#COVID19 Rais Samia azindua Kampeni ya Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya COVID-19 Jijini Dodoma

Baraka Mina

JF-Expert Member
Sep 3, 2020
581
574
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. Samia Suluhu Hassan akizindua kampeni ya maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO - 19 katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo 10 Oktoba 2021.​

Fuatilia matangazo hapa




Dondoo ujio wa Shilingi Trilioni 1.3 kutoka IMF.
1. Kujenga madarasa mapya 15,000 ya sekondari.
2. Kujenga madarasa 3,000 shule za msingi shikizi
3. Kutengeneza madawati 462,795
4. Kumalizia vyuo vya VETA 32
5. Magari 25 ya kuchimba visima vya maji.
6. Mitambo 5 ya kujenga mabwawa ya maji.
7. Kujenga ICU 72
8. Magari ya wagongwa (Ambulance) 395 na ya chanjo 214
9. Mifumo ya Oxygen hospitali 82
10. Mitungi ya gesi 4,640
11. Mitambo ya kuzalisha hewa ya Oksijeni 40.
12. Vitanda vya wagonjwa 2,700
13. Xray za kisasa 85
14. CT- Scan 29
15. MRI hospitali zote za kanda

Rais Samia Suluhu Hassan

Kwenye kipindi cha miezi sita tumeweza kutatua changamoto 11 za Muungano ikiwemo masuala ya usimamizi wa ukokotoaji na ukusanyaji wa kodi za huduma za simu unaofanywa na Mamlaka ya Mapato Zanzibar, Sheria ya Uvuvi kwenye ukanda wa uchumi wa bahari kuu pamoja na suala la ucheleweshaji wa mikataba mbalimbali ya miradi ya maendeleo

Hakuna shaka kutatuliwa changamoto hizo kumeimarisha muungano wetu.

Kwenye hotuba yangu tarehe 22 Aprili nilitaja baadhi ya hatua tulizopanga kuzichukua ili kukuza uchumi ikiwemo kuhakukisha viashiria vyote vya uchumi jumla vinabaki kuwa imara. Kutathmini mifumo, taratibu na viwango vya kodi, kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, kuimarisha ukusanyaji wa mapato. Nfarijika kuwa katika miezi 6 iliyopita, tumetekeleza hayo yote.

Uchumi umeongezeka hadi kufikia asilimia 4.3 ukilinganisha na asilimia 4 kipindi kama hicho mwaka uliopita

Tumedhibiti mfumuko wa bei ambapo umeendelea kuwa na tarakimu moja. Katika kipindi cha mnwezi Aprili hadi Septemba 2021 mfumuko wa bei ulikuwa kwa wastani wa asilimia 4. Hadi mwezi Agosti 2021 akiba ya fedha za kigeni ilifikia dola za Marekani bilioni 5.8 iliyotoshelea kuagiza bidhaa kwa kipindi cha miezi 6 ikilinganishwa na akiba ya dola za Marekani bilioni 4.9 iliyokuwa kipindi kilichopita.

Hali ya ukusanyaji wa mapato inakwenda vyema. Kuanzia Aprili mpaka Septemba tumakusanya trilioni 9, bilioni 905, na mapato yasiyokuwa ya kodi yalikuwa Tshs. Trilioni 1 bilioni 436

Tumrefanikiwa kupata mikopo ya masharti nafuu yenye thamani ya Tsh. Trilioni 1 bilioni 447.

Katika kipindi hicho tumetuliza kilio cha muda mrefu cha kufanya marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani, yaani VAT Refund. Kiasi cha bilioni 451 na milioni 300.

Tumeendelea kulipa madeni ya ndani na je. Tumeweza kumaliza uhakiki wa madeni ya ndani yanayofikia shilingi bilioni 439 yanayotokana na madai ya watumishi, wazabuni wakubwa na wadogo, wakandarasi wakubwa, madeni ya huduma za umeme maji na simu kwa taasisi za umma

Madeni yote hayo yameanza kulipwa na yanaendelea kulipwa. Kazi ya uhakiki wa madeni yaliyobaki inaendelea.

Kuhusu uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji na biashara, hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwemo ikiwemo kuondoa urasimu kwenye utoaji wa vibali vya kazi ambapo tumeanzi mfumo wa kielektroniki, yaani e-permit. Mfumo huu umepunguza siku za utoaji vibali kutoka siku 14 hadi siku moja kwa sasa endapo mwombaji atakuwa amekamilisha taratibu zote.

Katika Miezi 6 iliyopita tumeshughulikia maslahi ya Wafanyakazi kwa kuwaajiri wapya, kuwapandisha madaraja na kubadili kada

Pia tumewapa unafuu kwa kupunguza Kodi ya Mapato(PAYE). Tumetenga Tsh. Bilioni 20 zinazoenda kuongeza nguvu kwenye TASAF

Tumeanza mradi wa kushughulikia matatizo ya Machinga, mradi huu utaenda kujenga masoko kwa ajili yao

Pori la akiba la Selou limebaki chini ya mfumo wa Urith wa Dunia ambapo linaendelea kufaidika na misaada ya mfuko huo

Kuanzia Mwezi Desemba 2021 Wasanii wataanza kupokea mirabaha kutokana na kazi zao

Sanaa imeajiri Vijana wengi Nchini na kusaidia kukua kwa uchumi

Sitaki utitiri wa kamati. Ili kuwa na uwajibikaji ziundwe kamati za kimkoa ambazo zitashughulika na mradi huu wa maendeleo kwa Wananchi

Kwa wanaotaka kuzijua rangi zangu halisi, wajaribu kudokoa pesa hizi au wabadilishe matumizi

Kwenye fedha hii ya miradi ya maendeleo ya Taifa sitakuwa na huruma na Mtu

Kuanzia kwa Mawaziri wangu hadi chini kwa Wananchi. Kwa hiyo mkasimamie miradi kwa uadilifu

Natoa wito kwa Wananchi na Watumishi wa Umma mkiona kuna shida katika mpango huu wa maendeleo, mtoe taarifa ili tuweze kuchunguza na kuchukua hatua
 
Walishaanza kutapanya pesa za msaada toka kwa Mabeberu kuhusu korona, Naona wameanzisha tamasha ili kuwahadaa mabeberu kuwa pesa walizopata za IMF wanachukua hatua

Danganya toto Jinga

Sasa mbona jambo la kitaifa na la kiserikali limegeuzwa la chama

Haya mambo yanachekesha sana na yanarudisha nyuma sana hamasa na maendeleo

Meza zimewekwa bendera ya CCM na baadhi ya watu wamevaa sare za ccm

Kuna watu wakisikia neno ccm wanazima TV na kuondoka, Hawaitaji porojo na uwongo wa CCM

Unapohimiza mambo ya kitaifa kama chanjo, Kampeni za malaria, Kampeni za watu kuwa matajiri, Au kampeni za elimu yakupasa kusimamia Sera za Taifa

Watu ambao hawana chama ni wengi kuliko wana ccm au Chadema

CCM walisema tuchape kazi Corona hakuna na waliwacheka Chadema waliohimiza kuwa corona ipo na itaondoka na watu ikiwemo viongozi

Leo CCM inapiga kampeni ya chanjo ni wajinga waliopindukia na watu wasiojitambua wanaweza Sikiliza ujinga huu

Nashauri viongozi waombe radhi wananchi kwa kuwajaza upepo kuwa korona hakuna na ni kama mafua ya ndege

Humprey Polepole bado anahubiri hakuna korona na amesimama na msimamo wa ccm

Sasa Je Pesa za IMF zimetumikaje?

Mtuambie pesa mlizopata za IMF mmeajiri madaktari wangapi kama mkataba unavyotaka

CCM wanahubiri mapambano ya corona, Pathetic

CCM mlikuwa wapi mmesubiri mpaka watu wameondoka, Mlihimiza Bunge liendeleee na waliotoka bungeni wakatwe pesa
 
Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO - 19) upo na si janga letu pekee bali dunia nzima.
Ndio nauliza kweli tupo serious kabisa tunapambana nao ? Au tunafanya sarakasi ili kukidhi matakwa ya kupokea misaada ? Vyombo vya usafiri vinajaza nyomi kama kawaida, viwanja vya michezo, kkabu,bar...sioni mtu anayehangaika na UVIKO-19 kwa sasa
 
Back
Top Bottom