziba pengo kwa kuwatumia wanafunzi kama vibarua wa ujenzi huo hadi kuponda kokoto na kukoroga zege.
Mwanza wao wanadai nguvu ya wananchi itumike ili kuunga mkono msaada wa serikali. Kwa mtindo huu rais usitegemee lolote la maana. Huku wilayani huna wasimamizi, ni wezi tu!