Rais nakuomba umteue Joseph Kasheku Msukuma awe Waziri

Pilitoni

JF-Expert Member
Jul 11, 2011
1,190
497
Baada ya kuchoka na blaa blaa nyingi za hawa watu wanaojiita wasomi (wenye degrees, masters,PhD na maprofessa) naleta ombi kwako Mh Rais JPM umfikirie bwana Joseph Kasheku Msukuma kwenye nafasi ya uwaziri licha ya Elimu yake ya darasa la saba. Kama mtu aliyekwenda darasani kabisa anashindwa kutambua matatizo yanayoikumba jamii inayomzunguka anakwenda kununua gari la milioni 460 huyo ana msaada gani kwa nchi?

Mwingine alijua kabisa kwamba mwezi January 2021 wanafunzi waliomaliza darasa la saba wataingia kidato cha kwanza na kwa kuwa enrolment kwa sasa ni kubwa tulitegemea wanafunzi wa kidato cha kwanza kuwa wengi madarasa, viti na meza vingehitajika kwa wingi. Ni mwezi huu tu wa December ndio viongozi wetu wameliona hilo na kila mmoja anahangaika tu, hilo suala lilipaswa kuonwa mapema na kushughulikiwa huwa wanafanya nini? Facilities zote wanazo, magari, mishahara mizuri, posho nk wanafanya nini?

Leo utamsikia Jaffo anatamka hivi ilimradi anaongea tu ubunifu sifuri kabisa. Afrika Kusini waliwahi kuongozwa na Jacob Zuma mtu ambaye hakupitia hizi formal education za ma PhD, masters nk zinazotufanya tuwe wapumbavu wa kutokujua matatizo ya wananchi wetu na kuona gari la milioni 460 la mtu mmoja ndio bora sana kuliko maji, vituo vya afya, madawa, madawati na viti, ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na madaktari nk.

Kuna mwaka fulani Rais wa Iran Ahmed Nejad aliwajibu wabunge baada ya waziri wake mmoja kubainika kwamba aliforge cheti chake cha PhD ktk chuo cha Oxford uingereza na wabunge kumtaka waziri huyo ajiuzulu.

Rais aliwaambia alimteua huyo waziri kwa sababu ya utendaji wake mzuri wa kazi na siyo kwa sababu ya hayo makaratasi. Ni ukweli ulio wazi hawa watu tunaojidai nao kuwa wana Elimu zao wameshindwa kabisa kudeliver, Ndalichako kafanya nini Elimu?

Hatujachelewa, tujaribu hawa watu kama akina Msukuma wanaweza kufanya makubwa katika maendeleo kuzidi hawa tulionao.
 
Nami naunga mkono hoja hi maana hata katika maisha yetu ya kawaida sisi ambao hatukusoma tunadharaulika lakini sisi ndio tumetoboa kuliko hata hao wanaojiita wasomi maana sisi kazi yoyote tunafanya,Sasa hao wasomi unakuta Wana nadharia nyingi kuliko vitendo hivo mkulu akiwateua akina Msukuma na Kibajaji kazi itaenda vema maana wao usomiusomi tupa Kule kinacho baki ni KAZI TU.
 
Matapeli wanakuwa mawaziri kazi ipoo. Mwambie Msukuma arudishe ata robo ya hela alizotapeli kuna maisha baada ya hapa.
 
Abaki kuww Mbunge ili aendelee kulijenga taifa kwa uhuru zaidi; akiwa waziri mishughuliko inamwelemea.

Msukuma apewe uwaziri kwavile ni Msukuma? Au kwavile wasukuma wengi wamepata uteuzi? Mbona mnataka kushusha hadhi ya uwaziri!
 
Msukuma apewe uwaziri kwavile ni Msukuma? Au kwavile wasukuma wengi wamepata uteuzi? Mbona mnataka kushusha hadhi ya uwaziri!!!!
What matters ni kuchapa kazi, haijalishi fimbo unayotumia kuchapia ni bakora ama rungu ama mnepo ama mjeledi. Kipimo cha elimu kwenye makaratasi haitusaidii sana hasa ukizingatia makaratasi hayo wengi japo wanasema wameyatolea jasho, muda na pesa, but kwa kiasi kikubwa wamechakachua. "Mheshimiwa Spika, naomba hawa wasinikumbushe niwaoneshe maksi zao walizopata darasani."~ Prof. Kabudi.
 
What matters ni kuchapa kazi, haijalishi fimbo unayotumia kuchapia ni bakora ama rungu ama mnepo ama mjeledi. Kipimo cha elimu kwenye makaratasi haitusaidii sana hasa ukizingatia makaratasi hayo wengi japo wanasema wameyatolea jasho, muda na pesa, but kwa kiasi kikubwa wamechakachua. "Mheshimiwa Spika, naomba hawa wasinikumbushe niwaoneshe maksi zao walizopata darasani."~ Prof. Kabudi.

Unategemea aseme nini mtu aliyeokotwa jalalani; lazima atajipendekeza kwa aliyemuokota!!! Kazi ni muhimu lakini ni muhimu zaidi hiyo kazi iwe ya kiwango ambayo ni nadra kuipata kutoka kwa wenye elimu ya UPE.
 
Baada ya kuchoka na blaa blaa nyingi za hawa watu wanaojiita wasomi (wenye degrees, masters,PhD na maprofessa) naleta ombi kwako Mh Rais JPM umfikirie bwana Joseph Kasheku Msukuma kwenye nafasi ya uwaziri licha ya Elimu yake ya darasa la saba. Kama mtu aliyekwenda darasani kabisa anashindwa kutambua matatizo yanayoikumba jamii inayomzunguka anakwenda kununua gari la milioni 460 huyo ana msaada gani kwa nchi?

Mwingine alijua kabisa kwamba mwezi January 2021 wanafunzi waliomaliza darasa la saba wataingia kidato cha kwanza na kwa kuwa enrolment kwa sasa ni kubwa tulitegemea wanafunzi wa kidato cha kwanza kuwa wengi madarasa, viti na meza vingehitajika kwa wingi. Ni mwezi huu tu wa December ndio viongozi wetu wameliona hilo na kila mmoja anahangaika tu, hilo suala lilipaswa kuonwa mapema na kushughulikiwa huwa wanafanya nini? Facilities zote wanazo, magari, mishahara mizuri, posho nk wanafanya nini?

Leo utamsikia Jaffo anatamka hivi ilimradi anaongea tu ubunifu sifuri kabisa. Afrika Kusini waliwahi kuongozwa na Jacob Zuma mtu ambaye hakupitia hizi formal education za ma PhD, masters nk zinazotufanya tuwe wapumbavu wa kutokujua matatizo ya wananchi wetu na kuona gari la milioni 460 la mtu mmoja ndio bora sana kuliko maji, vituo vya afya, madawa, madawati na viti, ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na madaktari nk.

Kuna mwaka fulani Rais wa Iran Ahmed Nejad aliwajibu wabunge baada ya waziri wake mmoja kubainika kwamba aliforge cheti chake cha PhD ktk chuo cha Oxford uingereza na wabunge kumtaka waziri huyo ajiuzulu.

Rais aliwaambia alimteua huyo waziri kwa sababu ya utendaji wake mzuri wa kazi na siyo kwa sababu ya hayo makaratasi. Ni ukweli ulio wazi hawa watu tunaojidai nao kuwa wana Elimu zao wameshindwa kabisa kudeliver, Ndalichako kafanya nini Elimu?

Hatujachelewa, tujaribu hawa watu kama akina Msukuma wanaweza kufanya makubwa katika maendeleo kuzidi hawa tulionao.
Sababu zako hazina mashiko. Wasomi wetu kushindwa kudeliver haitoi sababu ya kuweka mtu wa darasa la saba. Acha utani mjomba. Na pia kuwa msomi sio kwamba ni tiketi ya kudeliver. Mfumo wetu hauwapi nafasi wasomi wenye uwezo wa kuleta mchango. Hao unawaona huwezi sema ni representattive sample ya wasomi. Wasomi wa kweli hawaitaki siasa na ndo tatizo linapoanzia. Pia mifano yako imekosa analysis ya kutosha. Mfano Jacob Zuma amedhihirisha nini katika kipindi chake cha uongozi? Hakuna kipindi ambacho South Africa ilipata kiongozi mjinga kama enzi za Zuma. Mtu anaundiwa baraza la mawaziri na wahindi kina Gupta. Kina Gupta walitake advantage ya limitation yake kwenye analytical skills. Katika kipindi ambacho uchumi ulivurugwa Afrika Kusini ni kipindi cha Zuma. Umewahi kufuatia ishu ya state capture iliyofanya Zuma akajiuzulu kuhofia impeachment au unaongea tu. Tunapoongelea uongozi katika ngazi ya taifa angalau kiwango fulani cha elimu kinahitajika. Nafasi ya uwaziri ni ya kisera zaidi, huwezi kuweka mtu kama Msukuma enzi hizi, unategemea ataenda kuongea na delegation mfano ya EU au World Bank kuhusu masuala ya kisera kwenye elimu ya msingi au sekondari? Kweli upo serious?
 
Unategemea aseme nini mtu aliyeokotwa jalalani; lazima atajipendekeza kwa aliyemuokota!!! Kazi ni muhimu lakini ni muhimu zaidi hiyo kazi iwe ya kiwango ambayo ni nadra kuipata kutoka kwa wenye elimu ya UPE.
Unajua yale makaratasi yaitwayo vyeti huwa hayasimami yenyewe. Huwa yanawakilisha maarifa akilini inayoaminika kwamba inaweza kutafsirika kivitendo na kuleta natija hanifu kwenye jamii. Sasa ikitokea manufaa hayo hayaoneshi uwiano mzuri kati ya elimu kubwa ya mtaalamu na output ("weka-nje"!??) zinazotarajiwa, lazima tu iwepo "kwere" kuhoji uhalali wa ubora wa elimu yake. Kwa mantiki hiyohiyo, muungwana wa kawaida asiye na cheti rasmi cha kutambulisha na kutangaza uwezo wa akili yake na ustadi wa utendaji wake, lakini matokeo yake ni ya kutamanisha, kwa nini asistahili hadhi yake halali??? Na wala siyo wazo geni: ndiyo maana ya udokta wa heshima. Hii ni kusema kwamba kuna wengine vyeti vyao huvipatia skuli na wengine wanapatia skili fildi. "There are three methods of gaining wisdom: reflection, imitation, and experience."~Confucius
 
Baada ya kuchoka na blaa blaa nyingi za hawa watu wanaojiita wasomi (wenye degrees, masters,PhD na maprofessa) naleta ombi kwako Mh Rais JPM umfikirie bwana Joseph Kasheku Msukuma kwenye nafasi ya uwaziri licha ya Elimu yake ya darasa la saba. Kama mtu aliyekwenda darasani kabisa anashindwa kutambua matatizo yanayoikumba jamii inayomzunguka anakwenda kununua gari la milioni 460 huyo ana msaada gani kwa nchi?

Mwingine alijua kabisa kwamba mwezi January 2021 wanafunzi waliomaliza darasa la saba wataingia kidato cha kwanza na kwa kuwa enrolment kwa sasa ni kubwa tulitegemea wanafunzi wa kidato cha kwanza kuwa wengi madarasa, viti na meza vingehitajika kwa wingi. Ni mwezi huu tu wa December ndio viongozi wetu wameliona hilo na kila mmoja anahangaika tu, hilo suala lilipaswa kuonwa mapema na kushughulikiwa huwa wanafanya nini? Facilities zote wanazo, magari, mishahara mizuri, posho nk wanafanya nini?

Leo utamsikia Jaffo anatamka hivi ilimradi anaongea tu ubunifu sifuri kabisa. Afrika Kusini waliwahi kuongozwa na Jacob Zuma mtu ambaye hakupitia hizi formal education za ma PhD, masters nk zinazotufanya tuwe wapumbavu wa kutokujua matatizo ya wananchi wetu na kuona gari la milioni 460 la mtu mmoja ndio bora sana kuliko maji, vituo vya afya, madawa, madawati na viti, ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na madaktari nk.

Kuna mwaka fulani Rais wa Iran Ahmed Nejad aliwajibu wabunge baada ya waziri wake mmoja kubainika kwamba aliforge cheti chake cha PhD ktk chuo cha Oxford uingereza na wabunge kumtaka waziri huyo ajiuzulu.

Rais aliwaambia alimteua huyo waziri kwa sababu ya utendaji wake mzuri wa kazi na siyo kwa sababu ya hayo makaratasi. Ni ukweli ulio wazi hawa watu tunaojidai nao kuwa wana Elimu zao wameshindwa kabisa kudeliver, Ndalichako kafanya nini Elimu?

Hatujachelewa, tujaribu hawa watu kama akina Msukuma wanaweza kufanya makubwa katika maendeleo kuzidi hawa tulionao.

Mkuu unataka kusema usomi unaharibu talanta ya uongozi ya mtu ?

Mi nadhani ni lazima tukubali kwamba wapo viongozi wazuri waliosoma na wasiosoma. Pia kwa upande mwingine, wapo viongozi wabaya waliosoma na wasiosoma.

Na kama unamaanisha unachokiwasilisha hapa (kama kilivyo), basi JPM (Msomi wa shahada tatu) amwachie Urais Musukuma (darasa la saba) maana ''U la saba'' ni dalili ya kuwa mtu huyu ni kiongozi mzuri zaidi.
 
Unajua yale makaratasi yaitwayo vyeti huwa havisimami vyenyewe. Huwa vinawakilisha maarifa akilini inayoaminika kwamba inaweza kutafsrika kivitendo na kuleta natija hanifu kwenye jamii. Sasa ikitokea hauonekani uwianifu kati ya elimu kubwa ya mtaalamu na output ("weka-nje"!??) zinazotarajiwa, lazima tu iwepo "kwere" kuhusiana na uhalali wa ubora wa elimu yake. Kwa mantiki hiyohiyo, muungwana wa kawaida asiye na cheti rasmi cha kutambulisha na kutangaza uwezo wa akili yake na ustadi wa utendaji wake, lakini matokeo yake ni ya kutamanisha, kwa nini aaistahili hadhi yake halali??? Na wala siyo wazo geni: ndiyo maana ya udokta wa heshima. Hii ni kusema kwamba kuna wengine vyeti vyao huvipatia skuli na wengine wanapatia skili fildi. "There are three methods of gaining wisdom: reflection, imitation, and experience."~Confucius

Haya Profesa, katika hizo methods zako tatu za justification ya Msukuma kuwa Waziri ili nae aokotwe jalalani, yeye una muweka kwenye category gani?
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom