Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,874
Akizungumza baada ya kurejea Nchini Tanzania kutoka Marekani, amesema Watanzania wategemee matunda kutoka Filamu ya TheRoyalTour na Nchi ijitayarishe kupokea wageni wengi
Amesema Fedha za kutengeneza Filamu hiyo zimetokana na michango ya Wafanyabiashara mbalimbali Ndani na Nje ya sekta ya Utalii iliyoanguka kidogo kutokana na mlipuko wa COVID19
Aidha, Rais Samia amesema akiwa ziarani amezungumza na Serikali ya Marekani na kunyoosha pale palipokuwa na changamoto, akisema "Sasa tupo vizuri, tunaenda nao vizuri sana"
Mambo zaidi aliyoongea Rais Samia.
Rais Samia Suluhu Hassan: Uhusiano wa Tanzania na Marekani umetimiza miaka 60 mwaka 2021. Zamani tulikuwa zaidi kunyoosha mikono, tunaomba hiki na kile
Lakini sasa tumekubaliana pamoja na kwamba hayo yatakuwepo, uhusiano mkubwa ni Uwekezaji na Biashara
Rais Samia: Tulifanya mazungumzo na Mashirika ya Fedha ya Kimataifa (Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani), tumekubaliana vizuri
Fedha kama ile tuliyoleta na kuipeleka kwenye Vituo vya Afya na Madarasa, tunatarajia kuna nyingine itakuja iende kwenye maendeleo
Rais Samia: Kuna kundi lilienda kufanya Mkutano na Meya wa Jiji la Dallas, na matokeo ya Mkutano ule ni kwamba wenzetu wamekubali na wana hamu wafanye undugu na Miji yetu
Tunaangalia uwezekano wa kuwa na ndege zitakazotoka moja kwa moja Dallas mpaka Tanzania kuleta wageni
Rais Samia: Katika mazungumzo yetu na Wafanyabiashara wa Marekani tumesaini mikataba ya makubaliano ya miradi ya kuja kuwekeza Tanzania, thamani tuliyopiga ilifikia Trilioni 11.7
Kazi ni kwetu kuwapokea hawa watu bila usumbufu na kufanya uwekezaji wao uwepo Tanzania