Memento
JF-Expert Member
- Jun 13, 2021
- 4,423
- 9,960
Kwanza kabisa mimi ni muumini wa kumkosoa mtu yoyote kwa staha, siamini kwenye kudhihaki Wala kutukana. Kama raisi kuna sehemu amekosea basi tumkosoe kwa staha tumkosoe bila kumvunjia heshima, yeye ni binadamu anapitiwa.
Hili la umeme wa kuunganisha watu wote kwa 27,000 ni yeye amelileta. Mwanzo 27,000 ilikua kwa watu wa REA tu ila kwa watu wa mijini ilikua 321,000.
Baada ya mama Samia kuwa raisi wote tulianza kulipa 27,000 mwezi June mwaka jana na kwa kweli tulimpongeza kwa hili.
Leo mama anasema hii 27,000 kwa wote haiwezekani. Sawa, Ila ina maana amesahau miezi michache nyuma alileta hili?
Akiwa njiani kuelekea Dodoma alisimama na kuwaambia wananchi kuwa tumepunguza gharama ya kuunganisha umeme kwa watu wote, watu wakashangilia sana. Leo watu hawa watakuaje?
Chini nimeweka video, mama Samia akizungumzia kupunguza gharama za kuunganisha umeme.
Huenda amesahau, tumkumbushe.
Hili la umeme wa kuunganisha watu wote kwa 27,000 ni yeye amelileta. Mwanzo 27,000 ilikua kwa watu wa REA tu ila kwa watu wa mijini ilikua 321,000.
Baada ya mama Samia kuwa raisi wote tulianza kulipa 27,000 mwezi June mwaka jana na kwa kweli tulimpongeza kwa hili.
Leo mama anasema hii 27,000 kwa wote haiwezekani. Sawa, Ila ina maana amesahau miezi michache nyuma alileta hili?
Akiwa njiani kuelekea Dodoma alisimama na kuwaambia wananchi kuwa tumepunguza gharama ya kuunganisha umeme kwa watu wote, watu wakashangilia sana. Leo watu hawa watakuaje?
Chini nimeweka video, mama Samia akizungumzia kupunguza gharama za kuunganisha umeme.
Huenda amesahau, tumkumbushe.