Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,096
- 9,466
Ndugu zangu watanzania,
Kwa hakika Rais Samia Anastahili pongezi kutoka kwa kila mtanzania mzalendo, Rais wetu Ni mpambanaji na aliyepambana kishujaa na kijasiri Sana kwa ajili ya Taifa letu, Amepambana kwa nguvu zake zote kuhakikisha kuwa licha ya mdororo wa uchumi wa kidunia uliosababishwa na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na Vita vya ukrein na kuathiri uchumi wa nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania ,alihakikisha ya kuwa watanzania hatuathiriki na kuelemewa na mzigo wa mfumuko wa Bei.
Rais wetu na serikali yake alihakikisha anatoa mabillioni ya Ruzuku katika Nishati ya mafuta pamoja na mbolea,mfano alitoa Ruzuku ya billion Mia moja kila mwezi katika mafuta pamoja na billion Mia moja hamsini katika mbolea, alipambana kwa kuhakikisha kuwa wakati wote bidhaa muhimu zinakuwepo nchini na zinapatikana kwa Bei nafuu na maeneo yote ya nchi zinakuwepo.
Rais wetu na serikali yake amepambana kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanaofaulu wanapata nafasi ya kuripoti shuleni kwa wakati,kwa kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu 20, alihakikisha Elimu inakuwa bure Hadi kidato Cha sita ili kutoa fursa kwa watoto wanaotoka Kaya za kipato Cha chini wanapata Elimu na kutimiza Ndoto zao,Amejenga zahanani na vituo vya Afya kila mahali ,ametoa maelfu ya ajira kila mwaka ili kuchochea utolewaji wa huduma kwa watanzania.
Rais Samia alizunguka na kufanya ziara huku na huko ili kuzungumza na wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania,matokeo yake tunaona kwa Sasa Tanzania limekuwa chaguo namba moja la wawekezaji, wafanyabiashara na watalii,mapato yameongezeka kufikia Trioni mbili kwa Mwezi,ajira zimeongezeka kupitia miradi mbalimbali ya kiuwekezaji, nchi imefunguka na Sasa Biashara zimeshamiri mitaani na kuchochea mzunguko wa fedha, soko la mazao Ni la uhakika kwa wakulima.
Rais Samia alihakikisha Taifa linakuwa moja,linazungumza lugha moja na Lina kuwa lenye umoja na mshikamano,haya yote yalitokana na maridhiano na mazungumzo mbalimbali aliyoyafanya na viongozi wa vyama vya siasa,viongozi wa Dini,wanaharakati wa haki za binadamu,mashirika mbalimbali na Taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa,na Matokeo au matunda ya juhudi hizi za mh Rais Ni kuwa kwa Sasa tunaona Taifa likiwa na umoja wa kitaifa,amani na utulivu, upendo miongoni mwa watanzania na Imani kubwa imejengeka kwa wawekezaji ,watalii na wafanyabiashara.
Rais Samia alipambana kuhakikisha kuwa anajenga uchumi Unaogusa maisha ya watu,uchumi unaokua katika mifuko ya watu,uchumi unaomnufaisha mtanzania moja kwa moja,uchumi unaokua mikononi mwa mtanzania, alifanya haya kwa kutambua ukweli kuwa uchumi unakuwa hauna maana ikiwa unakuwa katika makaratasi lakini ukakosa uharisia katika maisha ya watanzania.
Rais Samia alipambana kuhakikisha kuwa anaiweka serikali Yake mikononi mwa watanzania,alifanya hivi kwa kuwa msikivu kwa watu,kuwa na ajenda na sera zinazogusa hisia za watu ,maisha ya wengi,maoni ya watu,ushauri wa watanzania,kiu ya wengi na mahitaji ya wote,ndio sababu serikali Yake Ina baraka ya watanzania wote,inakubarika na kuungwa mkono na watanzania wa Rika zote ,makundi yote, jinsia zote,Dini zote na inatetewa na watanzania wote kwa kuwa kila mtu anajiona ni mmiliki wa serikali na kuwa serikali ipo kwa ajili ya kuwatumikia watanzania.
Kwa hakika Rais Samia na serikali Yake Anastahili kupongezwa Sana kwa hapa alipotufikisha,Anastahili kuambiwa Asante mama yetu kwa kazi njema na ya kutukuka aliyoifanya ndani ya muda mfupi,Anastahili kupewa zawadi ya upendo kutoka kwa watanzania wote ,Anastahili kuombewa Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia watanzania.
Amepambana Sana Rais wetu,amepigana Sana mama yetu, Amepigana na kupambana bila kuchoka,Bila kupumzika,bila kukata Tamaa,Bila kupata muda wa kukaa na familia yake, bila kinyongo Wala hasira ,bila kuwafokea au kuwalaumu watanzania,amelibeba Taifa letu katika mabega yake na kuishikiria Bendera yetu katika kifua chake na ramani ya nchi yetu katika macho yake na kuitazama Tanzania na watanzania kwa upendo,huruma ,unyenyekevu na ukarimu wa Hali ya juu Sana,amefanya kwa maslahi ya watanzania na siyo yake binafsi.
Pole Sana mh Rais kwa kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, watanzania tuna kuunga mkono na tupo na wewe bega kwa bega,usichoke Wala kukata Tamaa,Tunakutegemea Sana Kuendelea kupata utumishi wako,yawezekana wapo uliokuwa na matarajio nao makubwa lakini wakakukatisha Tamaa ,napenda kukwambia kuwa songa mbele kwa ujasiri maana walio upande wako Ni wengi Sana,Ni Taifa lote lipo na wewe na Lina kuunga mkono, mitaani kwote sauti za watu zinakuombea heri Sana wewe binafsi na serikali yako.watanzania hatutakuacha mpweke Bali tutapigana kimaombi ili mwenyezi Mungu akujalie Afya na nguvu za kututumikia,Tupo na wewe na tutaendelea kuwa na wewe,tutasimama na wewe na tutasonga na wewe.
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kwa hakika Rais Samia Anastahili pongezi kutoka kwa kila mtanzania mzalendo, Rais wetu Ni mpambanaji na aliyepambana kishujaa na kijasiri Sana kwa ajili ya Taifa letu, Amepambana kwa nguvu zake zote kuhakikisha kuwa licha ya mdororo wa uchumi wa kidunia uliosababishwa na ugonjwa wa COVID 19 pamoja na Vita vya ukrein na kuathiri uchumi wa nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania ,alihakikisha ya kuwa watanzania hatuathiriki na kuelemewa na mzigo wa mfumuko wa Bei.
Rais wetu na serikali yake alihakikisha anatoa mabillioni ya Ruzuku katika Nishati ya mafuta pamoja na mbolea,mfano alitoa Ruzuku ya billion Mia moja kila mwezi katika mafuta pamoja na billion Mia moja hamsini katika mbolea, alipambana kwa kuhakikisha kuwa wakati wote bidhaa muhimu zinakuwepo nchini na zinapatikana kwa Bei nafuu na maeneo yote ya nchi zinakuwepo.
Rais wetu na serikali yake amepambana kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanaofaulu wanapata nafasi ya kuripoti shuleni kwa wakati,kwa kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya elfu 20, alihakikisha Elimu inakuwa bure Hadi kidato Cha sita ili kutoa fursa kwa watoto wanaotoka Kaya za kipato Cha chini wanapata Elimu na kutimiza Ndoto zao,Amejenga zahanani na vituo vya Afya kila mahali ,ametoa maelfu ya ajira kila mwaka ili kuchochea utolewaji wa huduma kwa watanzania.
Rais Samia alizunguka na kufanya ziara huku na huko ili kuzungumza na wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza Tanzania,matokeo yake tunaona kwa Sasa Tanzania limekuwa chaguo namba moja la wawekezaji, wafanyabiashara na watalii,mapato yameongezeka kufikia Trioni mbili kwa Mwezi,ajira zimeongezeka kupitia miradi mbalimbali ya kiuwekezaji, nchi imefunguka na Sasa Biashara zimeshamiri mitaani na kuchochea mzunguko wa fedha, soko la mazao Ni la uhakika kwa wakulima.
Rais Samia alihakikisha Taifa linakuwa moja,linazungumza lugha moja na Lina kuwa lenye umoja na mshikamano,haya yote yalitokana na maridhiano na mazungumzo mbalimbali aliyoyafanya na viongozi wa vyama vya siasa,viongozi wa Dini,wanaharakati wa haki za binadamu,mashirika mbalimbali na Taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa,na Matokeo au matunda ya juhudi hizi za mh Rais Ni kuwa kwa Sasa tunaona Taifa likiwa na umoja wa kitaifa,amani na utulivu, upendo miongoni mwa watanzania na Imani kubwa imejengeka kwa wawekezaji ,watalii na wafanyabiashara.
Rais Samia alipambana kuhakikisha kuwa anajenga uchumi Unaogusa maisha ya watu,uchumi unaokua katika mifuko ya watu,uchumi unaomnufaisha mtanzania moja kwa moja,uchumi unaokua mikononi mwa mtanzania, alifanya haya kwa kutambua ukweli kuwa uchumi unakuwa hauna maana ikiwa unakuwa katika makaratasi lakini ukakosa uharisia katika maisha ya watanzania.
Rais Samia alipambana kuhakikisha kuwa anaiweka serikali Yake mikononi mwa watanzania,alifanya hivi kwa kuwa msikivu kwa watu,kuwa na ajenda na sera zinazogusa hisia za watu ,maisha ya wengi,maoni ya watu,ushauri wa watanzania,kiu ya wengi na mahitaji ya wote,ndio sababu serikali Yake Ina baraka ya watanzania wote,inakubarika na kuungwa mkono na watanzania wa Rika zote ,makundi yote, jinsia zote,Dini zote na inatetewa na watanzania wote kwa kuwa kila mtu anajiona ni mmiliki wa serikali na kuwa serikali ipo kwa ajili ya kuwatumikia watanzania.
Kwa hakika Rais Samia na serikali Yake Anastahili kupongezwa Sana kwa hapa alipotufikisha,Anastahili kuambiwa Asante mama yetu kwa kazi njema na ya kutukuka aliyoifanya ndani ya muda mfupi,Anastahili kupewa zawadi ya upendo kutoka kwa watanzania wote ,Anastahili kuombewa Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia watanzania.
Amepambana Sana Rais wetu,amepigana Sana mama yetu, Amepigana na kupambana bila kuchoka,Bila kupumzika,bila kukata Tamaa,Bila kupata muda wa kukaa na familia yake, bila kinyongo Wala hasira ,bila kuwafokea au kuwalaumu watanzania,amelibeba Taifa letu katika mabega yake na kuishikiria Bendera yetu katika kifua chake na ramani ya nchi yetu katika macho yake na kuitazama Tanzania na watanzania kwa upendo,huruma ,unyenyekevu na ukarimu wa Hali ya juu Sana,amefanya kwa maslahi ya watanzania na siyo yake binafsi.
Pole Sana mh Rais kwa kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, watanzania tuna kuunga mkono na tupo na wewe bega kwa bega,usichoke Wala kukata Tamaa,Tunakutegemea Sana Kuendelea kupata utumishi wako,yawezekana wapo uliokuwa na matarajio nao makubwa lakini wakakukatisha Tamaa ,napenda kukwambia kuwa songa mbele kwa ujasiri maana walio upande wako Ni wengi Sana,Ni Taifa lote lipo na wewe na Lina kuunga mkono, mitaani kwote sauti za watu zinakuombea heri Sana wewe binafsi na serikali yako.watanzania hatutakuacha mpweke Bali tutapigana kimaombi ili mwenyezi Mungu akujalie Afya na nguvu za kututumikia,Tupo na wewe na tutaendelea kuwa na wewe,tutasimama na wewe na tutasonga na wewe.
Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.