Rais Museveni ataka watuhumiwa wa makosa makubwa wasipewe dhamana

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Rais Yoweri Museveni wa Uganda anataka washukiwa wa mauaji na makosa mengine makubwa kama uhaini wasipewe dhamana lakini jaji mkuu ametahadharisha kuwa mabadiliko hayo yanakinzana na utawala wa sheria na haki za binadamu

Kwa muda wa miaka 10 sasa, rais Museveni amekuwa akikariri mtazamo wake kuwa washukiwa katika hatia za mauaji, uhaini, ubakaji na unajisi wasipewe dhamana hata kidogo. Amefufua tena mjadala huo siku ya Jumatatu alipoongoza sherehe za kumbukumbu za marehemu jaji mkuu Benedicto Kiwanuka aliyeuawa katika utawala wa Iddi Amin akisema kuwa jamii huona kero kubwa kuona mtu ambaye anashukiwa kutenda mauaji akiwa huru huku kesi dhidi yake ikiendeshwa kwa muda mrefu.

Rais alikuwa akimjibu jaji mkuu kwenye sherehe hizo aliyesisitiza kuwa kamwe kitengo cha sheria hakiwezi kusaliti katiba ya nchi kwa kuwanyima dhamana washukiwa kama anavyopendekeza yeye.

Jumuiya ya wanasheria na wanaharakati wa haki za binadamu wameendelea kupinga wazo la Museveni kwamba sheria zifanyiwe mageuzi dhamana ya mahakama kwa wanaoshukiwa kutenda uhalifu wa hali ya juu wasiachiwe.

Wameunga mkono jaji mkuu Alphose Owiny-Dollo kwa kumwambia waziwazi rais Museveni ambaye ndiye alimteua kuhusu msimamo wa kitengo cha sheria ambacho ni moja kati ya mihimili mitatu ya serikali mingine ikiwa bunge na baraza la mawaziri.
 
Back
Top Bottom