Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,047
Kwa miaka mingi sana Tanzania tumekuwa tunalalamika jambo moja kuu, nalo ni kwamba, pamoja na kuwa na maliasili na utajiri mwingi ila nchi yetu hasa wananchi wamekuwa masikini sana!
Mjadala huu umezungumzwa na kipindi kirefu sana na moja ya sababu ambazo zimekuwa zikitolewa kwa Tanzania kuendelea kuwa masikini pamoja na kuwa na utajiri na Maliasili nyingi ni kwa sababu tumekuwa hatutumii utajiri wetu vizuri ikiwemo kuutangaza kwa dunia ili utunufaishe kiuchumi! Siku zote biashara ni Matangazo!
Kwenye hili suala napenda leo nikiri kuwa Rais Samia ameanza kulipatia majibu suala hili!
Kwa Bara la Afrika, nchi zinazoongoza kwa kupokea watalii wengi ni Morocco, Algeria, Misri na South Africa. Nchi hizi zinapokea watalii zaidi ya Mil 5 hadi Mil 10 kwa mwaka. Na kusema kweli hizi nchi utalii unazinufaisha sana! Kiuhalisia hizi ndo nchi zenye Uchumi mkubwa Afrika na ndo zinaongoza kwa kuwa na chumi imara na maisha bora kwa sehemu kubwa ya wananchi wake!
Ila kwa uhalisia, Kama umetembelea nchi hizi zinazoongoza kwa utalii Africa utagundua kuwa hazina kitu kikubwa kuizidi Tanzania na ukweli ni kuwa Tanzania ina vivutio vingi vya utalii kuzizidi nchi zote hizi.
Kwa South Africa tu! Watalii wengi hupenda kutembelea makumbusho ya Mandela, beach za Cape Town na Mbuga maarufu ya Kruger National Park.
Kiuhalisia Tanzania tuna makumbusho nzuri za freedom fighters wa kusini mwa Afrika zilizopo Bagamoyo, Morogoro na Mtwara na pia Makumbusho ya Mwalimu Nyerere ambae kwa sehemu kubwa anaheshimika sana duniani. Ukiuliza kwa nini hazifahamiki jibu ni moja tu! Hatujazitangaza vya kutosha duniani huko! Na huu ndo ukweli! Vitu vyetu vizuri hatuvitangazi !
Kwa Kruger National Park ya South Afrika Hii ni sawa na nusu au robo ya Mikumi National Park. Kwa idadi ya wanyama haifikii Serengeti au Selous hata kwa robo tu, Ila Leo hii duniani huko ni watu wachache sana wanaijua Selous. Pamoja na Serengeti na Ngorongoro kufahamika ila bado hatujazipa promo za kutosha duniani huko! Selous ambayo kiuhalisia ina wanyama wengi kuliko hata Serengeti haitembelewi hata na watalii 10000 tu kwa mwaka na sababu kuu ni kwamba hatujaitangaza na haijulikani! Kweli kwa muda mrefu tumekuwa kichwa cha mwenda Wazimu!
Kwa beach za Cape Town hizi kwa uzuri hazifikii hata robo kwa uzuri compared na beach za Zanzibar na Mafia! Ila still wao beach zao zinatwmbelewa na watalii wengi kuliko beach zetu za Zanzibar na Mafia. Shida ni moja tu! Tumekuwa hatujitangazi na kujiuza kwa dunia ipasavyo!
Kabla ya COVID , sekta ya utalii ndo imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa zaidi katika kuingiza fedha za kigeni na kwenye pato la Taifa hapa Tanzania! Imekuwa ikifanya hivi huku Tanzania ikiwa haijawai kupokea Watalii Milioni 3 tu tangu kupata uhuru! Fedha hizi ndo zimekuwa zikiendesha nchi, kulipa mishahara na kununua madawa! Swali la kujiuliza ni Je hali ingekuwaje Tanzania ingekuwa inapokea watalii Milioni 5 au 7 au 8 au 10 kwa mwaka? Leo hii si tungekuwa na maendeleo makubwa sana?
Kusema kweli napenda kumpongeza sana Rais Samia kwa Hii Royal Tour, napenda sana tufanye season 2 ya Royal Tour ambapo tuionyeshe Dunia makubwa zaidi yaliyopo Tanzania.
Napenda kushauri kuwa sasa kuwe na Tangazo la kuitangaza Tanzania kwenye channel kubwa kama CNN, Al Jazeera na BBC, kuwe pia na Matangazo ya Tanzania kwenye klabu kubwa duniani kama Barcelona au Real Madrid au Liverpool au Chelsea
Tuvute mikataba nao na tuuze bidhaa zetu hata korosho na kahawa kwenye stadiums zao!
Hongera Rais Samia! Umeanza vizuri, Royal Tour iwe mwanzo tu na wala usiloose focus kwenye hili! Hayo ndo maono ya Rais!
Mjadala huu umezungumzwa na kipindi kirefu sana na moja ya sababu ambazo zimekuwa zikitolewa kwa Tanzania kuendelea kuwa masikini pamoja na kuwa na utajiri na Maliasili nyingi ni kwa sababu tumekuwa hatutumii utajiri wetu vizuri ikiwemo kuutangaza kwa dunia ili utunufaishe kiuchumi! Siku zote biashara ni Matangazo!
Kwenye hili suala napenda leo nikiri kuwa Rais Samia ameanza kulipatia majibu suala hili!
Kwa Bara la Afrika, nchi zinazoongoza kwa kupokea watalii wengi ni Morocco, Algeria, Misri na South Africa. Nchi hizi zinapokea watalii zaidi ya Mil 5 hadi Mil 10 kwa mwaka. Na kusema kweli hizi nchi utalii unazinufaisha sana! Kiuhalisia hizi ndo nchi zenye Uchumi mkubwa Afrika na ndo zinaongoza kwa kuwa na chumi imara na maisha bora kwa sehemu kubwa ya wananchi wake!
Ila kwa uhalisia, Kama umetembelea nchi hizi zinazoongoza kwa utalii Africa utagundua kuwa hazina kitu kikubwa kuizidi Tanzania na ukweli ni kuwa Tanzania ina vivutio vingi vya utalii kuzizidi nchi zote hizi.
Kwa South Africa tu! Watalii wengi hupenda kutembelea makumbusho ya Mandela, beach za Cape Town na Mbuga maarufu ya Kruger National Park.
Kiuhalisia Tanzania tuna makumbusho nzuri za freedom fighters wa kusini mwa Afrika zilizopo Bagamoyo, Morogoro na Mtwara na pia Makumbusho ya Mwalimu Nyerere ambae kwa sehemu kubwa anaheshimika sana duniani. Ukiuliza kwa nini hazifahamiki jibu ni moja tu! Hatujazitangaza vya kutosha duniani huko! Na huu ndo ukweli! Vitu vyetu vizuri hatuvitangazi !
Kwa Kruger National Park ya South Afrika Hii ni sawa na nusu au robo ya Mikumi National Park. Kwa idadi ya wanyama haifikii Serengeti au Selous hata kwa robo tu, Ila Leo hii duniani huko ni watu wachache sana wanaijua Selous. Pamoja na Serengeti na Ngorongoro kufahamika ila bado hatujazipa promo za kutosha duniani huko! Selous ambayo kiuhalisia ina wanyama wengi kuliko hata Serengeti haitembelewi hata na watalii 10000 tu kwa mwaka na sababu kuu ni kwamba hatujaitangaza na haijulikani! Kweli kwa muda mrefu tumekuwa kichwa cha mwenda Wazimu!
Kwa beach za Cape Town hizi kwa uzuri hazifikii hata robo kwa uzuri compared na beach za Zanzibar na Mafia! Ila still wao beach zao zinatwmbelewa na watalii wengi kuliko beach zetu za Zanzibar na Mafia. Shida ni moja tu! Tumekuwa hatujitangazi na kujiuza kwa dunia ipasavyo!
Kabla ya COVID , sekta ya utalii ndo imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa zaidi katika kuingiza fedha za kigeni na kwenye pato la Taifa hapa Tanzania! Imekuwa ikifanya hivi huku Tanzania ikiwa haijawai kupokea Watalii Milioni 3 tu tangu kupata uhuru! Fedha hizi ndo zimekuwa zikiendesha nchi, kulipa mishahara na kununua madawa! Swali la kujiuliza ni Je hali ingekuwaje Tanzania ingekuwa inapokea watalii Milioni 5 au 7 au 8 au 10 kwa mwaka? Leo hii si tungekuwa na maendeleo makubwa sana?
Kusema kweli napenda kumpongeza sana Rais Samia kwa Hii Royal Tour, napenda sana tufanye season 2 ya Royal Tour ambapo tuionyeshe Dunia makubwa zaidi yaliyopo Tanzania.
Napenda kushauri kuwa sasa kuwe na Tangazo la kuitangaza Tanzania kwenye channel kubwa kama CNN, Al Jazeera na BBC, kuwe pia na Matangazo ya Tanzania kwenye klabu kubwa duniani kama Barcelona au Real Madrid au Liverpool au Chelsea
Tuvute mikataba nao na tuuze bidhaa zetu hata korosho na kahawa kwenye stadiums zao!
Hongera Rais Samia! Umeanza vizuri, Royal Tour iwe mwanzo tu na wala usiloose focus kwenye hili! Hayo ndo maono ya Rais!