Rais Samia ashiriki sherehe za Jubilee ya miaka 25 ya Mhashamu Askofu Niwemugizi, aombwa kusamehe kodi hospitali za kanisa toka mwaka 2015

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
327
414
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25 ya Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi yatakayofanyika kwenye Viwanja vya Posta- Ngara Mjini Mkoani Kagera kuanzia Saa 4 asubuhi hii.

Utafuatilia matangazo haya ya moja kwa moja kupitia Televisheni, Redio na Mitandao ya Kijamii.

=======

Askofu Niwemugizi: Nikushukuru mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, mwaka 1997 nilipewa heshma kubwa sana ya kuwa na hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na hayati Benjamin Mkapa, Rais wa nchi wakati huo nilipopewa uaskofu na kusimikwa pale Rulenge, leo umenipa heshima wewe mheshimiwa Rais ambayo haitatoka moyoni mwangu.

Mimi ni mtu mdogo sana, sasa kwamba wewe unaacha majukumu yako unakuja hapa, ntaachaje kukumbuka. Asante sana, Mungu akubariki.

Nakupa pole kwa safari ndefu ya ughaibuni lakini nakupongeza kwa kuliwakilisha Taifa letu vizuri huko ulikokuwa kwa mikutano ya kimataifa. Kutojihurumia na kusafari tena baada ya safari hiyo ndefu nje ya nchi na kutenga muda ufike Ngara kwenye adhimisho hili ni heshima kwangu na kwa wanajimbo la Rulenga, Ngara.

Kufika kwako nakutafsiri kama ishara ya wewe kutaka kuwa karibu sana na kushirikiana na viongozi wa dini zote kusikilizana nao na kushauriana nao katika masuala muhimu ya kulijenga Taifa letu.

Mimi nakuahidi, niko tayari kukuunga mkono kushirikiana na Serikali yako kwa kuzingatia ukweli, kukuza haki na amani nchini mwetu.

Hospitali za Biharamulo ambazo ni hospitali teule ya wilaya na hospitali ya Rulenge. Hospitali hizi hazifanyi biashara, kile kinacholipwa kidogo ni kuziwezesha tu ziendelee kutoa huduma, kwa hakika zikifungwa hospitali hizi wananchi wataumia.

Tunaomba madeni tuliyonayo ya TRA tusamehewe kwasababu yanatuelemea kwelikweli toka mwaka 2015 mpaka 2020 Biharamulo inadaiwa milioni 113 na hospitali ya Lulenge inadaiwa milioni 213.

Kwakuwa mheshimiwa Rais hospitali hizi zinawahudumia raia wako, basi ikikupendeza utusamehe, pia ikiwezekana utusaidie kupata vibali vya ajira tuboreshe huduma kwa kuwa idadi ya watumishi itayotuwezesha kutoa huduma bora kwa raia wako wa Tanzania.

Amesema atajitahidi kuwa na hekima na uvumilivu na niwe na sikiko la kusikiliza yale yanayosemwa na wengine.


Rais Samia: Kumekuwa na matukio mengi ya mauaji na Watu kujiua kwa kipindi hiki, takwimu zinaonesha katika Wilaya hii ya Ngara pekee mwaka 2020 kulikuwa na matukio 22 ya mauaji na matukio matatu ya Watu kujiua,mwaka 2021 kulikuwa na matukio 21 ya mauaji na mawili ya Watu kujiua

Kuna sababu nyingi zinazofanya kuongezeka kwa matukio ya vifo na mauaji, huwa tunaunda Tume ndani ya Polisi kuchunguza sababu, ripoti zinapokuja wanasema, wivu wa mapenzi, imani za kishirikina, msongo wa mawazo, visasi, ugomvi wa kifamilia, ugumu wa maisha n.k

Ukiangalia sababu za mauaji zinakuonesha kwamba Watu hawako karibu na Mungu, hakuna Dini iliyotoa ruhusa kujiua au kuua, na tunafunzwa kuamini kwamba kifo kinapotokea ni kazi ya Mungu sasa sina hakika wanaojiua au kuua wenzao kama ni kazi ya Mungu sina hakika

Baba Askofu Niwemugizi umezungumzia mmomonyoko wa maadili na pia Watu kusahau mila na desturi ambako kumeondosha utu wetu, tuna kazi kubwa Viongozi wa Dini kurudisha tena nyoyo za Watu kuthamini utu, kurudisha tena Watu kumjua Mungu

Kama unamjua Mungu huendi kumuua mwenzio kwa urithi, kisasi au kwamba umeambiwa amekuroga hukuvuna huendi kumuua mwenzio kama kweli unamjua Mungu, nitoe wito kwa Viongozi wa Dini turudi kwenye mafundisho yetu tuisaidie Jamii
 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25 ya Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi yatakayofanyika kwenye Viwanja vya Posta- Ngara Mjini Mkoani Kagera kuanzia Saa 4 asubuhi hii.

Utafuatilia matangazo haya ya moja kwa moja kupitia Televisheni, Redio na Mitandao ya Kijamii.

Dah!
Baada ya askofu Niwemugizi kukosoa jiwe kwa uonevu wa raia wema akaambiwa yeye siyo raia wa Tanzania, akatakiwa awasilishe cheti cha kuzaliwa chake, cha baba yake, mama yake, bibi na babu zake..
 
Mimi siku hizi kidogokidogo naanza kukosa imani na haya madhehebu yetu...bora ni stick tu kwenye kuielewa Bibilia...unamualika mtu kama huyu ili iweje kwa mfano? na kwanini wanapenda sana kuwaalika viongozi wa siasa wanaotesa watu wasio na hatia?
Huwa inanikera sana hii kitu
 
Aisee hawa viongozi wa kiimani wanatufunza mengi!
...huyu askofu aliteswa na lile jitu katili lililodhani litaishi milele lakini yeye akalisalia sala ya mwisho na kulirushia mavumbi ya mwisho akaamuru jitu katili lifukiwe.
imani ililetwa na meli ukafia kbs unauhakika aliteswa au ni siasa?

huyu mama anaenda kula sherehe bado hujangamua kuwa niwemugizi ni mwanasiasa mwenye vazi la imani kiaskofu?
 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25 ya Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi yatakayofanyika kwenye Viwanja vya Posta- Ngara Mjini Mkoani Kagera kuanzia Saa 4 asubuhi hii.

Utafuatilia matangazo haya ya moja kwa moja kupitia Televisheni, Redio na Mitandao ya Kijamii.

Duh...!. Huyu Mhashamu Baba Askofu Niwemugizi huyu...
sio mtu wa mchezo mchezo!.
Ni huyu ndie alikuwa Rector wa Katoke seminary enzi zile wanafunzi mmoja mtundu akiwa form IV, akavunja kioo cha dirisha la bwenini, bila kujali mtihani ni karibu!, Niwemugizi alimtimua bila huruma!. Mungu bariki Lake Secondary School, walimpokea!, hivyo kufanikiwa kufanya mtihani wa form IV!.
Ni Father huyu ndie aliyemtimua upadiri Padri Kalugendo.
Hata baada ya yule mwanafunzi mtukutu kuja kuwa somebody big, bado Niwemugizi aliendelea kuchonga, mara paap... Baba Askofu akahojiwa uraia!.
Baada ya kuibuka janga la Corona, na Shujaa wetu wa Corona akapiga kambi Jimboni kwake na kutangaza no lock down kwasababu ka Corona ni kaugonjwa kadogo, tusikaogope!, Baba Askofu alitangaza lock down jimboni kwake, this made shujaa wetu to be very furios kumhusu Baba Askofu na akampaka...
Mwisho wa siku, ni Baba Askofu huyu huyu alimsindikiza ile safari yake ya ...
P
 
Kwanini huyu mama maadui wa JPM ndio marafiki zake anataka kutuma message gani. Angalia Mange Kimambi, Lissu, Zuhura Yunus nk.
Kwahiyo mumeo akiwa Na ugomvi Na jirani yake Basi Na ww mke wake uingie kwenye ugomvi hata kama haukuhusu?
 
Duh...!. Huyu Mhashamu Baba Askofu Niwemugizi huyu...
sio mtu wa mchezo mchezo!.
Ni huyu ndie alikuwa Rector wa Katoke seminary enzi zile wanafunzi mmoja mtundu akiwa form IV, akavunja kioo cha dirisha la bwenini, bila kujali mtihani ni karibu!, Niwemugizi alimtimua bila huruma!. Mungu bariki Lake Secondary School, walimpokea!, hivyo kufanikiwa kufanya mtihani wa form IV!.
Ni Father huyu ndie aliyemtimua upadiri Padri Kalugendo.
Hata baada ya yule mwanafunzi mtukutu kuja kuwa somebody big, bado Niwemugizi aliendelea kuchonga, mara paap... Baba Askofu akahojiwa uraia!.
Baada ya kuibuka janga la Corona, na Shujaa wetu wa Corona akapiga kambi Jimboni kwake na kutangaza no lock down kwasababu ka Corona ni kaugonjwa kadogo, tusikaogope!, Baba Askofu alitangaza lock down jimboni kwake, this made shujaa wetu to be very furios kumhusu Baba Askofu na akampaka...
Mwisho wa siku, ni Baba Askofu huyu huyu alimsindikiza ile safari yake ya ...
P
Ampe za uso huyu Hangaya...
 
Mimi siku hizi kidogokidogo naanza kukosa imani na haya madhehebu yetu...bora ni stick tu kwenye kuielewa Bibilia...unamualika mtu kama huyu ili iweje kwa mfano? na kwanini wanapenda sana kuwaalika viongozi wa siasa wanaotesa watu wasio na hatia?
Huwa inanikera sana hii kitu
Mchango na harambee kwanza. Lakini pia Askofu anapata kanafasi ka kuteta naye kwa faragha.
 
Duh...!. Huyu Mhashamu Baba Askofu Niwemugizi huyu...
sio mtu wa mchezo mchezo!.
Ni huyu ndie alikuwa Rector wa Katoke seminary enzi zile wanafunzi mmoja mtundu akiwa form IV, akavunja kioo cha dirisha la bwenini, bila kujali mtihani ni karibu!, Niwemugizi alimtimua bila huruma!. Mungu bariki Lake Secondary School, walimpokea!, hivyo kufanikiwa kufanya mtihani wa form IV!.
Ni Father huyu ndie aliyemtimua upadiri Padri Kalugendo.
Hata baada ya yule mwanafunzi mtukutu kuja kuwa somebody big, bado Niwemugizi aliendelea kuchonga, mara paap... Baba Askofu akahojiwa uraia!.
Baada ya kuibuka janga la Corona, na Shujaa wetu wa Corona akapiga kambi Jimboni kwake na kutangaza no lock down kwasababu ka Corona ni kaugonjwa kadogo, tusikaogope!, Baba Askofu alitangaza lock down jimboni kwake, this made shujaa wetu to be very furios kumhusu Baba Askofu na akampaka...
Mwisho wa siku, ni Baba Askofu huyu huyu alimsindikiza ile safari yake ya ...
P
Hii comment ni fupi lakini imejaa taarifa nyeti na nyingi sana.

Kumbe yule mtu Big alishawahi kufukuzwa shule?
 
Duh...!. Huyu Mhashamu Baba Askofu Niwemugizi huyu...
sio mtu wa mchezo mchezo!.
Ni huyu ndie alikuwa Rector wa Katoke seminary enzi zile wanafunzi mmoja mtundu akiwa form IV, akavunja kioo cha dirisha la bwenini, bila kujali mtihani ni karibu!, Niwemugizi alimtimua bila huruma!. Mungu bariki Lake Secondary School, walimpokea!, hivyo kufanikiwa kufanya mtihani wa form IV!.
Ni Father huyu ndie aliyemtimua upadiri Padri Kalugendo.
Hata baada ya yule mwanafunzi mtukutu kuja kuwa somebody big, bado Niwemugizi aliendelea kuchonga, mara paap... Baba Askofu akahojiwa uraia!.
Baada ya kuibuka janga la Corona, na Shujaa wetu wa Corona akapiga kambi Jimboni kwake na kutangaza no lock down kwasababu ka Corona ni kaugonjwa kadogo, tusikaogope!, Baba Askofu alitangaza lock down jimboni kwake, this made shujaa wetu to be very furios kumhusu Baba Askofu na akampaka...
Mwisho wa siku, ni Baba Askofu huyu huyu alimsindikiza ile safari yake ya ...
P
Aisee!
That's news to me! Kumbe walitoka mbali!
 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25 ya Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi yatakayofanyika kwenye Viwanja vya Posta- Ngara Mjini Mkoani Kagera kuanzia Saa 4 asubuhi hii.

Utafuatilia matangazo haya ya moja kwa moja kupitia Televisheni, Redio na Mitandao ya Kijamii.

Hainiusu
 
Duh...!. Huyu Mhashamu Baba Askofu Niwemugizi huyu...
sio mtu wa mchezo mchezo!.
Ni huyu ndie alikuwa Rector wa Katoke seminary enzi zile wanafunzi mmoja mtundu akiwa form IV, akavunja kioo cha dirisha la bwenini, bila kujali mtihani ni karibu!, Niwemugizi alimtimua bila huruma!. Mungu bariki Lake Secondary School, walimpokea!, hivyo kufanikiwa kufanya mtihani wa form IV!.
Ni Father huyu ndie aliyemtimua upadiri Padri Kalugendo.
Hata baada ya yule mwanafunzi mtukutu kuja kuwa somebody big, bado Niwemugizi aliendelea kuchonga, mara paap... Baba Askofu akahojiwa uraia!.
Baada ya kuibuka janga la Corona, na Shujaa wetu wa Corona akapiga kambi Jimboni kwake na kutangaza no lock down kwasababu ka Corona ni kaugonjwa kadogo, tusikaogope!, Baba Askofu alitangaza lock down jimboni kwake, this made shujaa wetu to be very furios kumhusu Baba Askofu na akampaka...
Mwisho wa siku, ni Baba Askofu huyu huyu alimsindikiza ile safari yake ya ...
P
Sema unajuaga kunogesha genge. Yaan magu azaliwe 1959 niwemugizi azaliwe 1956 af unakuja kutuambia ni mtu na rector wake kweli? Tena akiwa form 4.
 
Back
Top Bottom