Rais Samia afanya uteuzi. Katibu Mkuu Kiongozi ahamisha Vigogo 5 TANESCO

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Maharage Chande kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, akichukua nafasi ya Dkt. Tito Mwinuka

Kabla ya uteuzi huo, Chande alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Afrika Kanda ya Afrika Mashariki na Magharibi

Vilevile, Rais Samia amemteua Omari Issa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO

====

Rais Samia amemteua Hassan Seif Said kuwa Mkurugenzi Mkuu Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Kabla ya uteuzi, alikuwa Meneja wa Kanda Mwandamizi wa Kanda ya Mashariki TANESCO

Aidha, Michael Minja ameteuliwa kuwa Kamishna wa Petrol na Gesi, Wizara ya Nishati. Kabla ya kuteuliwa, Minja alikuwa Mkurugenzi Mkuu TIPPER

Vilevile, Rais amemteua Felschemi Mramba kuwa Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu

=====

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Hussein Kattanga amewahamisha Watumishi Waandamizi watano kutoka TANESCO kwenda Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambapo watapangiwa majukumu mengine

Waliohamishwa ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uwekezaji, Khalid James; Naibu Mkurugenzi Mtendaji Usambazaji na Masoko, Mhandisi Raymond Seya na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Usafirishaji, Mhandisi Isaac Chanje

Wengine ni Nyelu Mwamaja (Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi) na Amos Ndegi (Mwanasheria wa TANESCO)

View attachment 1952485

View attachment 1952487

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Bila katiba mpya pangua ,pangua ni KAZI bure
 
Udini Ni kitu mbaya Sana mkuu ndo maana inabidi itumike busara kubwa Sana hata kwenye promotion ya nafasi mbalimbali watu wasinuse hata harufu ya Jambo ilo watanzania tumejengwa kwa misingi ya umoja na mshikamo bila kujali itikadi zetu.
Nakubaliana na wewe mkuu, binafsi Mimi ntafocus zaidi katika Utendaji na Sio dini yako
 
Mimi heri Samia mara elfu kuliko magufuli bana tulikuwa tunaishi kwa hofu mda wote full mauonevu aaargh, Bora maustaadhi huwa hawaonei mtu vibaya atleast huwa wako fair, hawapendi kusifiwa wala kuabudiwa aisee
Kwenye kusifiwa na kuabudiwa huyu nae anapenda sana
Si uliona tukio la leo alivyokuwa akifurahi kuabudiwa na kupewa sifa za uongo. Eti hotuba ya kihistoria
 
Tuendelee kuabudu na kusifu za mapambio, walio fanya sherehe baada ya kifo chake hakika kwao kila kitu ni Safi,wateuzi ni furaha kwao!
 
Si ni juzi tu January aliwapiga mkwara TANESCO, imekuwaje tena anaibadilisha timu ile ile kabla hawajavurunda? Alikuwa hajui kuwa anaenda kuibadilisha? Na ule mkwara unawahusu hii timu mpya pia au?
unapotaka kumfanyia kitendo kibaya mtu usiemtaka kwenye mfumo wako,unamtafutia kajisababu..ukiona haingii kwenye 18 zako,basi unamfanyizia tu liwalo na liwe
ila hizo ni tabia za wanafiki wengi maana kama nia ilikuwa kuwaondoa wangefanya hivo tu hakuna ambaye angehoji maana mamlaka ni yao,ila siyo kuigiza kuwapa target uchwara then kuwatoa kabla hawashindwa hiyi target yako
 
M/kiti wa bodi Ya Tanesco Ni Muislam
DG Wa Tanesco pia ni Muislam
DG Wa Rea Ni Muislam Pia

Ts Islamic State

Bakwata Wanaupiga Mwingi Sana
Kabla ya hao 3 Waislam, vyeo hivyo vilikua vya watu gani na dini gani? Weka hapo kama katika 3 kulikua na Muislam 1 na Wakristo 2. Kama walikuwepo Wakristo3 na Muislam 0, basi udini ulikuwepo awamu ya 5 pia na hivyo Shut Up your a...!
 
Mkuu tupo pamoja......huyo ndio Rais Samia...zingine zote kelele tu...huu ndio mwingi anaoupiga sasa..
Mi binafsi sijui hivyo nashukuru kwa taarifa km una uhakika na hicho ulichokisema. Ombi langu tu ni kuwa tuletee pia takwimu za kipindi cha mwendazake. Fanya hivyo kumpendeza Mungu, fanya hivyo kuiokoa nafsi yako kutoka katika wingu zito la chuki na fitina!
 
Back
Top Bottom