Mzee makoti
JF-Expert Member
- Jul 27, 2016
- 2,571
- 3,055
Nyie misukule ya dikteta magufuli msimpangie Rais chakufanya, Rais wenu kashaozea chini ya udongo ukoNipo kwenye magroup mengi ya WhatsApp na Facebook nimeona wanaccm wengi sana zaidi ya asilimia 80% walivyochukizwa na kitendo cha Ole Sabaya kusimamishwa na kukiita usalaliti kwa chama, Chadema siwezi kuwalaumu kwa furaha walionayo sasa maana Sabaya aliwaweza sana.
Kiukweli Sabaya licha ya U-DC alikuwa Hai kwa kazi maalumu ya kichama kuvunja ngome ya CHADEMA na hilo alilitimiza kwa kiasi kikubwa.
Wanaccm wamekuwa wachungu najua hapa JamiiForums kuna watu wako huko kwenye makundi wameona hali halisi na kule muhambwe kelele zimeanza kutolewa kuhusu mwenendo wako wa kuwaengua Pro John Pombe Magufuli na kuanza kusuka muungano na upinzani huku WanaCCM waliotembea kifua mbele wakianza kuwa ndio wapinzani
WanaCCM wanahoja za wewe kusema utaanza kuteua kutoka kokote sio mbaya maana hata John Pombe Magufuli aliteuwa lakini sio sera ya chama hapo unaonesha ubaguzi wa kuwataka WanaCCM waanze kujificha na kujiona sio priority tena.
Kijana Sabaya, Arusha alimbana sana Lema akafanikiwa akaenda Hai, Mbowe akaondolewa kuwaona viongozi wa BAVICHA na BAWACHA wakikesha wanakunywa kwa shangwe jua kuna sehemu umekosea na unazidi kukosea kila siku.
Kinachoitwa usaliti wa chama kwa kiongozi mkubwa kama wewe ni ishara mbaya sana.
Jitafakari