Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,592
- 29,712
Leo tarehe 07 Nov. 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania alishiriki mkutano wa 27 wa kujadili mabadiliko ya tabia nchi.
Mkutano huo umefanyika kwenye mji wa Sharm El Sheikh. Rais Samia ameambatana na Waziri wa mambo ya nne na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Stergomena Tax.
---
Dar es Salaam. Kutokana na upungufu wa megawati zaidi ya 6,000 unaozikabili nchi za kusini mwa Afrika, Rais Samia Suluhu Hassan kesho ataongoza mjadala ya kuongeza uzalishaji wa umeme na usambazaji wake katika mkutano wa 27 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Tabianchi (COP 27) kutafuta suluhu ya kudumu.
Rais Samia amewaalika wakuu wenzake wa nchi 11, rais wa Benki ya Dunia na rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ili kufanikisha uzalishaji na usambazaji wa nishati ya kutosha kwa ajili ya viwanda vinavyoendelea kujengwa barani humu.
“Mara zote Tanzania ilikuwa mshiriki tu, hii ni mara ya kwanza tunaandaa mkutano wa pembeni unaowakutanisha wadau muhimu. Kwa sasa, kwa ujumla tuna upungufu wa megawati 6,000 lakini miaka mitano ijayo utafika megawati 10,000. Tunahitaji nguvu ya pamoja kuwekaza,” amesema Januari Makamba, Waziri wa Nishati.
Waziri Makamba amesema Afrika huzalisha umeme kwa ushirikiano wa mataifa kadhaa (power pools) na Tanzania ni mjumbe wa ushirika wa mataifa ya kusini (Southern Africa Power Pool) ulioanzishwa mwaka 1997 ukilenga kuimarisha uzalishaji na usambazaji ili Taifa litakalokuwa na ziada liliuzie lenye upungufu.
“Tangu SAPP ianzishwe hakujawahi kuwa na umeme wa kutosha hata miundombinu ya usambaji haikujengwa. Sasa hivi Tanzania tunakamilisha njia ya usambazaji kwenda Zambia na ile ya Kenya itakayokamilika Desemba. Kwa ukubwa wa soko letu, itakuwa rahisi kupata mkopo nafuu.
Rais (Samia) amewaita wadau ili kujadiliana vyanzo mbadala hasa umemejua na upepo vinavyoweza kuchangamkia na kampuni kubwa za nishati,” amesema Makamba.
Kwa sasa, waziri alisema Tanzania inavyo vyanzo vinavyoweza kuzalisha zaidi ya megawatu 2,000 za umemejua na upepo na tayari Serikali inatekeleza miradi ya kuzalisha megawati 300 akitolea mfano uliopo Kishapu mkoani Shinyanga na Singida.
Takwimu zilizopo zinaonyesha nchi wanachama wa SAPP zina vyanzo vya kuzalisha zaidi ya jigawati 10.3 vinavyoweza kuendelezwa ndani ya miaka 10 ijayo na kukidhi mahitaji iwapo zitajenga giridi ya kilomita 6,085 kuusambaza kwa wananchi wao.
“Tunahitaji uwekezaji wa dola 18 bilioni za Marekani kukidhi mahitaji yatakayoongezeka kwa miaka mitano ijayo katika mataifa yote 12 ya SAPP,” amesema Makamba.
Mkutano huo umefanyika kwenye mji wa Sharm El Sheikh. Rais Samia ameambatana na Waziri wa mambo ya nne na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Stergomena Tax.
---
Rais Samia awakutanisha marais 11 kujadili umeme
Ni katika mkutano wa COP 27 unaoendelea nchini Misri kuanzia Oktoba 31 mpaka Novemba 18.Dar es Salaam. Kutokana na upungufu wa megawati zaidi ya 6,000 unaozikabili nchi za kusini mwa Afrika, Rais Samia Suluhu Hassan kesho ataongoza mjadala ya kuongeza uzalishaji wa umeme na usambazaji wake katika mkutano wa 27 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Tabianchi (COP 27) kutafuta suluhu ya kudumu.
Rais Samia amewaalika wakuu wenzake wa nchi 11, rais wa Benki ya Dunia na rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ili kufanikisha uzalishaji na usambazaji wa nishati ya kutosha kwa ajili ya viwanda vinavyoendelea kujengwa barani humu.
“Mara zote Tanzania ilikuwa mshiriki tu, hii ni mara ya kwanza tunaandaa mkutano wa pembeni unaowakutanisha wadau muhimu. Kwa sasa, kwa ujumla tuna upungufu wa megawati 6,000 lakini miaka mitano ijayo utafika megawati 10,000. Tunahitaji nguvu ya pamoja kuwekaza,” amesema Januari Makamba, Waziri wa Nishati.
Waziri Makamba amesema Afrika huzalisha umeme kwa ushirikiano wa mataifa kadhaa (power pools) na Tanzania ni mjumbe wa ushirika wa mataifa ya kusini (Southern Africa Power Pool) ulioanzishwa mwaka 1997 ukilenga kuimarisha uzalishaji na usambazaji ili Taifa litakalokuwa na ziada liliuzie lenye upungufu.
“Tangu SAPP ianzishwe hakujawahi kuwa na umeme wa kutosha hata miundombinu ya usambaji haikujengwa. Sasa hivi Tanzania tunakamilisha njia ya usambazaji kwenda Zambia na ile ya Kenya itakayokamilika Desemba. Kwa ukubwa wa soko letu, itakuwa rahisi kupata mkopo nafuu.
Rais (Samia) amewaita wadau ili kujadiliana vyanzo mbadala hasa umemejua na upepo vinavyoweza kuchangamkia na kampuni kubwa za nishati,” amesema Makamba.
Kwa sasa, waziri alisema Tanzania inavyo vyanzo vinavyoweza kuzalisha zaidi ya megawatu 2,000 za umemejua na upepo na tayari Serikali inatekeleza miradi ya kuzalisha megawati 300 akitolea mfano uliopo Kishapu mkoani Shinyanga na Singida.
Takwimu zilizopo zinaonyesha nchi wanachama wa SAPP zina vyanzo vya kuzalisha zaidi ya jigawati 10.3 vinavyoweza kuendelezwa ndani ya miaka 10 ijayo na kukidhi mahitaji iwapo zitajenga giridi ya kilomita 6,085 kuusambaza kwa wananchi wao.
“Tunahitaji uwekezaji wa dola 18 bilioni za Marekani kukidhi mahitaji yatakayoongezeka kwa miaka mitano ijayo katika mataifa yote 12 ya SAPP,” amesema Makamba.