Rais Samia akiri kuwepo upungufu wa umeme, Makamba alisema ni 'scheduled maintainance'

Taarifa zilitoka mapema kuwa kutakuwa na ukame...tena toka mwezi wa nane!
Kiongozi yeyote au raia yeyote anaesingizia masuala ya ukame kama chanzo cha matatizo katika sector ya umeme ikiwa ni pamoja na wewe ni binadamu mwenye akili fupi sana.

Kwenye karne ya 21 vyanzo vya umeme vinapaswa kuwa diversified badala ya kutegemea chanzo kimoja cha umeme wa maji peke yake kwa sababu sasa hivi dunia inakumbwa na tatizo kubwa la global warming ambapo kama tulivyoshuhudia viongozi wa dunia wamekuwa wakisitasita katika kutatua tatizo hilo.

Suala la umeme katika level ya nchi linapaswa kuwa na long run solutions ikiwa ni pamoja na diversification katika vyanzo vyake.Kuna vyanzo vingi sana vya umeme kama vile gas na kadhalika.

Kusingizia ukame ni kuishiwa hoja na pumzi katika kuongoza.Dunia ya sasa hivi haipo tena kwenye zama za akili fupi kama hizo.WTF!!!

Kusingizia ukame ni akili za chekechea ambazo ndiyo naona zimejaa hapa JF pamoja na huko Serikalini.
 
Walikata miti milioni 2 kujenga bwawa linalotegemea mvua kama chanzo chake cha maji... maCCM wanaamini mvua zinatoka kwenye mawingu
 
Makamba: Hakuna mgao wa umeme bali ni matengenezo ya kawaida.

Samia: Kuna upungufu mkubwa kwenye vyanzo vya maji hali inayopelekea mgao wa umeme na maji kutoepukika.

Tumwamini nani kati ya mkuu wa Nchi na Waziri wake?!

Juzi niliuliza humu hivi Makamba anatufanya sisi ni mapunguani na hadi muda huu anasubiri nini ofisini?!


Waziri Mkuu: wawekezaji njooni tuna umeme wa kutosha
 
Rais Samia akiwa mkoani Mwanza amesema anatambua uwepo wa upungufu wa umeme ikimaanisha vyanzo vilivyopo havikidhi mahitaji yaliyopo. Waziri wetu wa nishati aliliongelea suala la kukatikatika kwa umeme chanzo chake ni marekebisho ya mfumo wa zamani.

Tunaandaliwa kwa umeme wa dharura?


View attachment 2015320
Wajifunze na waelewe kwamba watanzania siyo mabwege tena

Uwezo wa watu kuchambua mambo ni mkubwa kuliko wanavyofikiri. Viongozi wa kisiasa na kiserikali bado baadhi yao wana mawazo ya kizamani kwa kudhani anaweza akadanganya watu na akabaki salama.

Tabia hii inatakiwa kufa. Kwa ujumla kunahitajika a major overhaul ya watendaji wa ngazi zote ili twende kwa speed inayotakiwa
 
Huwa nasikitika Sana wanapolaumiwa wachezaji football wa Tanzania kuwa hawajui au hawapo serious pale timu yetu ya taifa inapofanya vibaya. Vijana hawa hulaumiwa sbb kazi yao hufanyikia hadharani ambapo na mashabiki hualikwa kushuhudia matokeo ya kazi yao.

Naamini kama na watendaji wa ofisi za umma wangekuwa wanafanyia kazi zao za kitaalam ktk majukwaa ya wazi na si ktk vi ofisi tena vyenye mafaili yaliyoandikwa SIRI wallah Watanzania tungeitisha mjadala wa kitaifa kutafuta suluhu ya matatizo ya uwajibikaji kati yetu. Serikalini kuna watendaji wabovu zaidi ya hawa wacheza football tunao watukana kila uchao.

Ni watendaji hawahawa wameshindwa kutengeneza miundombinu ya kuandaa wachezaji watetezi wa taifa wa kesho. Badala yake huishia kufanya mipango ya zimamoto kutaka matokeo ambayo wenzetu wamewekeza akili, maarifa, pesa na utaalam kuyapata.
Umesema kweli, watendaji wetu wa serikali, tume ya taifa ya uchaguzi, jeshi la polisi, mahakama za mwanzo, watendaji wa vijiji wameliangusha taifa kuliko wachezaji wa timu ya Taifa.
 
Huwa nasikitika Sana wanapolaumiwa wachezaji football wa Tanzania kuwa hawajui au hawapo serious pale timu yetu ya taifa inapofanya vibaya. Vijana hawa hulaumiwa sbb kazi yao hufanyikia hadharani ambapo na mashabiki hualikwa kushuhudia matokeo ya kazi yao.

Naamini kama na watendaji wa ofisi za umma wangekuwa wanafanyia kazi zao za kitaalam ktk majukwaa ya wazi na si ktk vi ofisi tena vyenye mafaili yaliyoandikwa SIRI wallah Watanzania tungeitisha mjadala wa kitaifa kutafuta suluhu ya matatizo ya uwajibikaji kati yetu. Serikalini kuna watendaji wabovu zaidi ya hawa wacheza football tunao watukana kila uchao.

Ni watendaji hawahawa wameshindwa kutengeneza miundombinu ya kuandaa wachezaji watetezi wa taifa wa kesho. Badala yake huishia kufanya mipango ya zimamoto kutaka matokeo ambayo wenzetu wamewekeza akili, maarifa, pesa na utaalam kuyapata.
Una akili sana!
 
Mabadiliko tabia nchi acha kabisa, ukitaka kulijua hilo vizuri njoo uone huo mto huko kwenye bwala la Nyerere kamebaki kamchirizi tu katikati hata likiisha bado tunaweza kuishia kwenye mgao tu.
Duh inamaana JIWE hakufikiri kuhusu hilo jamani?
 
Kiongozi yeyote au raia yeyote anaesingizia masuala ya ukame kama chanzo cha matatizo katika sector ya umeme ikiwa ni pamoja na wewe ni binadamu mwenye akili fupi sana.

Kwenye karne ya 21 vyanzo vya umeme vinapaswa kuwa diversified badala ya kutegemea chanzo kimoja cha umeme wa maji peke yake kwa sababu sasa hivi dunia inakumbwa na tatizo kubwa la global warming ambapo kama tulivyoshuhudia viongozi wa dunia wamekuwa wakisitasita katika kutatua tatizo hilo.

Suala la umeme katika level ya nchi linapaswa kuwa na long run solutions ikiwa ni pamoja na diversification katika vyanzo vyake.Kuna vyanzo vingi sana vya umeme kama vile gas na kadhalika.

Kusingizia ukame ni kuishiwa hoja na pumzi katika kuongoza.Dunia ya sasa hivi haipo tena kwenye zama za akili fupi kama hizo.WTF!!!

Kusingizia ukame ni akili za chekechea ambazo ndiyo naona zimejaa hapa JF pamoja na huko Serikalini.
Majibu nikuwa, sera ya nishati ya nchi inahimiza hiyo diversification yako ya vyanzo vya umeme. Ni kwa sera hiyo juhudi kubwa zimefanywa na serikali kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya nishati.

Juhudi hizi zimekumbwa na changamoto ya uchumi wetu ambao haugawanyiki kukidhi mahitaji yote ya nchi katika suala la maendeleo ya miundombinu na huduma kwa wananchi wote likiwemo suala la nishati.

Suala la mabadiliko ya hewa si halituathiri sisi tu hata nchi zenye uchumi unaogawanyika zinakumbwa nakdhia hii. Mfano mzuri ni namna Marekani ilivyoathirika na janga hili. Ndiyo, Marekani hiyo hiyo unayoijua inayoongizwa na Biden. Hivi majuzi huko nadhani Texas umeme ulikata kisa baridi imekuwa kali mabwawa ya umeme yakaganda, turbine hazizunguki!!! Ilifikia, seneta nadhani ndugu Rubio akakimbia jimbo akawaacha wananchi gizani!!! Nasisitiza ni Marekani hiyo hiyo ujuayo!

Kwa maelezo hayo hapo juu jitathimini kama unatosha kutumia maneno ya kibri na dharau mbele ya maelfu ya watumiaji wa JF.
 
Schedule maintenance inafanyika kwa mitambo yote kwani ilinunuliwa na kufungwa siku moja?
Waziri taahi.ra sana yule, wao waendelee, wanaleta siasa kwenye mambo ya watu, kauli ile haikuwa ya bahati mbaya, ilimaanisha kumdhihaki JPM...
 
Majibu nikuwa, sera ya nishati ya nchi inahimiza hiyo diversification yako ya vyanzo vya umeme. Ni kwa sera hiyo juhudi kubwa zimefanywa na serikali kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya nishati.
Hiyo miradi mbalimbali ya nishati iliyoanzishwa kwa juhudi kubwa ni ipi na imesaidia kupunguza tatizo la kutegemea umeme wa maji kwa kiwango gani?
Juhudi hizi zimekumbwa na changamoto ya uchumi wetu ambao haugawanyiki kukidhi mahitaji yote ya nchi katika suala la maendeleo ya miundombinu na huduma kwa wananchi wote likiwemo suala la nishati.
Kudai kwamba Tanzania inakumbwa na tatizo la uchumi ambao haugawanyiki ni mawazo ya kipunguani kwa sababu Tanzania ina miaka 60 sasa tokea ipate uhuru.Miaka ya 1950 Tanzania ilikuwa karibia sawa kiuchumi na nchi kama vile Korea kusini na Singapore. Sasa hivi Korea ya kusini na Singapore zinaelekea kuwa nchi za uchumi wa kwanza.Kwa hiyo kusema kuwa Tanzania ina matatizo ya uchumi wakati imeshapita miaka 60 tokea ipate uhuru ni kujitetea ya kitoto.
Suala la mabadiliko ya hewa si halituathiri sisi tu hata nchi zenye uchumi unaogawanyika zinakumbwa nakdhia hii. Mfano mzuri ni namna Marekani ilivyoathirika na janga hili. Ndiyo, Marekani hiyo hiyo unayoijua inayoongizwa na Biden. Hivi majuzi huko nadhani Texas umeme ulikata kisa baridi imekuwa kali mabwawa ya umeme yakaganda, turbine hazizunguki!!! Ilifikia, seneta nadhani ndugu Rubio akakimbia jimbo akawaacha wananchi gizani!!! Nasisitiza ni Marekani hiyo hiyo ujuayo!
Marekani au nchi yoyote iliyoendelea kuwa na sera mbaya katika masuala ya nishati ya umeme au hata katika jambo lolote lile haihalalishi nchi yoyote duniani kuwa na Sera mbaya.Kwa mfano Marekani haiwezi kuanza kuua watu wake na Tanzania ianze kuua watu kisa nchi kubwa Marekani imeamua kuua watu wake.Ulichoandika hapa hakina maana.
Kwa maelezo hayo hapo juu jitathimini kama unatosha kutumia maneno ya kibri na dharau mbele ya maelfu ya watumiaji wa JF.
Unajisifu wakati hakuna la maana uliloandika hapo juu.
 
Back
Top Bottom