Rais Samia atengua uteuzi wa Albert Chalamila RC Mwanza, Dkt. Batilda ateuliwa kuwa RC Tabora

mambo ya kijinga huwa yanapenda kushikilia vichwa zaidi kuliko yenye tija.

Tugusie bajeti,
mie najikita katika faini za waendesha pikipiki na bajaji, kiufupi naona hizo faini ka hazijasaidia kitu na pili waendesha bodaboda wanajua sheria za barabarani na vyombo vya moto kiujumla ila wengi wanakiuka makusudi, mfano kuambiwa wasipakize mishikaki na wao wanapakiza, yani hilo la mishkaki hata mtoto wa miaka 12 anajua kuwa haitakiwi
Pili swala la kofia ngumu, kila dereva wa pikipiki anajua kuwa inampasa yeye na abiria wake kuvaa hiyo kufia ngumu ila hawavai kwasababu mbalimbali ila zaidi ya 90% ya hizo sababu zao hazina mashiko.

Swala la usalama kwa mtu mmoja mmoja na jamii nzima halihitaji mbwembwe ama siasa flani maana yale ni maisha ya mtu, kitendo cha kushusha hizo adhabu mie sioni kama itawasaidia ila itawafanya waone adhabu hiyo ni ndogo ambako kutawafanya wawe wazembe zaidi ambako kutakuwa na madhara zaidi.

Kitendo cha dereva wa pikipiki kuona adhabu ka ni ndogo na anaimudu kunaweza fanya wale wenye uelewa mdogo kuona ka ndo muda wa kufanya vile waonavyo inafaa kwao
Bajeti kajadili na mkeo. Habari ya mjini ni kutenguliwa kwa Chalamila.
 
Bajeti kajadili na mkeo. Habari ya mjini ni kutenguliwa kwa Chalamila.
sina mkee dadekii, labda nije jadili na mkeo geto kwanguuu ila unajua ishu ya Chalamila bana ka kajitakia mwenyewee so tumwache na akili zake
 
Wewe mwenye akili mbona hatujawahi kuousikia umesimamisha bajeti kupitishwa baada ya wewe na mkeo kuijadili chumbani kwako? Acha kujitukuza wewe.
Usioneshe umbumbumbu wako mbele ya watu namna hii

Ni aibu hata kwa mimi mmeo
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 11 Juni 2021 amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa Mikoa na kuteua viongozi wengine kama ifuatavyo:-

=====

Rais Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza Albert Chalamila, na kumhamishia mkoa huo Mhandisi Robert Gabriel ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Hatua hiyo imetokana na Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko madogo ya wakuu wa Mikoa na kuteua viongozi wengine.

Taarifa iliyotolewa usiku huu wa Juni 11, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema katika mabadiliko hayo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ally Salum Hapi anahamia Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, Rais Samia amemteua Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Batilda Salha Buriani kuwa mkuu wa Mkoa wa Tabora kuchukua nafasi ya Ally Salum Hapi.

Aidha Katibu Twala Wilaya ya Simanjoro Zuwena Omari Jiri ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga kuchukua nafasi ya Batilda Salha Buriani.

Taarifa hiyo imesema tarehe ya uapisho wa viongozi wapya itatangazwa baadaye.

View attachment 1814796
Mama akomaa kutupa nje ya injini vipuri vibovu. "Magu legacy in the toilet".
 
Lkn huyu Jamaa mm naona alitaka mwenyewe kutumbuliwa mtu mwenye akili timamu unaweza sema maneno yale mbele ya wahandishi wa habari kweli?

Eti wananchi RUKHSA kubeba MABANGO na andikeni chochote HATA MKITAKA kuandika MATUSI hivi kweli RC hajui ya kwamba sio kila RAIA anaweza kumpenda RAIS, na anaweza kuchukuwa hiyo Advatage ya kupeleka ujumbe wenye matusi au maneno yasio kuwa na utu mbele ya RAIS.
 
Alikuwa ni Mhadhili Msaidizi kwenye moja ya chuo kikuu kimoja wapo Mkoani Iringa. Ni maarufu sana Iringa kwa uimbaji wake wa nyimbo za Kihehe. Na ni Mnyalukolo wa kutokea Wilayani Mufindi bila shaka.
Ongeza juhudi kujifunza kiswahili kizuri. ...."kwenye moja ya chuo kikuu kimoja wapo"...........
 
Malisa_GJ_(@malisa_gj)_posted_on_Instagram_•_Jun_11,_2021_at_10:23am_UTC%22_.jpg
 
Kasema waende ofisini kwake na hayo mabango wakatoe kero zao sio waende na mabango kwa mama akija...
Sijui kwa nini kimekatwa kipande hicho tu
Wafitini ni wengi. Wenye haki uzongwazongwa na wasio haki.
 
Challamila mm binafsi nakutakia kila la kheri kule uendako pumuzika tuliza akili songa mbele.Kazi yeyote ya kuteuliwa ina matokeo hayo,wewe ni msomi mzuri hakuna Diploma au degree ya Ukuu wa Mkoa,miaka Tisa sio mingi wewe bado kijana,kaa na adui zako mbali usimsahau Mungu wako.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 11 Juni 2021 amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa Mikoa na kuteua viongozi wengine kama ifuatavyo:-

=====

Rais Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza Albert Chalamila, na kumhamishia mkoa huo Mhandisi Robert Gabriel ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Hatua hiyo imetokana na Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko madogo ya wakuu wa Mikoa na kuteua viongozi wengine.

Taarifa iliyotolewa usiku huu wa Juni 11, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema katika mabadiliko hayo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ally Salum Hapi anahamia Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo, Rais Samia amemteua Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Batilda Salha Buriani kuwa mkuu wa Mkoa wa Tabora kuchukua nafasi ya Ally Salum Hapi.

Aidha Katibu Twala Wilaya ya Simanjoro Zuwena Omari Jiri ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga kuchukua nafasi ya Batilda Salha Buriani.

Taarifa hiyo imesema tarehe ya uapisho wa viongozi wapya itatangazwa baadaye.

View attachment 1814796
'Taarifa iliyotolewa usiku huu wa Juni 11, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema katika'
Juni 11 usiku mbona haujafika?
 
Duh Chalamila kaliwa kichwa, pombe itanywekwa kweli? Haha

chalamila hakuliwa kichwa ila yeye mwenyewe kafanya kusudi ili atolewe. chalamila ukimzingua anakuzingua mama alimzingua chalamila petrol na kiberiti chalamila akaona isiwe tabu si wewe hupendi mabango mimi nawaeleza wananchi waje na mabango tena hata ya kukutukana
 
Back
Top Bottom