Rais Samia anasema 'hili tunalichukua'. Hayati John Magufuli aliamua pale pale jukwaani

Ipo tofauti nimeiona ndani ya miezi saba tangu JPM aage dunia na Rais Samia apewe nchi. Tofauti ya uwezo wa kusikiliza na kufanya maamuzi yenye mizania sahihi. JPM hakubarikiwa busara za utatuzi wa matatizo mengi ya kiutekelezaji japokuwa alikuwa na sifa ya utatuzi huo. Hayati JPM alipenda kuamua suala pale pale jukwaani yaani muda ule ule alipokuwa ndio kwanza kalifahamu.

Rais Samia anaukwepa huu mzigo wa lawama ya wananchi. Hana pupa ya maamuzi na hutumia busara ya kusema 'mimi na wasaidizi wangu hili tunalichukua na tunakwenda kulifanyia kazi'. JPM aliamua muda ule ule, matokeo yake baada ya siku kadhaa kupita yale maamuzi yanakuwa yakifahamika kuwapendelea baadhi ya watu na kuwaumiza wengine. Baada ya siku kadhaa kupita inakuja kujulikana kuwa maamuzi yameegemea upande mmoja badala ya kuwa ni ya haki. Hulka hii ilisababisha baadhi ya watendaji serikalini kumuogopa Hayati JPM.

Na wengine hawakumuogopa bali walianzisha tabia ya kuharibu kazi makusudi ili wamuachie ofisi ateue watu wengine anaoona wanafaa kupewa ofisi. Rais Samia anakubali kutumia muda mrefu kupata utatuzi wa matatizo akijiridhisha na maamuzi yatakayofikiwa baada ya kulitazama suala husika kwa pande zote mbili. Unaweza kudhan ni udhaifu kumbe ni sifa ya uongozi, kuepuka kuleta mifarakano miongoni mwa watu wako wa karibu.

Kwani udhaifu wa tabia ya maamuzi ya jukwaani ni kiongozi kuwa wapendwa zaidi wanaoaminiwa na yeye na wapendwa wa kawaida tu. Watu wasioogopa wala kuona aibu ya kuwaharibia wenzao walio wengi kwa sifa ya muda mfupi tu.

Rais Samia ameonyesha utulivu wa kufanya maamuzi. Hajaonyesha pupa wala hasira pale anapochokozwa, mfano alichokifanya Baba Mchungaji Gwajima kingeweza kabisa kuiamsha hasira ya Samia lakini akatulia kama hakuna linalotokea. Aliweza kuonyesha ukomavu wa kiuongozi kwa kuweza kuistahimili misukosuko ya kisiasa kwa utulivu mkubwa.

Hayati JPM alipendwa kwa kusimamia haki za wananchi lakini upande mwingine wa sifa hiyo ulimpatia maadui haswa miongoni mwa wale waliokwazwa. Rais Samia ameweza kueleweka pale anaposema 'hili tunalichukua'. Hataki kufanya maamuzi halafu yakaleta msingi mbaya (precedent) wa siku zijazo.
Kwa Hangaya tumepigwa big time
 
Usisahau kwamba Kuna TISS.Hawa wapo active na ni committed sana na kazi zao.JPM taarifa zao alizifanyia kazi.
 
Acha hizo basi, Magu amesikika mara ngapi akiwataka tra wapunguze matozo yasiyo na tija ili wafanyabiashara wengi zaidi waweze kulipa kodi bila shuruti, badala ya kung'ang'ania kuwakamua wachache makodi makubwa! Hao walokuwa wakiwabambikizia mikodi watu ni wezi kama wezi wengine, na ilikuwa ukikomaa nao hao maafisa walichukuliwa hatua! Isitoshe, kwa ujenzi wa nchi Magu alioufanya kipindi chake watu tulishawishika kulipa kodi maana tulishuhudia kodi yetu ikitufanyia maajabu!
Aliwapa uhuru wa hovyo tra kuwabambikia wafanya biashara makadilio makubwa sana tofauti na biashara zao
 
Naona mashabiki wa Maendeleo ya Watu (Ufisadi/Wizi/Rushwa) mkikashifu wale waumini wa maendeleo ya vitu (Infrastructures)!
 
Acha hizo basi, Magu amesikika mara ngapi akiwataka tra wapunguze matozo yasiyo na tija ili wafanyabiashara wengi zaidi waweze kulipa kodi bila shuruti, badala ya kung'ang'ania kuwakamua wachache makodi makubwa! Hao walokuwa wakiwabambikizia mikodi watu ni wezi kama wezi wengine, na ilikuwa ukikomaa nao hao maafisa walichukuliwa hatua! Isitoshe, kwa ujenzi wa nchi Magu alioufanya kipindi chake watu tulishawishika kulipa kodi maana tulishuhudia kodi yetu ikitufanyia maajabu!
Hili halina shaka, kwa aliofanya Magufuli hata angesema tutoe Tozo ili mambo mazuri zaidi yafanyike watu tungezitoa bila kulalama!

Ila hizi tozo za sasa zinzoambatana na mabillion ya mikopo kila week raisi anatembeza bakuli ughaibuni huko kutoboa utakuwa ngumu! Hatuwezi kuendelea na uchumi tegemezi.

Hata wewe ungekomaa kula ugali wa shkamoo na kulala bure kwa babaako eti kisa kazi hujapata ungejikuta umefikisha miaka 50 ukiwa mjengoni kwa babaako! Lazma uwe na uchumi binafsi ili uweze kukua. Huwezi kukua kwa spoon feeding!
 
Acha hizo basi, Magu amesikika mara ngapi akiwataka tra wapunguze matozo yasiyo na tija ili wafanyabiashara wengi zaidi waweze kulipa kodi bila shuruti, badala ya kung'ang'ania kuwakamua wachache makodi makubwa! Hao walokuwa wakiwabambikizia mikodi watu ni wezi kama wezi wengine, na ilikuwa ukikomaa nao hao maafisa walichukuliwa hatua! Isitoshe, kwa ujenzi wa nchi Magu alioufanya kipindi chake watu tulishawishika kulipa kodi maana tulishuhudia kodi yetu ikitufanyia maajabu!
Wacha kujidanganya wewe na toka kwenye box hilo
 
Hili halina shaka, kwa aliofanya Magufuli hata angesema tutoe Tozo ili mambo mazuri zaidi yafanyike watu tungezitoa bila kulalama!

Ila hizi tozo za sasa zinzoambatana na mabillion ya mikopo kila week raisi anatembeza bakuli ughaibuni huko kutoboa utakuwa ngumu! Hatuwezi kuendelea na uchumi tegemezi.

Hata wewe ungekomaa kula ugali wa shkamoo na kulala bure kwa babaako eti kisa kazi hujapata ungejikuta umefikisha miaka 50 ukiwa mjengoni kwa babaako! Lazma uwe na uchumi binafsi ili uweze kukua. Huwezi kukua kwa spoon feeding!
Kafanya nini unachosifia sifia?
 
Hili halina shaka, kwa aliofanya Magufuli hata angesema tutoe Tozo ili mambo mazuri zaidi yafanyike watu tungezitoa bila kulalama!

Ila hizi tozo za sasa zinzoambatana na mabillion ya mikopo kila week raisi anatembeza bakuli ughaibuni huko kutoboa utakuwa ngumu! Hatuwezi kuendelea na uchumi tegemezi.

Hata wewe ungekomaa kula ugali wa shkamoo na kulala bure kwa babaako eti kisa kazi hujapata ungejikuta umefikisha miaka 50 ukiwa mjengoni kwa babaako! Lazma uwe na uchumi binafsi ili uweze kukua. Huwezi kukua kwa spoon feeding!
Sema na weye bana maana hii mikanjanja inayojaribu kumponda mtu kama JPM (may his soul rests in eternal peace & power, amen) inakera kuliko hata maana ya neno hilo!
Kunda mikodi ya kipuuzi mengi sana yaliondolewa wakati wa Magu, leo hii wameanza kutuletea kimgingomgongo huku wakipishana angani kutembeza mabakuli mfyuuuuu😠❗
 
Sema na weye bana maana hii mikanjanja inayojaribu kumponda mtu kama JPM (may his soul rests in eternal peace & power, amen) inakera kuliko hata maana ya neno hilo!
Kunda mikodi ya kipuuzi mengi sana yaliondolewa wakati wa Magu, leo hii wameanza kutuletea kimgingomgongo huku wakipishana angani kutembeza mabakuli mfyuuuuu
Hutaki hama nchi rudi kwenu burundi
 
So kwa upeo wako nchi haihitaji mahakama bali maamuzi ya hapo kwa hapo kutoka kwa kiongozi? Kweli kuna binadamu wanapenda kuongozwa kidicteta. Nilikiwa najiuliza hawa watu waliokuwa wanasifu yale mambo ya jiwe ni watu wa aina gani, na je wapo kweli au ni propaganda! Ila leo nimeamini kuwa kumbe wapo aisee
Kuna siku mama mmoja akasema mume wake kagongwa na gari la polisi aliye kua amelewa Magu akasema afukuzwe kazi na apelekwe military tribunal na akamzawadia yule mama hela. Yani vitu vya hovyo
 
Back
Top Bottom