Rais Samia akifungua barabara ya Afrika mashariki (Arusha Bypass) KM 42.4

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,191
4,104
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akifungua barabara ya Afrika Mashariki (Arusha Bypass) km 42.4 Ngaramtoni Arusha, leo Tarehe 22 Julai, 2022



=======
Hotuba ya Rais Samia, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania

Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mungu na pia kwa viongozi wote wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kujumiaka nasi kwenye ufunguzi wa barabara hii muhimu pamoja na wakandarasi na wananchi wote na wote waliohusika katika kukamilisha mradi huu. Na kwa dhati kabisa nitoe shukrani zangu kwa bank ya maendeleo Afrika waliowezesha ujenzi wa barabara hii.

Kukamilika kwa barabara hii italeta faida za kukuza uchumi na shughuli nyingine katika jumuiya ya Afrika Mashariki. Pamoja na barabara hii sisi Tanzania tunaendela na mradi wa barabara za kutuungunisha na nchi jirani kwa barabara, reli anga na majini ili usafiri na usafirisha uweze kufanyika kwa urahisi ndani ya Afrika Mashariki.

Napenda kutoa Rai kwa watu wote wanaoishi maeneo yote ambayo miradi hii inapita waweze kuchukua fursa za kujinufaisha kiuchumi ili waweze kupata fedha za kujikimu na kufanya maendleo.

Lakini barabara hizi zinatumia gharama kubwa na kumeanza kutokea uhalifu kwa watu kuharibu miondombinu, kwa watu kumwaga mafuta barabarani ambayo yanaharibu barabara lakini pia watu wanatupa takata kwenye madaraja na wengine wanaharibu miundombinu na kusababishia hasara Serikali.
 
naomba kuelewshwa kwanini mualiko ulikuwa mkubwa na wa kutoka mbali kwenye kuzindua 42km?
 
Arusha-Holili ni km 42??? Ufafanuzi please

Sent from my TECNO F3 using JamiiForums mobile app
Usipokuwa mwangalifu utapotea sana.

Kuna upotoshaji, tena wa maksudi kabisa katika uandishi wa habari hizi, hasa zinapoihusu Kenya.

Hiki kipande cha barabara ya Arusha, ni 42.4 Km tu; lakini habari yake inalazimishwa kuunganishwa na kile kipande kingine kilichopo Kenya, toka Voi hadi Taveta; ambacho pia kimejengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo hiyo, AfDB. Kwa hiyo habari inafanywa kama ni barabara moja iliyounganika, toka Arusha hadi huko Kenya ambako umbali wake ni zaidi ya 240-Km!

Kuna sababu za kufanya upotoshaji wa namna hii wa maksudi.
 
naomba kuelewshwa kwanini mualiko ulikuwa mkubwa na wa kutoka mbali kwenye kuzindua 42km?
Ngoja nijaribu kukujibu (kihuni kidogo)

Kwa sababu hii ni barabara yao hao waalikwa. Ndiyo maana kuna watu wamekazania sana kuipa jina barabara hiyo la "East African Road", yaani "Barabara ya Afrika Mashariki."

Sasa sijui kama umeelewa. Kama umeelewa, je, nami nikikuuliza swali utanisaidia kulijibu?

Swali langu ni hili: Je, mkopo wa ujenzi wa barabara hiyo ni nani ataulipa?

Hao watu wa Afrika Mashariki ndio watadaiwa na benki iliyotoa fedha za ujenzi, au mdaiwa ni serikali ya Tanzania kwa niaba yetu?

Nitashukuru sana kwa yeyote atakayesaidia kupata jibu.

Sasa tusubiri na ile nyingine iliyoahidiwa kwenye mpango huu huu; ile inayo ambaaamba kandokando ya bahari ya Hindi, ikitokea huko Malindi, hadi Bwagamoyo!

Na tusisahau, wakati huo huo, kama alivyokumbusjia mkuu 'Monttserrat' hapa chini:
Animalize huko aje kufungua potholes/ mahandaki ya nyakahura-rusumo-Burundi
Tukisema kuna njama dhidi yetu (Tanzania), katika mipango yote hii tunayosukumizwa kutoka nje, tunaonekana kama vichaa fulani hivi!
 
Back
Top Bottom