Rais Samia awezesha ndege mpya ya mizigo kutua Aprili

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Rais Samia awezesha ndege mpya ya mizigo kutua Aprili.

Na Bwanku Bwanku.

Ndege mpya ya mizigo iliyoagizwa na Serikali ya Tanzania kutoka nchini Marekani inatarajiwa kupokewa nchini mwezi Aprili mwaka huu ili ianze mara moja kuendelea kufungua uchumi wa Taifa kupitia usafarishaji wa mizigo kutoka Nje ya Nchi.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa wadau wa ATCL, Msajili wa Hazina Nehemia Mchechu amesema huu ni mwendelezo wa Serikali kuweka mazingira mazuri ya usafirishaji wa mizigo na kuwarahishia Wafanyabiashara kusafirisha mizigo yao hasa kwa kuzingatia kwasasa usafirishaji wa mizigo unafanyika kwa kutumia ndege za abiria.

Mchechu amesema ndege hiyo aina ya Boeing 767-300F ina uwezo wa kubeba tani 54 kwa mpigo wa mara moja na kutatua changamoto kubwa ya usafirishaji mizigo kwa Wafanyabiashara nchini ambao mara nyingine wamekuwa wakipata shida sana kusafirisha mizigo kutoka nje.

"Tuishukuru Serikali ya awamu ya 6 kwa uwekezaji huu mkubwa unaozidi kufanyika kwenye Shirika la ndege la Tanzania kwa kuleta ndege ya mizigo kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Chama kinachoongoza Taifa (CCM) na kwenye Mipango ya Nchi pamoja na ndege nyingine mpya ambazo inajiandaa kuleta. Uwekezaji huu unaifanya ATCL kuwa Shirika kubwa la ndege nchini na Afrika Mashariki na kuendelea kulikuza zaidi ukanda mzima wa Kusini kwa Afrika (SADC)." Alisema Mchechu.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amesema ndege hii ni kubwa na ya kisasa sana na kwa kuanzia kwa kipindi cha miezi miwili hadi sita wataanza kwenda kwenye nchi ambazo wamejijenga sana kwenye masoko ikiwemo China, India pamoja na kwenye nchi ambazo zimekuwa zikitumia sana bandari ya Dar es Salaam kupakua mizigo yao kama Congo, Zimbabwe, Comoro na kadhalika huku wakijipanga kwenda nchi zingine zilizojijenga kimasoko hivi karibuni kama Dubai.

FB_IMG_1679639624182.jpg
FB_IMG_1679639626463.jpg
FB_IMG_1679639628426.jpg
 
Bado mnanunua ndege kama mnavyonunua mbuzi? Najua kuwa mnanunua tu kwani JPM alishalipia advance na hakuna namna. Haya ni moja ya makosa ya hayati ambayo nchi haina budi kuyaendeleza angalau kwa kitambo kidogo. Ila ukweli itabaki palepale kuwa, kama nchi tunakula hasara kutokana na uwekezaji huu mgumu hata kwa mataifa kama Africa Kusini, Kenya na hata mataifa ya Ulaya.
 
Rais Samia awezesha ndege mpya ya mizigo kutua Aprili.

Na Bwanku Bwanku.

Ndege mpya ya mizigo iliyoagizwa na Serikali ya Tanzania kutoka nchini Marekani inatarajiwa kupokewa nchini mwezi Aprili mwaka huu ili ianze mara moja kuendelea kufungua uchumi wa Taifa kupitia usafarishaji wa mizigo kutoka Nje ya Nchi.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa wadau wa ATCL, Msajili wa Hazina Nehemia Mchechu amesema huu ni mwendelezo wa Serikali kuweka mazingira mazuri ya usafirishaji wa mizigo na kuwarahishia Wafanyabiashara kusafirisha mizigo yao hasa kwa kuzingatia kwasasa usafirishaji wa mizigo unafanyika kwa kutumia ndege za abiria.

Mchechu amesema ndege hiyo aina ya Boeing 767-300F ina uwezo wa kubeba tani 54 kwa mpigo wa mara moja na kutatua changamoto kubwa ya usafirishaji mizigo kwa Wafanyabiashara nchini ambao mara nyingine wamekuwa wakipata shida sana kusafirisha mizigo kutoka nje.

"Tuishukuru Serikali ya awamu ya 6 kwa uwekezaji huu mkubwa unaozidi kufanyika kwenye Shirika la ndege la Tanzania kwa kuleta ndege ya mizigo kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Chama kinachoongoza Taifa (CCM) na kwenye Mipango ya Nchi pamoja na ndege nyingine mpya ambazo inajiandaa kuleta. Uwekezaji huu unaifanya ATCL kuwa Shirika kubwa la ndege nchini na Afrika Mashariki na kuendelea kulikuza zaidi ukanda mzima wa Kusini kwa Afrika (SADC)." Alisema Mchechu.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amesema ndege hii ni kubwa na ya kisasa sana na kwa kuanzia kwa kipindi cha miezi miwili hadi sita wataanza kwenda kwenye nchi ambazo wamejijenga sana kwenye masoko ikiwemo China, India pamoja na kwenye nchi ambazo zimekuwa zikitumia sana bandari ya Dar es Salaam kupakua mizigo yao kama Congo, Zimbabwe, Comoro na kadhalika huku wakijipanga kwenda nchi zingine zilizojijenga kimasoko hivi karibuni kama Dubai.

View attachment 2563584View attachment 2563585View attachment 2563586
Nakumbuka Rais Samia Suluhu alisema ataifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara naona anaendelea kutimiza lengo lake safi sana
 
"Tuishukuru Serikali ya awamu ya 6 kwa uwekezaji huu mkubwa unaozidi kufanyika kwenye Shirika la ndege la Tanzania kwa kuleta ndege ya mizigo kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Chama kinachoongoza Taifa (CCM) na kwenye Mipango ya Nchi pamoja na ndege nyingine mpya ambazo inajiandaa kuleta. Uwekezaji huu unaifanya ATCL kuwa Shirika kubwa la ndege nchini na Afrika Mashariki na kuendelea kulikuza zaidi ukanda mzima wa Kusini kwa Afrika (SADC)." Alisema Mchechu.
120909684_117545516779837_7410527070517376392_n.jpg
 
Kuna warrant ishatolewa ya kuikamata hiyo ndege ya mizigo kufidia deni la kampuni iliyowahi kujenga barabara hapa nchini.
 
Back
Top Bottom