Rais Samia ataenda tena kujitambulisha wapi? Sijasikia akizindua hata mradi mmoja

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,899
Akiwa nchini Kenya, Rais Samia alieleza kuwa nia ya kuizuru Kenya mapema sana ilikuwa kujitambulisha kwa majirani kwa kuwa alikuwa "mpangaji mpya"!

Leo akizungumza na wanaoitwa "wazee wa Dar es Salaam" amekariri tena ya kuwa ataendelea kuzuru nchi mbalimbali akitoa sababu ileile ya "kujitambulisha kwa majirani" akiwa ni "mpangaji mpya"!

Kiongozi mzalendo anawajibika kueleza manufaa ya kila anachonuia kufanya. Inashangaza ni kwa nini Rais anakimbizana kujitambulisha kwa majirani, yaani utii wake upo kwa majirani na siyo kwa mwenye nyumba, watanzania waliompangisha Ikulu yao.

KWA kuwa mwenye nyumba anayo madhara ikiwa ni pamoja na kutompangisha tena, nilitegemea angeweka kipaumbele kuwazuru wananchi kwanza ndipo aanze kupepea iwapo kuna manufaa ya umma katika kupepea.

Nawasalimu kwa jina la Mwenyezi Mungu aliyeumba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kazi Iendelee 🇹🇿🇹🇿
 
UWANJA WA SOKA WA KISASA KUJENGWA CHATO... Serikali itajenga Uwanja wa soka wa kisasa katika eneo la Chato na utajulikana kama Chato Stadium.

Waziri wa Nishati, Medard Kalemani amesema Uwanja huo utakuwa wa pili kwa ukubwa baada ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kalemani amesema Uwanja huo utatumika kwa ajili ya kuvutia watalii na wawekezaji katika masuala ya utalii.

Waziri Kalemani amesema Uwanja huo utaanza kujengwa hivi karibuni.
 
Kila Mtz. anamfahamu Mama yetu,na sio kwamba anatakiwa kujitambulisha kuanza kuzunguka nchini kana kwamba kuna uchaguzi. Atazunguka kama kuna penye umuhimu, kazi za ufunguzi wa kila mradi si lazima afanye yeye na anao viongozi, chini yake wanaweza vilevile kufanya kazi hizo.

Ama sivyo hakuna haja kwa wasaidizi hao kuwepo. Rais ana majukumu mengi muhimu zaidi ya kuwa kila leo awe ni wa kufungua miradi midogo midogo ambayo, hata mtendaji wa kata,DC/RC/ Waziri au PM au VP wanaweza fanya....kazi iendelee.
 
Back
Top Bottom