Rais na Wabunge Waliwakampeni Pamoja Vyama Vyote (UKAWA), Viti Maalum Vyote Kwa CHADEMA Pekee Yake?

NAMNA WABUNGE WA VITI MAALUMU WANAVYOPATIKANA.

NA: Joseph Mshinga.

1.idadi yote ya wabunge wa viti maalumu katika bunge ni asilimia 40 ya viti vyote vya bunge katika majimbo yote(40% of all seats/constituencies ).

idadi ya viti vya ubunge ama majimbo kwa sasa ni 264.

40% ya 264 ni ngapi? unaweza kupiga kujua kutakuwa na jumla ya viti maalum wangapi.

FURSA YA CHAMA KUPATA WABUNGE VITI MAALUMU.

kwanza ili chama husika kiweze kupata wabunge wa viti maalumu ni sharti chama hicho kiwe na jumla ya kura zisizopungua asilimia 5 ya kura zote za wagombea wote wa ubunge wa chama hicho katika jumla ya kura zote za wabunge wa vyama vyote.

Hii bila kujalisha kama chama kimeshinda wabunge ama hakikushinda katika majimbo kiliyogombea. Hata kama chama kimeshindwa katika majimbo yote lakini kikafanikiwa kupata kura zinazofikia asilimia 5 ya kura zote za wabunge wa vyama vyote basi chama hicho kinapata fursa ya kuwa na wabunge wa viti maalumu.

kwa hiyo ieleweke wazi kuwa idadi ya wabunge walioshinda haitumiki kupata wabunge viti maalumu.

mbunge aliyeshinda kutoka jimbo la wapiga kura wachache mathalani majimbo ya Zanzibar atakuwa na kura chache pengine kuliko mtu aliyeshindwa katika jimbo la wapiga kura wengi kama majimbo ya mjini Dar es salaam.Hivyo huyu aliyeshindwa anaweza kuchangia zaidi kupatikana kwa mbunge wa viti maalumu kuliko aliyeshinda kwa mfano huu niliotoa.

na kwa vyovyote vile majimbo ya Zanzibar yanachangia asilimia ndogo sana katika viti maalumu. Mchango wa kura za viti maalumu katika majimbo yote ya Zanzibar yenye jumla ya wapiga kura laki 4 na ushehe ni mdogo kuliko mchango wa majimbo yote ya mkoa wa Shinyanga ulio na wapiga kura wapatao laki 7.

kwa hiyo hapa ni mchezo wa kupata kura nyingi zaidi na si kushinda viti vingi zaidi vya ubunge.

MGAWANYO WA HAO WABUNGE.

ili kupata kila chama kinapaswa kugawiwa wabunge wangapi inabidi asilimia ya kura za wabunge wote waliogombea katika kila chama dhidi ya kura zote za vyama vinavyostahili kupata wabunge viti maalumu ikokotolewe na hiyo itasaidi kujua kila chama kitapata asilimia ngapi kati ya hao wabunge wote(40% of 264). Idadi hiyo ipe jina la M.

kuna mazingira ambayo chama hakikusimamisha wagombea ubunge ama mgombea ubunge wake alipita bila kupingwa katika jimbo. Katika mazingira haya hakuna kura halali za mbunge kwa chama husika zilizopigwa na wapiga kura.

kwa hiyo ili kupata idadi ya kura zote zingatia mambo yafutayo.

1.Jumla ya kura zote za wagombea ubunge wa chama hicho katika maeneo kilichosimamisha wagombea ni sehemu ya kura zinazotumika. ziite jina la kura X.

2.Jumla ya kura zote za mgombea urais katika maeneo ambayo chama hicho hakikusimamisha mgombea ubunge zitahesabiwa kuwa ni kura za ubunge za chama hicho, Ziite jina la kura Y.

Mfano katika jimbo la Kinondoni ambapo Chadema haikusimamisha mgombea ubunge bali alisimamishwa wa CUF (UKAWA) basi kura za Edward Lowassa(mgombea Urais) katika Jimbo hili zitahesabiwa kama kura za mgombea ubunge wa chadema kwa swala la viti maalumu katika jimbo hili la kinondoni.

na hizo za mbunge wa CUF kinondoni zinaingia katika hesabu ya CUF. zile za mgombea wa CCM alieshindwa bwana IDD AZAN zinaingia katika hesabu ya CCM.

3.kama chama kimepita bila kupingwa katika jimbo. Maana yake uchaguzi haukufanyika kabisa kwa kuwa mgombea alikuwa mmoja tu na hivyo hakuna kura zilizopigwa. Kwa mazingira haya hapa kura za Rais hazitahusika. Kinachofanyika ni kukokotoa asilimia 51 ya wapiga kura wote walioandikishwa katika jimbo hilo bila kujali walijitokeza wote kupiga kura ama laa. (51% of registered voters in that constituency).Ziite jina la kura Z.

asilimia hizo zinahesabiwa kuwa ni kura halali za mgombea huyo aliyepita bila kupingwa ambazo zinapaswa kutumika wakati wa kukokotoa wabunge wa viti maalumu.

kwa kuwa mwaka huu hakuna mbunge aliyepita bila kupingwa basi kipengere cha 1 na 2 ndivyo vitatumika kukokotoa idadi ya vitu maalumu kwa kila chama.

hesabu ni kama hivi.

X + Y + Z= kura zote za ubunge za kila chama.

NB:
1.kama chama hakima mgombea urais Y= 0 kwenye mazingira ya Y.

2. kwa kuwa hakuna mbunge aliyepita bila kupingwa nchi nzima basi Z=0 kila mahali.

(a). Chadema=X+Y+Z= P1

(b). CUF=X+Y+Z=P2

(c). CCM=X+Y+Z=P3

kura zote walizopigiwa wabunge.

P1+P2+P3+P4+............+Pn=W (Jumla ya kura za wagombea ubunge wote toka vyama vyote vilivyosimamisha wagombea). W itatumika tu kujiridhisha kama chama kinastahili kupata wabunge viti maalumu na si vinginevyo.

hapa kuna kura za vyama ambavyo havitapata viti maalumu kama ACT, NRA, CHAUMA nk nazo zinaingizwa katima jumla ya kura zote zilizopigwa kwa wagombea wabunge wote.

lakini mgawanyo wa asilimia kwa vyama utahusisha tu vyama vyenye sifa ya kupata wabunge wa viti maalumu.

kwa hiyo chukua P1+P2+P3=Q. na utafute asilimia ya kila chama katika hivyo vitatu.

lakini sina uhakina kama CUF imefikisha asilimia 5 ya kura zote kwa maana ya P2.kwa kuwa wagombea wengi wametoka Zanzibar kuliko na wapiga kura wachache ama kura chache.(mpaka kujiridhisha kwa CUF).

(i). viti maalumu chadema.

(P1/Q x 100) x M= Viti maalumu chadema.

(ii). viti maalumu CUF.
( P2/Q x 100) x M=viti maalumu CUF.

(iii). viti maalumu CCM.

(P3/Q x 100) x M= viti maalumu CCM.

M ni jumla ya wabunge wote wa viti maalumu bungeni ambao ni (40/100 x 264).

NA: Joseph Mshinga

signature: 04/11/2015.
 
Nashauri hospital za mirembe ziongezwe ili matahira kama mleta uzi wakatibiwe mapema vinginevyo ifikapo mwaka 2020 tutakuwa na idadi maradufu ya matahira. 1.Elimu......2.Elimu.........3.Elimuuuuuuuuu!!
 
Nakumbaliana na wewe Mkuu! Na huo ndo utaratibu!
Kwa nini wasifanye huo mgawanyo wa ruzuku kwa vyama vyote nje ya utaratibu wa NEC?
Hii iendane na ukubwa wa chama! La sivyo vyama vingime vimefanya kazi ya kanisa kuisaidia CHADEMA kupata ruzuku kumbwa, wabunge wa kuchanguliwa na kuteuliwa (viti maalum) wengi! Kwa nini mgombea uraisi (Lowass) amepewa nafasi nne? Kwa nini Mbatia asipewe nafasi tatu? NLD nafasi moja? Haji Duni nafasi mbili?

Kazi gani ya Kanisa viliyofanya,Mbatia Bila Ukawa huenda Ubunge angekosa.NLD Kabla yake kilikuaje? CUF Zanzibar wamepata neema unataka nini tena?
 
Nakumbaliana na wewe Mkuu! Na huo ndo utaratibu!
Kwa nini wasifanye huo mgawanyo wa ruzuku kwa vyama vyote nje ya utaratibu wa NEC?
Hii iendane na ukubwa wa chama! La sivyo vyama vingime vimefanya kazi ya kanisa kuisaidia CHADEMA kupata ruzuku kumbwa, wabunge wa kuchanguliwa na kuteuliwa (viti maalum) wengi! Kwa nini mgombea uraisi (Lowass) amepewa nafasi nne? Kwa nini Mbatia asipewe nafasi tatu? NLD nafasi moja? Haji Duni nafasi mbili?

Mbatia atapewaje wakati yeye siyo mwanachadema? na hata akipewa atamweka nani wakati inatakiwa amweke mwanachadema?
 
Aliyekuwa anagombea na Julius Mtatiro naye amepewa viti maalum! Hii ni zawadi ya kumwangusha Mtatiro?
Kuhusu Segerea suala hilo limeishaongelewa sana na time ndio waliofanya makusudi hayo, hivyo huyo Dada alijitoa na ushahidi upo na kwa kufanya hivyo kupewa ubunge ni haki yake kwani alikubali kutogombea.
 
ACT na TLP hvyo ni kwa uchache tu vipo UKAWA? Wana wabunge wangapi viti maalum!? Tuanzie hapo halaf tutaendelea mdogo mdogo mpaka uelewe,

NB; WANDUGU TUSITUMIE KICHWA KUBEBEA MASIKIO
 
Nina uhakika unao uwezo wa kumwelewesha huyu mleta mada, ila kwakuwa unaona ni kitu ambacho kikiachwa kikapotoshwa na kueleweka vibaya inatoa pointi kwa chama chako CCM, ndo maana unashabikia tu.

Hivi hakuna siku nafsi inakusuta unapoamua kwa makusudi kabisa kushabikia uongo, uchonganishi, uzushi, chuki, kukoseana heshima, kudhalilisha binadamu wenzio, nk?

Kama unavyopenda kutuuliza humu kuwa hizi shule tulienda kusomea ujinga, nami nikuulize: hizo ibada huwa unafanya kwa mola wako, au kwa shetani?

So disgusting!!

Naona yamekuingia mpaka umeshindwa kujibu unaanza kuhororoja na kubwabwaja bila mpango.

Indeed you'll be disgusted, what else?
 
Mbatia atapewaje wakati yeye siyo mwanachadema? na hata akipewa atamweka nani wakati inatakiwa amweke mwanachadema?
CHADEMA inawatu wa ajabu kweli! Yule wa CCM amepewaje viti maalum? Ruth Molel amepewaje?
 
mheshimiwa sana lowassa kapewa nafasi nne kuweka wabunge wa viti maalum.

Sina hakika kama kikweke au magufuli walipata fursa hiyo ccm.

Kila chama na demokrasia yake.

chadema imenunuliwa na el kwa hiyo lazima mnunuzi ajipendelee jk na magufuli si wamilki wa ccm bali ni viongozi wa chama hilo kwa chedma hakuna kwani kule kuna mmiliki na ndiyo mwenye sauti ya mwisho
 
Ndugu Wanabodi!
Ninauliza mgawanyo vya viti maalum-wabunge kwa vyama vyote vinavyounda UKAWA.
Nakumbuka kwamba vyama hivi vilioamua kusimamisha mgombea mmoja wa Uraisi na wabunge katika majimbo.
Kwa maana hiyo, CHADEMA ndo iliyojulikana kusisimamisha mgombea uraisi aliyekuwa akiungwa mkono na vyama
vyote vinavyounda UKAWA. Kwa maana hiyo kura alizopata Lowassa ni za wanaUKAWA wote. Vivyo hivo kura walizopata wabunge wa Ukawa ni za wanaUKAWA wote.
Kutokana na kura hizo ndizo zinapelekea kutolewa kwa viti maalumu. Sasa vyama vingine vinavyounda ukawa ukiondoa CDM vimepata nafasi za viti maalum? Kama siyo, hii ndo issue niliyokuwa naisema kwamba vyama vingine vitakuja kuingizwa mjini.

Mwenye majibu aje atufafanulie hapa!

Aksanteni!

Idadi ya viti kwa kila chama ilitengenezwa na NEC, CUF wakapata viti kumi japo hawakuwa na mgombea Urais. ACT hawakupata hata kiti kimoja japo wao pia walikuwa na mgombea. Majibu ya swali lako yanapatikana NEC.
 
No any correction.The target found.
Navyojua mimi idadi ya viti maalum hutokana na idadi ya wabunge wa majimbo

Idadi ya kura za urais inamata kwenye kukokotoa ruzuku ya chama

I stand to be corrected anyway
 
We kweli umesoma shule za taka.
Inamaana hujaona msaada wa UKAWA kwa CUF?
Kumuelewa mwenzio kunahitaji uelewa vile vile!
Nimekwambia hapo juu kwamba wanavisaidiaje hivi vyama vingine?
Kama walivyomkopa Duni kwa umakamu wa uraisi, wangekopa watu kutoka vyama vingine! Kama iliwezekana kwenye ungombea mwenza, kwa nini haiwezekani kwenye viti maalumu?
Kumshikisha mtu kadi ya CDM kwa ajili ya kupata ubunge kwa manufaa ya chama chake haiwezekani?
 
Ndugu Wanabodi!
Ninauliza mgawanyo vya viti maalum-wabunge kwa vyama vyote vinavyounda UKAWA.
Nakumbuka kwamba vyama hivi vilioamua kusimamisha mgombea mmoja wa Uraisi na wabunge katika majimbo.
Kwa maana hiyo, CHADEMA ndo iliyojulikana kusisimamisha mgombea uraisi aliyekuwa akiungwa mkono na vyama
vyote vinavyounda UKAWA. Kwa maana hiyo kura alizopata Lowassa ni za wanaUKAWA wote. Vivyo hivo kura walizopata wabunge wa Ukawa ni za wanaUKAWA wote.
Kutokana na kura hizo ndizo zinapelekea kutolewa kwa viti maalumu. Sasa vyama vingine vinavyounda ukawa ukiondoa CDM vimepata nafasi za viti maalum? Kama siyo, hii ndo issue niliyokuwa naisema kwamba vyama vingine vitakuja kuingizwa mjini.

Mwenye majibu aje atufafanulie hapa!

Aksanteni!
Kwa nin usiconfirm tu kuwa ikitokea hivyo basi wabunge wa viti maalum wa CHADEMA ni wa UKAWA wote! Pamoja na hayo, jitathmini vizuri upo outdated sana na habari, au hili suala lilishafafanuliwa mara nyingi sana. Kuna nyuzi kibao hum kuhusiana na hilo.
 
Back
Top Bottom