Rais Samia arudi nchini, kuzindua 'Royal Tour' Arusha. Benki ya Dunia na IMF waahidi fedha kama zilizojenga madarasa

Hadi hii hii tour na uzinduzi wa muvi uishe tutakua tumechoka sana. Kwa nini wasingefanya uzinduzi mmoja tuu Tanzania. Lakini imeanza kua kama mbio za mwenge.
 
Mwambie huyo Samia achape kazi sio kushinda kwenye makorido ya IFM na WB anaombaomba, hakuna Mtu au nchi iliyofanikiwa kwa kuombaomba, Tanzania tunazo rasilimali na ardhi ya kutosha, tukitumia akili na nguvu tulizojaliwa na mwenyezi Mungu tunatoboa.

Samia anataka kila kitu tufanyiwe na mzungu na mwekezaji, huku mwananchi akiwa mtazamaji, maana sioni akihamashisha wananchi kuchapa kazi kwa bidii na kujiletea mnaendeleo, yeye ni IFM na wawekezaji, wakati tokea enzi za Mkapa tunaimba wimbo huu wa wawekezaji lakini hatujawahi kutoboa.
Tatizo la Tz ni matumizi makubwa na ufisadi
 
Hivi mimi hii royo tua mbona siielewi!
Kwa hiyo ndio tunakuja kuonyeshwa sehemu zile zile ambazo tunashinda kila siku ili sasa tugeuke nasi tuwe watalii?
Au walimu wa jiografia hawakutufundisha vizuri juu ya maeneo ya nchi yetu hivyo hii itatusaidia vizuri kuyaelewa kwa kupitia 'huyu mwalimu' mpya?
Na je, hizo nchi zenye utalii mwingi nao walifanya haya haya kufikia walipofika?

Haya yananikumbusha 'big results now', 'kilimo kwanza' na 'viwanda milioni 2'. Hatuna dira kabisa
Ni upigaji wa pesa umeandaliwa, nimeenda Seregenti, Ngorongoro, Mikumi, Ruaha, Manyara, Tarangire sijaona kitu cha ajabu sn ambacho baada ya hii Royal Tour kitakuwa kipya
 
Leo Rais Samia Suluhu amerejea nchini na atazindua filamu ya 'Royal Tour' jijini Arusha. Rais Samia ametoa mrejesho wa kilichojiri kwenye ziara yake Marekani ambapo aliondoka nchini April 13, 2022.

Miongoni Rais Samia ameongelea kukutana na IMF na benki ya dunia ambapo ameahidiwa fedha kama iliyoletwa na kupelekwa kwenye vituo vya afya, madarasa na mengineyo.

Rais Samia: Nimesahau moja, kwamba tulifanya pia mazungumzo na mashirika ya fedha ya kimataifa, benki ya dunia na shirika la fedha duniani nao pia mambo ni mazuri, tumekubaliana vizuri na fedha kama ile tuliyoleta na kupeleka kwenye vituo vya afya, madarasa na mengine, tunatarajia kuna nyingine itakuja ya aina ile iende kwenye maendeleo.
Kati ya hizo msafara wake umetumia kiasi gani? Walimu hufunga safari kwenda benki mjini kuchukua mshahara shs 300,00/= nauli, malazi na chakula, anarudi kijijini kwake na shs 220,000/= elfu themanini amegharamia nauli, chakula na malazi! Huyu hana naiti alawansi ila hawa wetu kumenona.
 
Hivi mimi hii royo tua mbona siielewi!
Kwa hiyo ndio tunakuja kuonyeshwa sehemu zile zile ambazo tunashinda kila siku ili sasa tugeuke nasi tuwe watalii?
Au walimu wa jiografia hawakutufundisha vizuri juu ya maeneo ya nchi yetu hivyo hii itatusaidia vizuri kuyaelewa kwa kupitia 'huyu mwalimu' mpya?
Na je, hizo nchi zenye utalii mwingi nao walifanya haya haya kufikia walipofika?

Haya yananikumbusha 'big results now', 'kilimo kwanza' na 'viwanda milioni 2'. Hatuna dira kabisa
Brazil nasikia fukwe tu lkn zinawaingizia matilioni ya fedha hivyo ni bora hata tungeenda huko kujua wenzetu wanatumia mbinu gani sababu hata ss tuna fukwe nzuri sana na tunawaambiwa ni wa pili duniani na Brazili ikiongoza.Mm naamini nchi hii tuna mali nyingi sana lkn cjui tunafeli wapi?
 
Brazil nasikia fukwe tu lkn zinawaingizia matilioni ya fedha hivyo ni bora hata tungeenda huko kujua wenzetu wanatumia mbinu gani sababu hata ss tuna fukwe nzuri sana na tunawaambiwa ni wa pili duniani na Brazili ikiongoza.Mm naamini nchi hii tuna mali nyingi sana lkn cjui tunafeli wapi?
Nchi kubwa, rasiliamali nyingi na watu wengi lakini (huenda - nasikitika kuandika hivi) tatizo ni akili kidogo.

Mfano, ukishakuwa na population ya milioni 60+ inabidi uamini kuwa ni 60m ya mafuvu yaliyojaa ubongo na ubongo ndio hufikiri. Sasa kitendo cha kutumia karibia rasilimali zote za nchi kuwadhibiti wenye mawazo tofauti na kakikundi ka watu wasiozidi 200 (mia mbili) wakishangiliwa na wasiojua hata wanachokitaka ndio kunasababisha haya yote. Na hili ni suala la muda tu wataanza kulaumiana, ndio maana kwao mtu mzuri ni yule atakayehakikisha 'it is our time to eat' inasonga hivyo kupelekea maisha kuwa kusifia na kuponda.
 
Leo Rais Samia Suluhu amerejea nchini na atazindua filamu ya 'Royal Tour' jijini Arusha. Rais Samia ametoa mrejesho wa kilichojiri kwenye ziara yake Marekani ambapo aliondoka nchini April 13, 2022.

Miongoni Rais Samia ameongelea kukutana na IMF na benki ya dunia ambapo ameahidiwa fedha kama iliyoletwa na kupelekwa kwenye vituo vya afya, madarasa na mengineyo.

Rais Samia: Nimesahau moja, kwamba tulifanya pia mazungumzo na mashirika ya fedha ya kimataifa, benki ya dunia na shirika la fedha duniani nao pia mambo ni mazuri, tumekubaliana vizuri na fedha kama ile tuliyoleta na kupeleka kwenye vituo vya afya, madarasa na mengine, tunatarajia kuna nyingine itakuja ya aina ile iende kwenye maendeleo.
Uzuri wanatupa bure...so what is the big deal?😂😂😂😂
 
Brazil nasikia fukwe tu lkn zinawaingizia matilioni ya fedha hivyo ni bora hata tungeenda huko kujua wenzetu wanatumia mbinu gani sababu hata ss tuna fukwe nzuri sana na tunawaambiwa ni wa pili duniani na Brazili ikiongoza.Mm naamini nchi hii tuna mali nyingi sana lkn cjui tunafeli wapi?
Tunafeli kwenye akili zetu zisizochangamka. Tunafeli sababu ya ubinafsi wetu, bila kujari mali za umma na watanzania waliowengi, pindi tukipata madaraka. Tunafeli sababu work ethics yetu ni chini kabisa ya viwango.
 
Nimesahau moja, kwamba tulifanya pia mazungumzo na mashirika ya fedha ya kimataifa, benki ya dunia na shirika la fedha duniani nao pia mambo ni mazuri, tumekubaliana vizuri na fedha kama ile tuliyoleta na kupeleka kwenye vituo vya afya, madarasa na mengine, tunatarajia kuna nyingine itakuja ya aina ile iende kwenye maendeleo.
We are a donor country
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom