Babu Kijiwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2010
- 4,762
- 4,576
- Thread starter
- #21
Kwani nimesema Majaliwa hafai,?Ukiona Mtu anaanzisha Uzi halafu mwishoni anawaomba Wahusika wasiufute jua hata Yeye ameshajua kuwa huo Uzi una Pumba nyingi hivyo anawahi Kujihami. Bado sijaona Mapungufu yoyote wa Waziri Mkuu wa sasa Mheshimiwa Kassim Majaliwa Kassim na ninachojua tu huku nikiwa na uhakika nacho tena kwa 100% kuwa kama nchi ya Tanzania iliwahi Kubarikiwa kuwapata Mawaziri Wakuu wa kweli, wachapa Kazi na wanaojitoa kabisa kwa Tanzania yao bila Kuchoka na hata muda mwingine huwa wanayafuta Makosa ya Marais wao Kiutendaji basi alikuwa ni Hayati Edward Moringe Sokoine na sasa ni huyu Kassim Majaliwa Kassim. Kwako Mheshimiwa Rais JPM wala usipoteze muda wako Kumbadilisha huyu Waziri Mkuu wao Mahiri kwa sasa na nakushauri sana kuwa ukiendelea Kutuongoza kwa Awamu yako ya pili na ya mwisho ya 2020 hadi 2025 endelea nae Kassim Majaliwa Kassim na hutokuja Kujutia kuwa nae katika Safu yako ya Uongozi / Utawala.