Kikwete amejenga kijiji kizima kwao Msoga kwa pesa ya IKULU na akajengewa nyumba nyingine pale Migombani ambayo alinunua kwa bei poa na zaidi ya hayo yote ana nyumba nyingine anayodanganya kuwa amepanga hapo Msasani na sasa amejengewa nyumba nyingine huko Masaki ufukuweni!!! Mtu huyo huyo mmoja na nyumba zote hizo za nini?Hata Mzee kupokea na kuridhika inaleta ukakasi.
Mwalimu Julius asingepokea na angewashangaa sana kwa hicho wanachokifanya.
Angekuwa ni mtu wa busara kawavile ana nyumba ya hadhi yake,angekataa kupewa hiyo nyumba na kuomba hizo fedha ambazo zingetumika kumjengea zielekezwe kwenye maendeleo ya kwao Chalinze!! Lakini kwasababu ya ubinafsi hawezi kuwa na mawazo hayo!!! Viongozi wetu ni walafi wanaowatumia wananchi wao kujijengea ufalme!!