Rais Samia atengua uteuzi wa Albert Chalamila RC Mwanza, Dkt. Batilda ateuliwa kuwa RC Tabora

Ally Happy ni kiongozi was kisiasa katika nafasi ya R.C, lakini amekwisha kabisa kisiasa na huku saiti kila mtu anam-ng'ong'a, huu ni mzigo Mh. Rais, usikubali kuubeba...
Vijana wa mzee Kikwete mpo kazini Awamu hii.

Mnamfanya atazamwe vibaya na watu wasiopenda siasa za kipumbavu za makundi.
 
Kwa kosa lipi wewe..?

Vijana mnawivu Kwa vijana wengine wanapopata vyeo halafu wewe upo tu nyumbani, mnaanza kuwaombea mabaya waliopata kazi ili mlingane, akili za kijinga Sana Hizi na usikute wewe ni mtu nzima na akili zako, kazi yako ni wivu za kikekike, Acha uvivu aliyebarikiwa kabarikiwa tu

Pambafu
Vijana wa aina hii wamejaa mtaani. Wanafanya kazi ya wale wanaopaa na ungo usiku.

Wanaishi maisha ya kishirikina kwa uvivu wao wasiotaka kuushughulikia.
 
Wale vigogo si mna remote maneno ya nini peleke vimemo tu haniu atangaze msituchoshe na insha zenu.
 
Kwani hawa makatibu tawala na wakuu wa mikoa huwa wana mshahara mmoja, manake teua tengua si kila siku watakuwa na mishahara mipya
 
Acheni roho mbaya kila siku kuombea mabaya wenzenu, ukimfanyia mwenzio fitina ikishamaliza kazi kwake, lazima ikurudie, kwani yeye huyo mnaye mwambia ni malaika? Acheni hizo!
 
Ila watz mna roho mbaya sana.
Nadhani Mungu uwa anaangalia nature ya roho zetu kabla hajaamua atulete nchi gani duniani.
Maana ukiangalia tuliozaliwa Africa wote roho zetu ni mbaya.
Isitoshe Happy akiondolewa yeye hapati ,mshahara ulioachwa.Yaan MTU anaandika gazeti.Kumbe ni chuki tu.Nenda kaanzishe business upate pesa.Kuliko kuwazia wengine mabaya.Na namwambia huyu jamaa,kuwa atapoteza vingi kwa kuwa na chuki.
 
Ally Happi kilichombakiza ni UISLAMU wake. Ufisadi aliyofanya Iringa Mungu anajua:
- Wamejenga stendi ya mabasi Iringa mjini kilometa 21 kutoka mjini. Wakalazimisha abiria wote washushiwe huko porini halafu mabasi yaende tupu mjini.

- Maeneo yote karibia na hiyo stendi wamewauzia waarabu wa Iringa na hata hawayaendelezi. Mbele ya stendi wamemuuzia muarabu mwingine ajenge sheli kwa hiyo stendi imefichwa na sheli ya muarabu.

Mateso aliyowaachia abiria wa Iringa wanaotoka mikoani anatakiwa afungwe jiwe zito atupwe ziwa Victoria.

Yaani basi linatoka Mbeya linapita Iringa linaenda kuwashusha abiria kilomita 21 mbele kisha linarudi Iringa tupu, eti ni sheria lazima ukashushwe stendi.

Basi likitoka Dar linafika stendi linashusha abiria wote kisha linaenda mjini tupu. Nauli kutoka Iringa hadi Dar ni elfu 22 halafu nauli kukodi taxi kutoka stendi hadi mjini ni elfu 12. Huu ni zaidi ya unyama!
 
Ukiulizwa Wewe binafsi Ally amekukosea nini utasemaje?

Mwache rais afanye kazi aonavyo yeye, yeye ndio mwenye kujua roles zao hao wateule wake
Jamani watu wanaroho mbaya , wivu unawasumbua ukimfuatilia yeye hata familia yake imemshimda kuongoza, lakini kusagia wengine kunguni tu kila kukicha.
 
Watanzania tuna shida flani tusio ijua wenyewe, akitolewa wewe unapata faida gani, wakati mwingine tuwe tunaona na mazuri na mabaya tupa kule.
 
FB_IMG_16234174098152068.jpg

😂😂😂
 
Ila watz mna roho mbaya sana.
Nadhani Mungu uwa anaangalia nature ya roho zetu kabla hajaamua atulete nchi gani duniani.
Maana ukiangalia tuliozaliwa Africa wote roho zetu ni mbaya.
Sio roho mbaya mkuu,natimiza wajibu wangu wa wa kiraia kuhakikisha viongozi was hovyo wanaondolewa
 
Jamani watu wanaroho mbaya , wivu unawasumbua ukimfuatilia yeye hata familia yake imemshimda kuongoza, lakini kusagia wengine kunguni tu kila kukicha.

Badala mtu apambane ili afanikiwe anapambana ili wenzie waharibikiwe, hii ndio dunia
 
Vijana wa aina hii wamejaa mtaani. Wanafanya kazi ya wale wanaopaa na ungo usiku.

Wanaishi maisha ya kishirikina kwa uvivu wao wasiotaka kuushughulikia.
Mkuu, mwendazake kakuacha kapa, hata cheo cha mwenyekiti kamati ya misiba mtaani hujapata
 
Halafu imekuwa kasumba mbaya sana mtu akipata chochote anaibuka anayekufahamu kuzidi hata mwenyewe unavyojijua

Na ikitokea amepata shida yeye anataka umsaidie sababu mnajuana
Fake ID hizi zimeficha mengi
 
Kama ni kweli huyu alishalewa madaraka.
Mkuu wa mkoa, halafu uwaambie wananchi wampokee Rais kwa mabango ya matusi!
Nini hii jamani?
Tumwache Rais SSH afanye kazi. JPM aliichafua sana serikali.

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
37 Reactions
Reply
Back
Top Bottom