Rais Samia akemea urasimu Kituo cha Uwekezaji Tanzania

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuna kasumba ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wa nje na kuweka urasimu mwingi kwa wawekezaji wa ndani.

Amesema hayo alipokuwa akizindua kiwanda cha Faddy Fiber wilayani Mkuranga ambacho ni cha nne kwa ukubwa Afrika, na kitakuwa cha tatu kikikamilika kabisa.

Rais Amesema kuchelewesha uwekezaji kunachelewesha ajira kwa watu ambao wangeajiriwa katika viwanda husika, pia huchelewesha mapato ya kodi ambayo serikali inapata kwa viwanda kuendelea na shughuli.
 
Back
Top Bottom