Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,479
- 30,144
Wakati akipokea ripoti ya Tume ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2020, hapo tarehe 21 mwezi huu, Ikulu jijini Dar, nilimsikia Rais Samia Suluhu Hassan, akielezea dosari alizoziita ndogo, zilizofanywa na Tume ya uchaguzi Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kuwa ni "kuwa-disqualify" wagombea wa vyama vya upinzani kwa kosa la kutojaza kwa usahihi, form za uchaguzi.
Nimuulize Rais Samia Suluhu Hassan, hivi hajaziona kasoro nyingine kubwa Sana, chungu mzima, zinazolalamikiwa na wapinzani, ila ameiona hiyo kasoro moja pekee??
Wapinzani wamekuwa wakilalamika Katika kipindi kirefu Sana kuwa Tume ya uchaguzi siyo huru na imekuwa ikikipendelea waziwazi chama kilichoko madarakani cha CCM wakati wa uchaguzi
Hivi Mwenyekiti huyo wa Taifa wa CCM, Samia Suluhu Hassan hajasikia malalamiko kuhusu mawakala wa vyama vya upinzani kunyimwa viapo, wakati wenzao wa CCM, wakipewa "kiulaini" viapo hivyo??
Hivi hajasikia kilio cha muda mrefu kuwa mawakala hao wa vyama vya upinzani wamekuwa wakiondolewa kwa nguvu kwenye vituo vyao, wakati wa upigaji kura, kwa msaada wa Polisi??
Hivi hajasikia malalamiko ya wapinzani kuwa mawakala wa vyama vya upinzani wamekuwa wakinyimwa form za matokeo ya uchaguzi, wakati wa chama cha CCM wakipewa??
Hivi hajasikia malalamiko ya vyama vya upinzani ya kuwaweka wakurugenxi wa wilaya, ambao ni makada wa CCM, kuwa ndiyo wasimamizi wskuu wa uchaguzi huo??
Hizo ndiyo sababu Kuu, ambazo zinawafanya vyama vya upinzani vipiganie kufa na kupona Tume ya uchaguzi iliyo huru, kusimamia uchaguzi wa nchi hii, pamoja na kupata Katiba mpya ya nchi hii, kwani Katiba ya hivi sasa ilitungwa kwa ajili ya mfumo wa chama kimoja, ambacho ni cha CCM
Nimuulize Rais Samia Suluhu Hassan, hivi hajaziona kasoro nyingine kubwa Sana, chungu mzima, zinazolalamikiwa na wapinzani, ila ameiona hiyo kasoro moja pekee??
Wapinzani wamekuwa wakilalamika Katika kipindi kirefu Sana kuwa Tume ya uchaguzi siyo huru na imekuwa ikikipendelea waziwazi chama kilichoko madarakani cha CCM wakati wa uchaguzi
Hivi Mwenyekiti huyo wa Taifa wa CCM, Samia Suluhu Hassan hajasikia malalamiko kuhusu mawakala wa vyama vya upinzani kunyimwa viapo, wakati wenzao wa CCM, wakipewa "kiulaini" viapo hivyo??
Hivi hajasikia kilio cha muda mrefu kuwa mawakala hao wa vyama vya upinzani wamekuwa wakiondolewa kwa nguvu kwenye vituo vyao, wakati wa upigaji kura, kwa msaada wa Polisi??
Hivi hajasikia malalamiko ya wapinzani kuwa mawakala wa vyama vya upinzani wamekuwa wakinyimwa form za matokeo ya uchaguzi, wakati wa chama cha CCM wakipewa??
Hivi hajasikia malalamiko ya vyama vya upinzani ya kuwaweka wakurugenxi wa wilaya, ambao ni makada wa CCM, kuwa ndiyo wasimamizi wskuu wa uchaguzi huo??
Hizo ndiyo sababu Kuu, ambazo zinawafanya vyama vya upinzani vipiganie kufa na kupona Tume ya uchaguzi iliyo huru, kusimamia uchaguzi wa nchi hii, pamoja na kupata Katiba mpya ya nchi hii, kwani Katiba ya hivi sasa ilitungwa kwa ajili ya mfumo wa chama kimoja, ambacho ni cha CCM