Rais Museveni alijisikiaje baada ya kuona video na taarifa za kifo cha huyu mtu?

feyzal

JF-Expert Member
Apr 20, 2016
6,784
12,594
Raia wa sehemu hiyo ni watu wanaounga mkono harakati za Boby Wine kwa yanayofanywa na Museveni huko Uganda aliyepokea kipigo na kufa baadae baada ya kipigo anajulikana kwa jina la Sweet Pepsi (Ssewankambo Hannington).

================

Ssewankambo Hannington maarufu kama Sweet Pepsi ambaye alipigwa na wanausalama wa Uganda katika maandamano ya ‘’Free Bobi Wine’’ mwaka jana, amefariki dunia.

Taarifa kutoka kwa wanafamilia yake wanasema kijana huyo aliyekuwa mfuasi wa harakati za ‘’People Power’’ alivuta pumzi yake ya mwisho siku ya Jumatano.

Mwanahabari wa BBC Atulinda Allan ambaye alimsaidia Sweet Pepsi kwa kumfunga ‘bandage’ baada ya kupwigwa na wanajeshi amesema kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii kuwa amepata taarifa za kifo hicho kutoka kwa dada wa Sweet Pepsi.

IMG_20191101_071209.jpeg
IMG_20191101_071159.jpeg
IMG_20191101_071153.jpeg

 
Wanywa damu ulishaona wanasikitika? Nadhani alitaka akailambe kabisa. Samahani kwa maneno haya ila inatia uchungu.
 
Ukiwa chama pinzani lazima upate tabu sana ! I hope Bob wine hatapoteza focus kwenye harakati zake
Rest easy young soul
 
Sidhani kama kuna kiongozi yeyote kwenye tukio kama hilo yakayokea hayo ati atakisikia vibaya hakuna
 
Raia wa hiyo sehemu ni watu wanaounga mkono harakati za Boby Wine kwa yanayofanywa na Museveni huko Uganda aliyepokea kipigo na kufa baadae baada ya kipigo anajulikana kwa jina la Sweet Pepsi (Ssewankambo Hannington).

================

Ssewankambo Hannington maarufu kama Sweet Pepsi ambaye alipigwa na wanausalama wa Uganda katika maandamano ya ‘’Free Bobi Wine’’ mwaka jana, amefariki dunia.

Taarifa kutoka kwa wanafamilia yake wanasema kijana huyo aliyekuwa mfuasi wa harakati za ‘’People Power’’ alivuta pumzi yake ya mwisho siku ya Jumatano.

Mwanahabari wa BBC Atulinda Allan ambaye alimsaidia Sweet Pepsi kwa kumfunga ‘bandage’ baada ya kupwigwa na wanajeshi amesema kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii kuwa amepata taarifa za kifo hicho kutoka kwa dada wa Sweet Pepsi.

View attachment 1250437View attachment 1250439View attachment 1250441
View attachment 1250442
Museveni anajisikia poa tu...hata huku kwetu kuna watu wanakufa(mfano Akwilina, Daniel, Mawazo) lakini kuna mtu anajisikia poa tu yani fresh na Jumapili anaingia Church kama kawa yani
 
Nakumbuka historia kadhaa niliwahi kusoma miaka kadhaa iliyopita, Mapinduzi ya Uingereza, Mapinduzi ya Ufaransa yalianza hivyo hivyo. Iko siku Umma utaingia barabarani na hakuna Askari atakaeweza kudhibiti
 
Wakati naiona hiyo video nilipata uchungu sana utadhani huyo jamaa ndugu yangu
Museveni anajisikia poa tu...hata huku kwetu kuna watu wanakufa(mfano Akwilina, Daniel, Mawazo) lakini kuna mtu anajisikia poa tu yani fresh na Jumapili anaingia Church kama kawa yani
 
Inatia sana uchungu ni unyama wa hali ya juu sana
Wanywa damu ulishaona wanasikitika? Nadhani alitaka akailambe kabisa. Samahani kwa maneno haya ila inatia uchungu.
 
Back
Top Bottom