The Monk
Platinum Member
- Oct 12, 2012
- 19,254
- 42,873
Tofauti ya mwalimu na viongozi wetu wa leo ni ile dhamira yao, dhamira ya mwalimu kuwa kiongozi ilikua ni kwa maslahi ya umma ndio maana alipotakiwa kuchagua kati ya kazi yake na siasa aliacha kazi na kujitoa kutetea wananchi, wakuu wetu wa leo jambo la kwanza ni watapata nini wao na vizazi vyao suala la wananchi halipo kabisa kwenye ajenda zao ndio maana wako tayari kufanya lolote kuhakikisha wanajilimbikizia mali huku wananchi wakiwa na hali ngumu. aiendelea kusisitiza kwamba yeye ni Mwalimu, ona tulivyo na viongozi ma Dr. wengi leo hata kama elimu yao haiwapi hiyo hadhi, ila kwa kutunukiwa ila wanaweza kukuweka ndani usipofuata protoko ya kutamka Dr. kwenye majina yao.