Rais, ni kweli kuwa huwa unakosea kuteua viongozi

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,087
6,568
Kama kuna eneo ambalo Watanzania wanakupongeza Rais JPM basi ni kuwa mkweli. Na jana ukiwa Kagera umekiri kuwa kweli huwa unakosea kuchagua viongozi.

Hilo la kule Ubungo la watoto wa shule kukaa chini, kusomea kwenye madarasa mabovu tena kuna RC, DC, Mkurugenzi na Mbunge wote wana CCM kweli limekuchefua, na sio jambo zuri.

Ila Mh Rais kwa kuwa umekiri kuwa huwa unakosea kuchagua viongozi sometimes, basi tambua sio hao tu wa Dar es Salaam uliokosea kuchagua maana wapo wengi.

Ukizunguka Tanzania kero kubwa ni hiyo. Uhaba wa vyumba vya madarasa huku viongozi uliowachagua wanakusanya kodi, ukosefu wa maji na huduma za afya ndio balaaa. Kwa ufupi Mh Rais ungekuwa unafuatilia kero za wananchi kupitia mitandao ya kijamii, ungepata ukweli kuwa 60% ya viongozi uliowachagua wanakuangusha na ulikosea kuwachagua. Maana hata utawala bora wengi ni bure kabisa.
 
Tatizo viongozi wengine ni Chadema moyoni nje CCM wanamwangusha mh rais makusudi ili wapate cha kupinga.

Nashauri aendelee kutumbua wote wanaoenda kinyume na mipango Yake.
 
Tatizo viongozi wengine ni Chadema moyoni nje CCM wanamwangusha mh rais makusudi ili wapate Cha kupinga.
Nashauri aendelee kutumbua wote wanaoenda kinyume na mipango Yake.
Kwamba mtu ni damu ya Chadema alafu analamba teuzi? Ili afanye hovyo! Sikubaliani na wewe.
 
Watoto wa Dada wamejaa Dar, anzia munene wa jiji hadi wakulu wa area ilala.
 
Kama kuna eneo ambalo Watanzania wanakupongeza Rais JPM basi ni kuwa mkweli. Na jana ukiwa Kagera umekiri kuwa kweli huwa unakosea kuchagua viongozi.

Hilo la kule Ubungo la watoto wa shule kukaa chini, kusomea kwenye madarasa mabovu tena kuna RC, DC, Mkurugenzi na Mbunge wote wana CCM kweli limekuchefua, na sio jambo zuri.

Ila Mh Rais kwa kuwa umekiri kuwa huwa unakosea kuchagua viongozi sometimes, basi tambua sio hao tu wa Dar es Salaam uliokosea kuchagua maana wapo wengi.

Ukizunguka Tanzania kero kubwa ni hiyo. Uhaba wa vyumba vya madarasa huku viongozi uliowachagua wanakusanya kodi, ukosefu wa maji na huduma za afya ndio balaaa. Kwa ufupi Mh Rais ungekuwa unafuatilia kero za wananchi kupitia mitandao ya kijamii, ungepata ukweli kuwa 60% ya viongozi uliowachagua wanakuangusha na ulikosea kuwachagua. Maana hata utawala bora wengi ni bure kabisa.
Huyu rais wa kata shida kweli.
 
Tatizo viongozi wengine ni Chadema moyoni nje CCM wanamwangusha mh rais makusudi ili wapate cha kupinga.

Nashauri aendelee kutumbua wote wanaoenda kinyume na mipango Yake.
Sema unione na Mimi katika teuzi za baada yatumbua.
 
Back
Top Bottom