Rais Samia achana na siasa za watemi na machifu, ni hatari, hazikusaidii na hazilisaidii taifa

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,105
35,046
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
 
Kuna mqmbo hutokea ili yaje kutengeneza kitu hapo baadae siku za usoni. Mambo hayo huwezi kuyazuia since yanajileta yenyewe naturally.

Chukulia mfano jinsia ke kushika hatamu za uongozi kwenye nafasi nyeti jambo ambalo kwa miaka 60 ya uhuru halijapata kuwepo.

Lakini yote hayo yatatengeneza jambo siku za usoni. Shida inakuja namna ya kung'amua jambo hilo litakalo tokea. Wazee wa trend reading kina paskali mayala wanaweza kuelezea vyema
 
Hii kitu imeandaliwa kimkakati na system ili kuangalia hoja za watu wata jitokeza vipi hasa juu ya issue ya Mbowe. Ndio maana waka kusanya watu Boma kama trial. Na ujumbe wameupata.
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Amefeli big time
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Atatuletea balaa. Huko tulishapita wala hatutaki kusikia machifu. Yuko desperate kutafuta political base. Nadhani 'reactionaries' wapinga maendeleo wanamshauri kwenye machifu. Uchifu unaambatana na desturi za imani za kishirikina umwinyi na kuleta ukabila na kunyanyasa wanawake. Hatutaki hiyo.
Hangaya hana uwezo kuongoza nchi hii. Ajitahidi tu ku maintain status quo hadi 2025 tuweze tafuta magufuli mpya.
Tumeona tayari yuko pro business people tofauti na desturi nchi hii tunataka kiongozi pro people... Maendeleo kwa umma sio watu wachache kuhodhi uchumi wa nchi kushirikiana na ubeberu wa kimataifa.
 
Atatuletea balaa. Huko tulishapita wala hatutaki kusikia machifu. Yuko desperate kutafuta political base. Nadhani 'reactionaries' wapinga maendeleo wanamshauri kwenye machifu. Uchifu unaambatana na desturi za imani za kishirikina umwinyi na kuleta ukabila na kunyanyasa wanawake. Hatutaki hiyo.
Hangaya hana uwezo kuongoza nchi hii. Ajitahidi tu ku maintain status quo hadi 2025 tuweze tafuta magufuli mpya.
Tumeona tayari yuko pro business people tofauti na desturi nchi hii tunataka kiongozi pro people... Maendeleo kwa umma sio watu wachache kuhodhi uchumi wa nchi kushirikiana na ubeberu wa kimataifa.
Ulipotaja Magufuli ndo ulipoharibu, kwa dunia ya wasitaarabu na yenye usitawi haiwezi kulilia kuongozwa na sadist Kama JPM. Taja mwingine plz, Kama Taifa tulikosea sana awamu ya tano, na Mungu akaamua kutuponya, usiturejeshe huko.
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Chief Marialle huwa analetewa fedha kutoka kwa Malkia Elizabeth wa Uingireza.
Hivyo kitendo cha samia kuungana naye kuna upigaji mkubwa wa fedha kutoka UK. Na picha zitatumwa UK nyingi sana Leo
 
Back
Top Bottom