Rais Samia ashauri umuhimu wa kusikiliza watangulizi lakini hailazimiki kufata matakwa yao. Akemea udikteta kwani hufupisha safari

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,806
Rais Samia leo ameongelea ushauri ambao anaweza kuwapa wanawake viongozi wa sasa. Rais Samia amesema wasijikite kwenye misingi ya uongozi ya chuoni pekee. Ni muhimu kutambua na kujua lengo na ni muhimu kuwa mnyenyekevu ikiwemo kuwasikiliza watu zaidi na kuzungumza kidogo.

Rais Samia kasema ni muhimu kuwasikiliza hata wale wanaodhaniwa ni wapumbavu kwasababu wanaweza kuwa na kitu cha msingi cha kujifunza kutoka kwao. Pia kuelewa jamii yako unayotaka kuwasiliana nao.

Ushauri wa mwisho Rais Samia amesema ni muhimu kujifunza kutoka kwa watangulizi, wale ambao wanafahamu taasisi unayoifanyia kazi kwani wapo wazoefu, watangulizi ambao wamekuwa kwenye ofisi husika kwa muda mrefu, Rais Samia amewataka viongozi kuwasikiliza lakini wasilazimike kufata matakwa yao bali watafute njia yao na muelekeo wao.

Pia Rais Samia ametaka viongozi hao kutolazimisha watu, wasiwe na udikteta bali washirikishe watu, wasiagize watu wakafanye vitu bali wawe na mbinu shirikishi. Amesema wakiwa na udikteta safari yao itakuwa fupi na wahakikishe nafasi walinayo wanayo kwa muda mrefu sio mfupi kwani kuna wakati watakuwa wanajaribiwa.

Kongamano la wanawake viongozi vijana Afrika
Zanzibar
03/12/2022

 
Rais Samia leo ameongelea ushauri ambao anaweza kuwapa wanawake viongozi wa sasa. Rais Samia amesema wasijikite kwenye misingi ya uongozi ya chuoni pekee. Ni muhimu kutambua na kujua lengo na ni muhimu kuwa mnyenyekevu ikiwemo kuwasikiliza watu zaidi na kuzungumza kidogo.

Rais Samia kasema ni muhimu kuwasikiliza hata wale wanaodhaniwa ni wapumbavu kwasababu wanaweza kuwa na kitu cha msingi cha kujifunza kutoka kwao. Pia kuelewa jamii yako unayotaka kuwasiliana nao.

Ushauri wa mwshi Rais Samia amesema ni muhimu kujifunza kutoka kwa watangulizi, wale ambao wanafahamu taasisi unayoifanyia kazi kwani wapo wazoefu, watangulizi ambao wamekuwa kwenye ofisi husika kwa muda mrefu, Rais Samia amewataka viongozi kuwasikiliza lakini wasilazimike kufata matakwa yao lakini watafuta njia yao na muelekeo wao.

Pia Rais Samia ametaka viongozi hao kutolazimisha watu, wasiwe na udikteta bali washirikishe watu, wasiagize watu wakafanye vitu bali wawe na mbinu shirikishi. Amesema wakiwa na udikteta safari yao itakuwa fupi na wahakikishe nafasi walinayo wanayo kwa muda mrefu sio mfupi kwani kuna wakati watakuwa wanajaribiwa.

Kongamano la wanawake viongozi vijana Afrika
Zanzibar
Rais Samia kasema ni muhimu kuwasikiliza hata wale wanaodhaniwa ni wapumbavu kwasababu wanaweza kuwa na kitu cha msingi cha kujifunza kutoka kwao. Pia kuelewa jamii yako unayotaka kuwasiliana nao.
CC: aunt Fettie
 
Mimi nadhani upumbavu ni kuhangaika kusikiliza ushauri wa mtangulizi wako wakati ukijua sio lazima kwako kuufuata, sasa kwanini ujihangaishe kuusikiliza?

Na inapotokea anashauriwa kufanya jambo lililopo kisheria, halafu yeye kwa ujinga wake akaacha kulifanya kwa kuamini sio lazima afuate ushauri wa wengine, huu wake utakuwa sio upumbavu tu, bali ni level ya juu zaidi ya upumbavu.
 
Rais Samia leo ameongelea ushauri ambao anaweza kuwapa wanawake viongozi wa sasa. Rais Samia amesema wasijikite kwenye misingi ya uongozi ya chuoni pekee. Ni muhimu kutambua na kujua lengo na ni muhimu kuwa mnyenyekevu ikiwemo kuwasikiliza watu zaidi na kuzungumza kidogo.

Rais Samia kasema ni muhimu kuwasikiliza hata wale wanaodhaniwa ni wapumbavu kwasababu wanaweza kuwa na kitu cha msingi cha kujifunza kutoka kwao. Pia kuelewa jamii yako unayotaka kuwasiliana nao.

Ushauri wa mwisho Rais Samia amesema ni muhimu kujifunza kutoka kwa watangulizi, wale ambao wanafahamu taasisi unayoifanyia kazi kwani wapo wazoefu, watangulizi ambao wamekuwa kwenye ofisi husika kwa muda mrefu, Rais Samia amewataka viongozi kuwasikiliza lakini wasilazimike kufata matakwa yao bali watafute njia yao na muelekeo wao.

Pia Rais Samia ametaka viongozi hao kutolazimisha watu, wasiwe na udikteta bali washirikishe watu, wasiagize watu wakafanye vitu bali wawe na mbinu shirikishi. Amesema wakiwa na udikteta safari yao itakuwa fupi na wahakikishe nafasi walinayo wanayo kwa muda mrefu sio mfupi kwani kuna wakati watakuwa wanajaribiwa.

Kongamano la wanawake viongozi vijana Afrika
Zanzibar
03/12/2022

View attachment 2434304
Kama nchi tumepata hasara sana, zilingwa mbali zitendwa mbali, huyu ni ceremonial head of state, she is remoted by certain gangs
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naona kashaanza kushtuka juu ya wastaafu hasa wanaopenda kumpa ushauri ambao hauna afya katika kuendesha nchi kwa maneno hayo huenda alishaanza kuona yule mtu wa Msoga anamsumbua sumbua maana ni miongoni mwa wastaafu wenye nguvu na ushawishi ndani ya CCM aliyebaki hata kwa wafanyabiashara pia ambao mfano mzuri ni Rostam Azizi

Kwa hali hii naona kuna kitu hakipo sawa sasa ni wakati Rais ajue yeye ndiye Rais asiwepo kama nembo tu ni vizuri asikilize watu wake na achuje yale wanayomshauri hii nikutokana kwamba tangu aingie madarakani ni kama chombo kinaendeshwa na mtu aliye nje ya Serikali


Kwa maneno hayo hapo chini kuna kitu hakipo sawa mambo yanazidi kubadilika siku hadi siku tunapoelekea 2025
FB_IMG_1670073138485.jpg
 
Ameanza kujiamini eeh! Atembee kwa uangalifu lakini, hao watangulizi wana nguvu ya bara ambayo ndio inampa uraisi. Asipoangalia wanaweza kuridhia Chadema ichukue nchi kuliko yeye aendelee kuwa raisi

Msoga alimpa Mkapa kavukavu, msiponiteua kuwa mgombea wa CCM basi naenda kugombea Chadema, na tutashinda. Sasa kama unataka CCM ifie mikononi mwako weka mgombea wako ambae taarifa ya TISS zinasema yeye hana madhambi.

Mkapa akatupilia mbali ripoti za TISS
 
Aliyoyasema yakifanyika Kwa vitendo, Nchi itajinasua mikononi mwa wahuni wachache wezi na mashetani wa enzi na enzi wasio taka kuona nchi yetu ikinufaika na utajiri Mkubwa ambao Mungu ameipatia

Hili Genge la kihuni, kazi yao ni kuhakikisha nchi inakuwa chini yao milele ikiwezekana ili waendelee kuiba bila kujali watakufa!

Nitaanza kumuunga mkono Mh Rais sasa
 
Aliyoyasema yakifanyika Kwa vitendo, Nchi itajinasua mikononi mwa wahuni wachache wezi na mashetani wa enzi na enzi wasio taka kuona nchi yetu ikinufaika na utajiri Mkubwa ambao Mungu ameipatia

Hili Genge la kihuni, kazi yao ni kuhakikisha nchi inakuwa chini yao milele ikiwezekana ili waendelee kuiba bila kujali watakufa!

Nitaanza kumuunga mkono Mh Rais sasa
Mi nadhani amewakusudia wale wa kwa upande wa Bashiru sio yule Mheshimiwa !!
 
Back
Top Bottom