SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
✓Wapo wanaopotosha Rais Samia hakupigiwa Kura
✓Wapo wanaopotosha hastahili kugombea tena Urais
✓Wapo wanaopotosha hana uhalali wa kushika wadhifa huo wa Urais hivyo;
SASA TUELEWANE
Kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa tano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli mnamo tarehe 17 Machi, 2021 kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 37(5) Aliyekuwa Makamu wa Rais kwa wakati huo Mheshimiwa SAMIA SULUHU HASSAN ndiye aliyeapa kuongoza nchi kwa nafasi ya Rais na hivyo atakuwa Rais wa sita wa Tanzania.
Ibara hiyo ya 37(5) inasema, "Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."
Aidha Ukomo wa madaraka pia umeelekezwa kwa mujibu wa katiba hiyo katika mazingira kama haya ambayo Makamu wa Rais hulazimika kuchukua madaraka ya Urais,
"Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu."
Hivyo, kwa kuzingatia matakwa ya katiba ni wazi Mheshimiwa Samia kwa kuwa ameshika madaraka haya ikiwa ni miezi mitano tu toka awamu ya pili ya Magufuli kuanza, ataongoza nchi kwa takribani miaka minne unusu, hivyo ataruhusiwa kugombea urais mara moja tu kwa maana ya kipindi cha miaka mitano tu.
Kisiasa: Wakati wa Uchaguzi Mkuu karatasi za kura kwa nafasi ya urais zilikuwa na jina na picha za Mgombea Urais na Mgombea Mwenza pamoja na jina na nembo ya Chama Cha siasa kilichodhamini. Kwa mantiki hiyo dhana ya katiba kumpa kipaumbele makamu wa Rais kwenye kuchukua madaraka ya Rais kama ilivyoelezwa kwenye katiba ibara hiyo ya 37(5) ni kwa sababu alifanya kampeni za kuomba kura na wananchi walishiriki kumpigia kura kumuweka madarakani kwa hiyo dhana ya demokrasia ilionekana.
Darasa Huru.
✓Wapo wanaopotosha hastahili kugombea tena Urais
✓Wapo wanaopotosha hana uhalali wa kushika wadhifa huo wa Urais hivyo;
SASA TUELEWANE
Kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa tano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli mnamo tarehe 17 Machi, 2021 kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 37(5) Aliyekuwa Makamu wa Rais kwa wakati huo Mheshimiwa SAMIA SULUHU HASSAN ndiye aliyeapa kuongoza nchi kwa nafasi ya Rais na hivyo atakuwa Rais wa sita wa Tanzania.
Ibara hiyo ya 37(5) inasema, "Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."
Aidha Ukomo wa madaraka pia umeelekezwa kwa mujibu wa katiba hiyo katika mazingira kama haya ambayo Makamu wa Rais hulazimika kuchukua madaraka ya Urais,
"Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu."
Hivyo, kwa kuzingatia matakwa ya katiba ni wazi Mheshimiwa Samia kwa kuwa ameshika madaraka haya ikiwa ni miezi mitano tu toka awamu ya pili ya Magufuli kuanza, ataongoza nchi kwa takribani miaka minne unusu, hivyo ataruhusiwa kugombea urais mara moja tu kwa maana ya kipindi cha miaka mitano tu.
Kisiasa: Wakati wa Uchaguzi Mkuu karatasi za kura kwa nafasi ya urais zilikuwa na jina na picha za Mgombea Urais na Mgombea Mwenza pamoja na jina na nembo ya Chama Cha siasa kilichodhamini. Kwa mantiki hiyo dhana ya katiba kumpa kipaumbele makamu wa Rais kwenye kuchukua madaraka ya Rais kama ilivyoelezwa kwenye katiba ibara hiyo ya 37(5) ni kwa sababu alifanya kampeni za kuomba kura na wananchi walishiriki kumpigia kura kumuweka madarakani kwa hiyo dhana ya demokrasia ilionekana.
Darasa Huru.