Rais Samia awakaribisha nchini Mawaziri wa michezo wa nchi 14

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
325
414
Na Bwanku M Bwanku.

Leo Alhamisi Mei 04, 2023 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ni mgeni rasmi na atafungua mkutano wa Mawaziri wa Michezo wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya 4 ambapo Mawaziri 14 kutoka Nchi za Comoro, Mauritius, Sudan, Somalia, Madagascar, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Shelisheli, Eritrea, Sudan Kusini, Uganda na mwenyeji Tanzania watashiriki Jijini Arusha kwenye hoteli ya Glan Melia.

Kuelekea mkutano huo mkubwa utakaowakutanisha Mawaziri 14, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za kuwakaribisha Mawaziri hao kwenye mkutano huo mkubwa wa Kanda ambao ni mara ya kwanza unafanyika nchini Tanzania.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo kwenye ukanda huo wa 4 wa michezo wa Umoja wa Afrika na namna ya kuboresha michezo zaidi.

 
Nilijua mawaziri wa uwekezaji.
Nasikia tumeomba kuandaa AFCON na wenzetu, ni miji/viwanja vipi ambavyo sisi tunaweza kupata "A" kwenye ukaguzi wa CAF!!???
 
Na Bwanku M Bwanku.

Leo Alhamisi Mei 04, 2023 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ni mgeni rasmi na atafungua mkutano wa Mawaziri wa Michezo wa Baraza la Michezo la Umoja wa Afrika Kanda ya 4 ambapo Mawaziri 14 kutoka Nchi za Comoro, Mauritius, Sudan, Somalia, Madagascar, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Shelisheli, Eritrea, Sudan Kusini, Uganda na mwenyeji Tanzania watashiriki Jijini Arusha kwenye hoteli ya Glan Melia.

Kuelekea mkutano huo mkubwa utakaowakutanisha Mawaziri 14, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za kuwakaribisha Mawaziri hao kwenye mkutano huo mkubwa wa Kanda ambao ni mara ya kwanza unafanyika nchini Tanzania.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo kwenye ukanda huo wa 4 wa michezo wa Umoja wa Afrika na namna ya kuboresha michezo zaidi.

View attachment 2609592
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom