CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,984
- 4,083
Maajabu ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Tanzania imeagiza Jumla ya ambulance mpya 395 na magari mapya 214 kwa ajili ya chanjo kwa mpigo kitu ambacho hakijawahi kufanyika tangu tuwe huru kama Taifa,
===Mtakumbuka awamu ya tano kwa miaka yote mitano tulifanikiwa kununua jumla ya ambulance 117,
Maajabu ni haya ya awamu hii ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwani tayari tumeagiza ambulance zingine brand new 395 na magari ya Chanjo 214 mapya,
Mambo haya yanafanywa na Rais anayethamini na kulinda Utu na Uhai wa Watanzania wote bila kujali dini, kabila, rangi wala kanda,
Rais Samia Suluhu kwa kutumia fedha ya kusisimua uchumi Economic Stimulus relief fund toka IMF,
Tayari ameagiza zinunuliwe Jumla ya Toyota Land cruiser ambulance mpya 395 pamoja na magari mapya 214 kwaajili ya Chanjo aina zote 15 ikiwemo chanjo ya Covid-19,
Nahapa lazima niwe mkweli kama mambo ni haya basi kumbeza Rais Samia Suluhu Hassan nikujitafutia laana za bure kwa Mungu kwani kazi hii ni ya Mungu mwenyewe,
Mtakumbuka awamu yetu ya tano katika kutekeleza Ilani ya CCM tulifanikiwa kununua Toyota Land cruiser ambulance mpya 117 kwa miaka mitano,
Hayati Dkt John Joseph Magufuli kwa kutununulia hizo ambulance lazima tuendelee kumuenzi na kumwombea pumziko jema,
Kwakuwa Tanzania tuna jumla ya Wilaya 139 na zote zina hospitali za Wilaya,
Wilaya zote baada ya hizi ambulance kufika kila Hospitali ya wilaya itapata ambulance mpya ( brand new) kwaajili ya kunusuru roho za Watanzania hawa masikini kwa kuwakimbiza kwenye hospitali za juu (referral hospitals).
Kwakuwa Tanzania pia tuna jumla ya Halmashauri zipatazo 184 ,
Nakwakuwa hesabu ya ambulance zilizoagizwa ni 395 basi kila halmashauri itapata ambulance mpya,
Ambulance hii mpya itakuwa ni kwaajili ya kuhudumia ama Kituoa cha afya ama Zahanati kwaajili ya rufaa za wagonjwa wao kwenda hospitali za Wilaya na Mikoa,
Watu wa Idara ya afya tunzeni sana mali hizi za Watanzania hawa masikini.
Ambulance hizi 395 ni mara tatu zaidi ya ambulance zote 117 zilizonunuliwa kwa miaka mitano yote ya awamu ya tano,
Jambo hili kwa Wale wenye kumbukumbu nzuri mtakubaliana na mimi kuwa hii halijawahi kutokea katika historia ya nchi hii,
" kama kuna mtu wa kumwombea kwa nguvu zote kwa sasa basi ni Rais Samia Suluhu Hassan "