MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,734
Kwangu mimi kutokana na Tuhuma zao (hasa walipokuwa katika Nyadhifa zao) namfananisha Ole Sabaya ni Papa na Paul Makonda ni Nyangumi.

Unatoaje amri ya kuchunguzwa kwa Papa Ole Sabaya na ukamuacha Nyangumi Paul Makonda? Hapa Rais Samia Mimi Krav Maga sijakuelewa

Rais Samia tafadhali hakikisha na hiki ulichokifanya kwa Ole Sabaya pia ukifanye kwa Paul Makonda kwani ana Madhambi yaliyomshangaza hata Shetani.
 
Kubwa la maadui "Hon Paul Makonda" tumbo la kuharisha limemshika huko alipo.

Eid hii kuna watu watailia Mzena Hospital na drip za glucose mikononi ku stabilize BP.

Hawa viongozi waliopewa nyadhifa kutuongoza walitufanya tuishi kama tumbili ndani ya nchi yetu, unaamka asubuhi unasali kwa dini zote ili usiingie kwenye mikono yao ukapotezwa, sasa muda wao kuishi kama ngedele mamaqxe.
 
Huwezi kuwafananisha kwani Makonda hayuko serikalini na huyo Sabaya alikuwa mtumishi wa serikali!
Makonda hayuko Serikalini sasa ila je, huko nyuma hakuwa Serikalini huko?

Kwahiyo Tuhuma za Mtumishi wa Serikalini huwa zinayeyuka pale akitoka Serikalini?

Kuna Waziri nchini Uingereza amestaafu miaka 17 iliyopita ila alikamatwa kujibu Tuhuma zake.

Nionyeshe ni wapi katika Katiba ya Tanzania inazuia Mtumishi aliyetoka Serikalini asihojiwe.

Kuna Watu mna Akili za hovyo hovyo tu.
 
Kwangu Mimi kutokana na Tuhuma zao ( hasa walipokuwa katika Nyadhifa zao ) namfananisha Ole Sabaya na Papa na Paul Makonda ni Nyangumi.

Utoaje AMRI ya Kuchunguzwa kwa Papa Ole Sabaya na ukamuogopa au ukamuacha Nyangumi Paul Makonda? Hapa Rais Samia Mimi Krav Maga sijakuelewa.

Rais Samia tafadhali hakikisha na hiki ulichokifanya kwa Ole Sabaya pia ukifanye kwa Paul Makonda kwani ana Madhambi yaliyomshangaza hata Shetani.
Taratibu basi!!!

Hata kama angekuwa na nia ya kufanya kama hayo unayo mshauri ayafanye, mbona papara hivyo?

Wewe ungekuwa kiongozi ungesumbua sana, huenda hata Mwenda zake angekuwa nafuu kuliko wewe!
 
Kwani kuchunguzwa maana yake ni kukamatwa?
Sikutegemea kama unayejiita Great Thinker ungeuliza Swali la Kipumbavu sana hili.

Yaani hujui kuwa kutokana na Tuhuma zako unaweza Kuchunguzwa ukiwa under House arrest au ukiwa ndani Polisi?

Wakati Akili zinagawiwa kwa Watu ( akina Krav Maga ) na Mwenyezi Mungu Mwenzetu ulikuwa wapi labda? Nimekudharau kuliko...!
 
Kuna Watu mna Akili za hovyo hovyo tu

Hoja hapa ilikuwa Rais awachukulie hatua wengine kama alivyomchukulia Sabaya ya kuwasimamisha kazi wote kwa pamoja na ndipo likatajwa jina la Makonda!! Hapo ndipo tukabainisha kuwa Makonda hayupo tena serikalini hivyo sio rahisi kumchukulia hatua ya kumsimamisha!!

Suala la kuhojiwa kwa matendo yake alipokuwa RC na kama alivunja sheria hilo liko chini ya taasisi husika na sioa kazi ya rais kuwaambia nini cha kufanya kwani sheria ndio inayochukua mkondo wake!
 
Taratibu basi!!!

Hata kama angekuwa na nia ya kufanya kama hayo unayo mshauri ayafanye, mbona papara hivyo?

Wewe ungekuwa kiongozi ungesumbua sana, huenda hata Mwenda zake angekuwa nafuu kuliko wewe!
Nasisitiza Rais Samia Suluhu Hassan aamuru upesi sana aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda ( Daud Albert Bashite ) nae akamatwe na achunguzwe kwa Tuhuma zake ambazo ni zaidi ya alizonazo DC Ole Sabaya. Acha Unafiki Hopeless mkubwa Wewe sawa?
 
Hoja hapa ilikuwa Rais awachukulie hatua wengine kama alivyomchukulia Sabaya ya kuwasimamisha kazi wote kwa pamoja na ndipo likatajwa jina la Makonda!! Hapo ndipo tukabainisha kuwa Makonda hayupo tena serikalini hivyo sio rahisi kumchukulia hatua ya kumsimamisha!!

Suala la kuhojiwa kwa matendo yake alipokuwa RC na kama alivunja sheria hilo liko chini ya taasisi husika na sioa kazi ya rais kuwaambia nini cha kufanya kwani sheria ndio inayochukua mkondo wake!
Hebu acha kunipotezea Muda tafadhali.
 
39 Reactions
Reply
Back
Top Bottom