Rais Mstaafu Jakaya Kikwete agomea eneo la ekari 50, ataka ekari 500

Muhimu wasilazimishe kutafuta hizo hekari 500 kwa kuwapora wanyonge ardhi yao, wakitaka kuzipata wawe tayari kuwalipa fidia wote watakaoathirika na hili wazo la Kikwete.

Sioni sababu kwanini wasijenge vitu vichache vya msingi kwa eneo lililopo, hizo nyumba za wahadhiri, hosteli, na hospitali vinaweza kuwa sehemu nyingine bora pasiwe mbali sana na chuo, kuliko kulazimisha vyote viwe pamoja kama chuo kimekuwa mbuga ya wanyama.
Asante.
Jakaya ana utata fulani ambao sio mzuri..hili suala litaleta utata soon.
Ila umri nao ni shida....
 
Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amekataa kupokea ekari 50 ambazo Serikali ya Mkoa wa Mbeya imezitoa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Dar es Saalam kampasi ya Mbeya na kutaka wapewe eneo lenye ukubwa wa ekari 500 au 1,000.

Kikwete amesema kama mkoa huo hautawapa eneo wanalolihitaji watahamishia chuo hicho katika mkoa mwingine ambao utakuwa tayari kuwapa ardhi yenye ukubwa wanaouhitaji.

Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi, Novemba 27,2021 wakati wa mahafali ya 51 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi kampasi ya Mbeya yaliyofanyika jijini hapa.

Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa chuo hicho kina hadhi kubwa hivyo wanahitaji ekari 500 hadi 1000 kwa ajili ya kujenga hosteli, makazi ya wahadhiri, wafanyakazi na hospitali.

Kauli hiyo ameitoa baada ya hotuba ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Mwanaidi Mtanda kusema kuwa ukosefu wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili licha ya kuwasilisha maombi yao kwa Serikali ya mkoa tangu mwaka jana.

"Ingawa simuoni hapa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (Juma Homera) lakini naamini viongozi wa Mkoa watamfikishia ujumbe, tunaomba kiwanja tujenge chuo cha kisasa na hili lipewe kipaumbele" amesema Mwanaidi.

Mara baada ya hotuba hiyo, Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa hazikidhi mahitaji yao

"Hii siyo sekondari kupewa ekari 50, tunataka eneo kubwa la ekari 500 hadi 1000 tenga hata kule Forest, mkishindwa tunahamia mkoa mwingine utakaoweza kutoa eneo kubwa, huu ni ujumbe kwa nyie viongozi" amesema Kikwete.
Chuo cha ushirika moshi, kcmc, mwenge stefano moshi havina zaidi ya ekari 10 kila kimoja na maisha yanaendelea. Mwambieni JK aache mbwembwe
 
Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amekataa kupokea ekari 50 ambazo Serikali ya Mkoa wa Mbeya imezitoa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Dar es Saalam kampasi ya Mbeya na kutaka wapewe eneo lenye ukubwa wa ekari 500 au 1,000.

Kikwete amesema kama mkoa huo hautawapa eneo wanalolihitaji watahamishia chuo hicho katika mkoa mwingine ambao utakuwa tayari kuwapa ardhi yenye ukubwa wanaouhitaji.

Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi, Novemba 27,2021 wakati wa mahafali ya 51 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi kampasi ya Mbeya yaliyofanyika jijini hapa.

Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa chuo hicho kina hadhi kubwa hivyo wanahitaji ekari 500 hadi 1000 kwa ajili ya kujenga hosteli, makazi ya wahadhiri, wafanyakazi na hospitali.

Kauli hiyo ameitoa baada ya hotuba ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Mwanaidi Mtanda kusema kuwa ukosefu wa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili licha ya kuwasilisha maombi yao kwa Serikali ya mkoa tangu mwaka jana.

"Ingawa simuoni hapa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (Juma Homera) lakini naamini viongozi wa Mkoa watamfikishia ujumbe, tunaomba kiwanja tujenge chuo cha kisasa na hili lipewe kipaumbele" amesema Mwanaidi.

Mara baada ya hotuba hiyo, Kikwete amesema hawawezi kukubali kupokea ekari 50 walizopewa kwakuwa hazikidhi mahitaji yao

"Hii siyo sekondari kupewa ekari 50, tunataka eneo kubwa la ekari 500 hadi 1000 tenga hata kule Forest, mkishindwa tunahamia mkoa mwingine utakaoweza kutoa eneo kubwa, huu ni ujumbe kwa nyie viongozi" amesema Kikwete.
Bwana JK anang'aka siku hizi bwana kwani yupo na dadake Sammy.
 
Naunga mkono hatua ya JK. Na chuo kikihamishwa utakuwa ni uhujumu. Hapo chuo cha kilimo wana kama ekari zaidi ya 3,000 mjini. Kwa nini wasiwagawie wenzao.

Nasikia waliomba Tanganyika packers, wana maelfu ya ekari, kwanini wasiwape UD? Hayo ni maeneo ya wizara ya kilimo, kama waziri wa kilimo na mifugo anagoma kutoa eneo basi aambiwe bosi wake.
 
Naunga Mkono Kikwete Kaona Mbali

Kweli kaona mbali na pia ameona wazungu walivyokuwa wanachukuwa maeneo makubwa hata kama kulikuwa na watu wachache sana

Kwani watu wanaongezeka na ni bora kuwa na sehemu kubwa kuliko baadae kuhangaika kutafuta maeneo mengine

Hebu angalia Vyuo vikuu na ukubwa wake
IMG_3327.jpg
 
Muhimu wasilazimishe kutafuta hizo hekari 500 kwa kuwapora wanyonge ardhi yao, wakitaka kuzipata wawe tayari kuwalipa fidia wote watakaoathirika na hili wazo la Kikwete.

Sioni sababu kwanini wasijenge vitu vichache vya msingi kwa eneo lililopo, hizo nyumba za wahadhiri, hosteli, na hospitali vinaweza kuwa sehemu nyingine bora pasiwe mbali sana na chuo, kuliko kulazimisha vyote viwe pamoja kama chuo kimekuwa mbuga ya wanyama.
Umeshawahi kufanya utafiti wa ukubwa wa maeneo ya vyuo kama UDSM na UDOM?

Na ujifunze vitu hivi.vikijengwa vinaweza kudumu miaka 100 na kuendelea.
 
Kwa nini anataka hicho chuo kihamishiwe katika mikoa mengine badala ya kubaki Dar tu?
Naunga mkono hatua ya JK. Na chuo kikihamishwa utakuwa ni uhujumu. Hapo chuo cha kilimo wana kama ekari zaidi ya 3,000 mjini. Kwa nini wasiwagawie wenzao. Nasikia waliomba Tanganyika packers, wana maelfu ya ekari, kwanini wasiwape UD? Hayo ni maeneo ya wizara ya kilimo, kama waziri wa kilimo na mifugo anagoma kutoa eneo basi aambiwe bosi wake.
 
Unafuu huo ni upi? Mbona kwenye nchi nyingine zenye vyuo bora vya umma hawavipanui kwa kuanzisha matawai mengi ndani ya nchi hiyo moja?
Hata nje ishu ya kutanua ipo mkuu. Mfano University of Calfornia, ina matawi kibao.
 
Ina matawi kibao ndani ya California ?
Huoni ingekuwa na maana zaidi kama Mbeya nayo ingekuwa na chuo kikuu kubwa mithili ya UDSM kiitwe University of Mbeya?!
Hata nje ishu ya kutanua ipo mkuu. Mfano University of Calfornia, ina matawi kibao.
 
Back
Top Bottom