Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Shida kubwa ya Dangote ni mtu anaeamini in monopoly. Sehemu zote anapowekeza huwa ana bad reputation ya ku corrupt viongozi wa kisiasa ili kuua competition nahisi ndio maana hawakuwezana na mwendazake.
Sasa Dangote anasema kaja kumsapoti Samia Suluhu. Unatafuta hela unajifanya umekuja kumsapoti Rais wa Tanzania. Nenda kamsapoti Muhammad Buhari huko kwenu anahitaji sapoti! Unamsapoti Rais wa Tanzania wewe nani kwa Watanzania kujifanya unajali ?????

Serikali hii nayo inayopelekeshwa na busara za Kikwete inasema itahakikisha inamlinda Dangote na kumwondolea kero zote.

Why Dangote ? Kwa nini isilinde wenye boda boda imlinde Dangote ? Kwa nini isiondoe kero za ushuru wa wavuvi badala ya Dangote ???

KWA NINI Dangote anahitaji kulindwa kuliko wachuuza korosho wa Nachingwea au wauza spea wa Shaurimoyo ?????
 
Mkuu Babati kwa kuwa una chuki na uongozi wa CCM badala ya kuwa mchambuzi, kwa maslahi mapana ya Taifa, hujapenda kusoma na/au kufuatilia utekelezaji wa Ilani zake za Uchaguzi ambazo kimsingi ni mikakati ya kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa (Development Vision 2025).

Moja ya mikakati iliyomo kwenye Ilani yake ya Uchaguzi 2025 kuhusu Kukuza uchumi wa kisasa, fungamanishi, jumuishi na shindani uliojengwa katika msingi wa viwanda, huduma za kiuchumi na miundombinu wezeshi ni Kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kukua na kustawi pamoja na kuvutia wawekezaji ili watoe mchango stahiki katika maendeleo ya nchi yetu.

Serikali zote za CCM zimekuwa zikifanya hivyo tofauti imekuwa katika kutafsiri Ilani zake na kusimamia utekelezaji.
Mkuu mbona hakuna chuki ni ushauri tu! angalia Pinda alikuja na sera ya kilimo kwanza iko wapi? mwendazake viwanda vikowapi? mama hata halijulikani anasimamia nini? miradi kibao ilianzishwa Chato toka mwendazake ameondoka kuna mtu anataja Chato tena? tuwe na mikakati/sera ambayo kila mtawala akija iwe ni kuisimamia na siyo kuja na sera zake, JK ilikuwa bandari ya Bagamoyo na gesi ya Mtwara sasa hakuna hata mtu anaviongolea.
 
Umenena vema kabisa. Sera za Uwekezaji inatakiwa iwe ni mipango ya Kimkakati ya Ki-Taifa tena ya muda mrefu. Sera ya Uwekezaji haipaswi kubadilishwa pale Kiongozi mmoja anapoondoka na kubalisha uongozi wa Kitaifa. Ndio maana Uwekezaji Tanzania umekuwa ukisuasua mno kwa kile Wawekezajia wanacho kilalamikia kuwa "luck of seriousness and vision" ya viongozi wa Tanzania kwenye masuala mazima ya Uwekezaji mkubwa na wa kimkakakati.
Kabisa mkuu kila mtawala anakuja na sera zake, kwa namna hiyo hatutafika
 
Madereva wake wameajiriwa kama contractors badala ya kupewa full time employment, hilo linawakosesha haki zao za kisheria nyingi ikiwemo uhakika wa kazi zao, kuingizwa kwenye pension schemes, kwenda likizo ya malipo, sick pay na faida wanazopewa wafanyakazi wenzao; bila ya kusahau kupoteza PAYE za TRA.

Hayo ndio mambo ya kumkubusha na yeye. Juzi tu madereva wa Dangote walikuwa kwenye mgomo kisa kuchukuliwa kama vibarua wakati watu wanafanya kazi sehemu moja zaidi ya miaka miwili, hakuna madereva wenye mkataba wa kudumu na kampuni; kuna middleman anaewapa ajira na kuwapunja kwa kuwakata kilicho chao, bila ya ulazima.

Wafanyabiashara sio kuja kuomba mazingira mazuri tu, bali na wao waweke mazingira mazuri kwa waajiriwa, sakata lote la mgomo limeenda karibu week nzima Mhagama kama alikuwa aoni vile na nina uhakika wale madereva madai yao ya msingi ayajatatuliwa.
Hii inaitwa outsourcing. Ni mojawapo ya mbinu inayotumika kuleta ufanisi.
 
Huo ndio m
Madereva wake wameajiriwa kama contractors badala ya kupewa full time employment, hilo linawakosesha haki zao za kisheria nyingi ikiwemo uhakika wa kazi zao, kuingizwa kwenye pension schemes, kwenda likizo ya malipo, sick pay na faida wanazopewa wafanyakazi wenzao; bila ya kusahau kupoteza PAYE za TRA.

Hayo ndio mambo ya kumkubusha na yeye. Juzi tu madereva wa Dangote walikuwa kwenye mgomo kisa kuchukuliwa kama vibarua wakati watu wanafanya kazi sehemu moja zaidi ya miaka miwili, hakuna madereva wenye mkataba wa kudumu na kampuni; kuna middleman anaewapa ajira na kuwapunja kwa kuwakata kilicho chao, bila ya ulazima.

Wafanyabiashara sio kuja kuomba mazingira mazuri tu, bali na wao waweke mazingira mazuri kwa waajiriwa, sakata lote la mgomo limeenda karibu week nzima Mhagama kama alikuwa aoni vile na nina uhakika wale madereva madai yao ya msingi ayajatatuliwa.
Huo ndio mfumo wa dunia ya sasa isiyotabirika, hakuna mtu anataka kubeba Mzigo wa kuajiri mtu full time hata nchi zilizoendelea unafanya kazi kwa masaa na kazi zikipungua anapunguza saa, ukizembea anakuondoa saa hiohio, Ukifanya kazi vizuri unaongezewa masaa na malipo, Pakitokea mtikisiko wa uchumi au Pandemic anasimamisha kazi hapo hapo. Hilo ndio soko la ajira la dunia, Hapa TZ wanataka waajiriwe full time ili watege, wakiiba na kuzembea wanaenda mahakamani. Dunia imeshatuacha nyuma sana
 
Maamuz ya kuhamia Dodoma yalikuwa ni moja ya maamuz ya hovyo mno kuwah kufanywa ......!!!
Jikaze tu uamini kwamba Tanzania siyo Dar. Unalaani jambo ambalo kila mtu aliliona ni safi tangu 1974! Kama haikuwa safi kwa nini haikufutwa kwa miaka yote hiyo? Unafiki ktk siasa isiwe ni fasheni.
 
Hivi Kwa nini hawa wafanya biashara wakubwa huwa wanakaa kudekadeka saana!!!

Huyu jamaa anaongoza Kwa kudeka, haishiwi kulalama kama litoto Fulani hivi, Mo, na Bakhlesa, sjawahi kuona wakideka hivyo
Wewe hujui maumivu ya kuwekeza Tilion moja anakuja mtu hata pesa ya kununulia soksi Hajui kuitafuta anataka umpe pesa za bure.
 
Msemaji wa serikali Bwana Gerson Msigwa aposti katika ukurasa wake wa twitter kauli hiyo ambayo imezua maswali mengi kwa wananchi.Ametoa kauli hii hivi leo baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mazungumzo na mwekezaji Dangote.

Wengi wamejiuliza kwani hali ilikuwaje kabla?Wengine wakijiuliza ni nani huyo ambae aliharibu nchi kiasi hicho?
View attachment 1796261
Kwa kweli hata mimi nimejiuliza sana hili swali...Dangote mwenyewe kasema things have opened up, kwani vipi vilifungwa...na vimefunguliwa kwa maslahi gani
 
Madereva wake wameajiriwa kama contractors badala ya kupewa full time employment, hilo linawakosesha haki zao za kisheria nyingi ikiwemo uhakika wa kazi zao, kuingizwa kwenye pension schemes, kwenda likizo ya malipo, sick pay na faida wanazopewa wafanyakazi wenzao; bila ya kusahau kupoteza PAYE za TRA.

Hayo ndio mambo ya kumkubusha na yeye. Juzi tu madereva wa Dangote walikuwa kwenye mgomo kisa kuchukuliwa kama vibarua wakati watu wanafanya kazi sehemu moja zaidi ya miaka miwili, hakuna madereva wenye mkataba wa kudumu na kampuni; kuna middleman anaewapa ajira na kuwapunja kwa kuwakata kilicho chao, bila ya ulazima.

Wafanyabiashara sio kuja kuomba mazingira mazuri tu, bali na wao waweke mazingira mazuri kwa waajiriwa, sakata lote la mgomo limeenda karibu week nzima Mhagama kama alikuwa aoni vile na nina uhakika wale madereva madai yao ya msingi ayajatatuliwa.
Kuna watu wanaoshangilia Dangote utadhani ni binadamu wa kwanza kutengeza sementi, au utadhani kaja kuajili wa-TZ wote mitaani.
Huyu ni mtu aliyeahidiwa huruma ya uwekezaji kwa mdomo na hakujiridhisha kama ni kinyume cha sheria. JPM alipokuja na kutaka sheria zifuatwe bila upendeleo, anaanza kulalama eti anakwamishwa. baadhi ya wanufaika wa ufisadi wakaanza kumsaidia kupiga kelele. Afuate sheria! Mambo ya kutemebelea Ikulu kila leo yanatukwaza wa-TZ na kuhisi rais alivyo wa bei ndogo.
 
Sema Dangote naye ni mtu asiweza kabisa figisu. Biashara zake nyingi ustawi wake unategemea sana kulelewa na serikali. Hata Nigeria iko hivyo.

Ingawa ndio kazi ya serikali kulea sekta binafsi lakini ukipata mtawala roho mbaya kama Magu mambo yanayumba sana.
Investment inahitaj mazingira wezeshi na support kutoka serikali husika, huez ku investment kwa kutegemea figusu.
 
Wewe hujui maumivu ya kuwekeza Tilion moja anakuja mtu hata pesa ya kununulia soksi Hajui kuitafuta anataka umpe pesa za bure.
Bwege wewe! Twiga cement imewekeza ngapi? Tanga cement imewekeza ngapi? KIla siku anagonga mlango wa Ikulu, mbona wenzake wako kimya hatuwasikii? Ufisadi tu unamsumbua.
 
Bwege wewe! Twiga cement imewekeza ngapi? Tanga cement imewekeza ngapi? KIla siku anagonga mlango wa Ikulu, mbona wenzake wako kimya hatuwasikii? Ufisadi tu unamsumbua.
Pole sana, hata hao wengine wanaenda na wanatembelewa kwenye viwanda vyao, ila yeye amewekeza pesa nyingi kushinda hao wengine unaowasema na ametangaza hazarani kiasi cha pesa alichowekeza, hizo ni chuki za kimasikini, na ndio maana ni masikini
 
Investment inahitaj mazingira wezeshi na support kutoka serikali husika, huez ku investment kwa kutegemea figusu.
Ni kweli kabisa, na ndio maana wafanyabiashara wa hapa hawezi kufanya biashara nje kwani wanategemea figisu badala ya maarifa,utaalamu na wataalamu
 
Hakuna cha PR! Ameitoa wapi wakati hajawahi interact na dunia? Hapa sisi tunajua kinachotafutwa. Marais wa kiafrika wanazuzuliwa na vitu vya kishenzi tu! Hata kuambiwa wewe ni zaidi ya wote, inampa kichwa kikubwa. Iliwahi sikika JK alipewa suti na ikatosha kutoa upendeleo. Sasa endeleeni kuamini huyu anajua mambo kumbe wao wameshajua udhaifu wake. Ndo kazi ya ofisi za ubalozi zilizoko hapa nchini, kujua udhaifu wa viongozi wetu.

Baadaye ataalikwa uchina na kupigiwa Tanzania Nakupenda kwa moyo wote kama tunavyowaona wengine, akirudi anasimulia kama spika kwamba alifanyiwa presentation nzuri saaana!
Ha ha ha
 
Madereva wake wameajiriwa kama contractors badala ya kupewa full time employment, hilo linawakosesha haki zao za kisheria nyingi ikiwemo uhakika wa kazi zao, kuingizwa kwenye pension schemes, kwenda likizo ya malipo, sick pay na faida wanazopewa wafanyakazi wenzao; bila ya kusahau kupoteza PAYE za TRA.

Hayo ndio mambo ya kumkubusha na yeye. Juzi tu madereva wa Dangote walikuwa kwenye mgomo kisa kuchukuliwa kama vibarua wakati watu wanafanya kazi sehemu moja zaidi ya miaka miwili, hakuna madereva wenye mkataba wa kudumu na kampuni; kuna middleman anaewapa ajira na kuwapunja kwa kuwakata kilicho chao, bila ya ulazima.

Wafanyabiashara sio kuja kuomba mazingira mazuri tu, bali na wao waweke mazingira mazuri kwa waajiriwa, sakata lote la mgomo limeenda karibu week nzima Mhagama kama alikuwa aoni vile na nina uhakika wale madereva madai yao ya msingi ayajatatuliwa.
Nadhani hi sasa ndio kazi ya serikali kuhakikisha wafanyabaishara nao wanafuata sheria; kama kuna loop holes, mfanyabaishara atazitumia, kwanini EWURA, TCRA nk vilianzishwa? Kazi yake ni ku regulate mambo ya sekta husika. wizara ya kazi na vijana na hasa kitengo cha kazi (of course na vyama vya wafanyakazi, in this case ni TAMICO ) ndio kazi zao hizi, wasikae tu ofisini, watembee kwa waajiri na kwenda kuwatia moyo, kuwarekebisha, kuwashauri na hata kutumia nguvu ili wao wafuate sheria. Hapa sasa ndio tutamuelewa profesa Asad alivyokua kule USA kwenye ile interview iliomletea matatizo na watawal pamoja na bwana Ndugai (naogopa kulihusisha bunge hapa ), jamaa alishauri kwamba, Africa tunawekeza kwenye strong personalities badala ya kuwekeza kwenye strong institutions, hi ndio mahala pake.
 
Ahsante sana Bagamoyo,
Kweli teknologia haiongopi, ndio hiki nimekizungumzia, na hapo nimesikia hata huo mpango wa kujenga kiwanda cha mbolea ulikuwa toka hicho kipingi cha Magufuli.

wamlaum kwa mambo mengine lakini haki yake apewa,

kwangu mimi Magufuli amefanya mambo ambayo watanzania tuliyalilia muda mrefu.
Pamoja na mapungufu yake kama binadamu sote tulivyo, lakini tukubali kwa kauli moja kwamba Dk. Magufuli hakuwa binadamu wa kawaida kimaono, kiutendaji kazi na ufatiliaji wa karibu.

Baadhi ya watu wanajaribu kumsema mambo mengi mabaya Magufuli walwatu,lakini nawakumbusha kwa mara nyingine tena kwamba hakuna Rais yeyote Tanzania pamoja na barani Afrika ambaye aliwahi kuwa mbunifu na muona mbali kama Magufuli - miradi yote mikubwa ya kimkakati inayo endelea hapa Tanzania mwanzilishi wake si mwingine bali Magufuli - ndani ya utawala wake mfupi wa miaka mitano amebuni na kutekeleza miradi mikubwa mikubwa ambayo kwa akili za kawaida uwezi kui-comprehend hata kidogo - halafu watu wenye akili za ajabu wana beza beza miradi na maendeleo yaliyo letwa na mzalendo wa kweli wa Taifa hili.

Wengi wanao mchukulia Magufuli for a ride wanashindwa mpaka na Umoja wa mataifa ambao ulimuenzi wakati alipo aga Duniani kwa kutambuwa sana mchango wake wa kuwaletea maendele binadamu wenzake specifically Tanzanians - kila mara Magufuli alikuwa anatukumbusha kwamba tutakuja kumkubuka - na kweli!! Bottom line ni kwamba: tunapo mlahumu the late Dk. Magufuli tujifunze kubakiza hakiba ya maneno.

Kitu kingine ambacho huwa akina ukweli wowote ni hiki cha kudai eti ukoo wa Magufuli hauna asili ya Tanzania - huu ni uzushi husiokuwa na kichwa wala miguu - ukweli wa mambo ni kwamba kabila la Magufuli ni Mzinza, sio Msukuma mama yake ndio Msukuma na Magufuli alikuwa fluent kwenye lugha ya Kisukuma kutokana na mama yake kuwa Msukuma, kabila la Kizinza has nothing in common na kabila la Kisukuma, mila za Kizinza zinarandana zaidi na mila za Kihaya, hata lugha ya Kizinza haina tofauti sana na lugha ya Kihaya.
 
Huo ndio m

Huo ndio mfumo wa dunia ya sasa isiyotabirika, hakuna mtu anataka kubeba Mzigo wa kuajiri mtu full time hata nchi zilizoendelea unafanya kazi kwa masaa na kazi zikipungua anapunguza saa, ukizembea anakuondoa saa hiohio, Ukifanya kazi vizuri unaongezewa masaa na malipo, Pakitokea mtikisiko wa uchumi au Pandemic anasimamisha kazi hapo hapo. Hilo ndio soko la ajira la dunia, Hapa TZ wanataka waajiriwe full time ili watege, wakiiba na kuzembea wanaenda mahakamani. Dunia imeshatuacha nyuma sana
Sehemu nyingi duniani wanapoajiri watu kupitia agencies ni sababu za seasonal variations na product shelf life.

Mfano labda kwa mwaka mfanyabiashara ana miezi mitano ndio anazalisha zaidi kipindi cha summer na kuelekea Christmas
kutokana na demand, muda huo ndio wanatoa seasonal employment na ina make business sense kutumia agency worker ndani ya hiyo miezi.

Lakini rarely kampuni itatumia watu kwa miaka miwili mfululizo in full time basis bila ya kuajiri moja kwa moja.

Kuna sababu za msingi kwanza agency worker analipwa zaidi ya permanent worker sema tu baadhi ya mshahara wake unaenda kwa agent aliyempa kazi, pili sheria za kazi nchi nyingi zinataka agency kama ana ajiri mtu kwa muda mrefu ampe likizo zake za week sita. Kama ni short term employment basi kila week au mwezi wa mshahara anatakiwa amuwekee na entitlement zake za holiday ambazo atopata kwa kuwa kazi yake aitofikisha miezi mitatu.
 
Kuna watu wanaoshangilia Dangote utadhani ni binadamu wa kwanza kutengeza sementi, au utadhani kaja kuajili wa-TZ wote mitaani.
Huyu ni mtu aliyeahidiwa huruma ya uwekezaji kwa mdomo na hakujiridhisha kama ni kinyume cha sheria. JPM alipokuja na kutaka sheria zifuatwe bila upendeleo, anaanza kulalama eti anakwamishwa. baadhi ya wanufaika wa ufisadi wakaanza kumsaidia kupiga kelele. Afuate sheria! Mambo ya kutemebelea Ikulu kila leo yanatukwaza wa-TZ na kuhisi rais alivyo wa bei ndogo.
Kabisa
 
Back
Top Bottom