Utingo
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 10,270
- 8,031
badilisha title. Unadai ametoa onyo kisha content unasema amewasihi-begged.....??RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewanasihi wafanyabiashara kuacha kutumia mgogoro wa Urusi na Ukraine kama kisingizio cha kupandisha bei za bidhaa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Dk. Mwinyi alieleza hayo jana katika risala maalum aliyoitoa yenye lengo la kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa mwaka 1443 hijria, aliyoitoa kupitia vyombo vya habari.
Alisema serikali hatua haitosita kuwachukulia kali wafanyabiashara kinyume na maagizo inayoyatoa, kwani amepata taarifa kwamba bidhaa nyingi zitakazouzwa kwa kipindi cha mwezi wa Ramadhani zimeingizwa nchini kabla kuibuka kwa mgogoro wa Urusi na Ukraine.
Dk. Mwinyi aliwahakikishia wafanyabiashara na wananchi kuwa Serikali itaendelea kufuatilia mwenendo wa uchumi wa dunia na gharama za kufanya biashara duniani, ili kuhakikisha kwamba bei za bidhaa zinazouzwa kwenye maduka ya jumla na rejareja zinaakisi gharama na uwezo wa kipato cha wananchi.
Aliwahimiza wakuu wa taasisi zinazoshughulika na biashara, mikoa, masheha, wahakikishe wanafuatilia wakuu wa wilaya na kwa karibu mwenendo wa bei za bidhaa katika maeneo yao ya utawala na kuwachukulia hatua za kisheria wanaojaribu kukiuka sheria na maagizo ya serikali.
Alisema kuwa wakati wa Ramadhani ukikaribishwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa dunia bado haiko katika hali ya kawaida, kama ilivyokuwa kabla ya kuzuka kwa janga la UVIKO 19, mwishoni mwa mwaka 2019.
Aliongeza kuwa pamoja na kuendelea kuwepo kwa changamoto zilizoambatana na maradhi hayo, hivi karibuni mgororo wa vita baina ya Taifa la Urusi na Ukraine umeibua taharuki mpya kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii duniani kote.
Alieleza kuwa kwa kuzingatia hali ya uchumi nchini pamoja na uchumi wa dunia kwa jumla amekuwa akiitisha vikao na watendaji wa taasisi mbali mbali za Serikali kwa lengo la kujadili maendeleo ya biashara nchini ambapo amekuwa akitoa maagizo na maelekezo yenye lengo la kudhibiti hali ya upandaji wa bei za vyakula, mafuta ya petroli na bidhaa nyengine muhimu.
Dk. Mwinyi alisema kuwa kwa kipindi cha mwezi wa Ramadhani, serikali imepunguza viwango vya kodi kwa bidhaa muhimu ambapo yaliyofanywa yamezingatia maslahi maamuzi katika suala hilo ya wananchi na wafanyabiashara ambapo serikali imeweka bei elekezi.
Chanzo: Zanzibar Leo