tatum
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 5,786
- 4,490
Rais Mstaafu amekuwa mtu wa karibu sana kumjulia hali kwa Waziri Dr Kigwangalla mara baada ya kupata ajali mbaya huko Mkoa wa Manyara na kuhamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Hii ni mara ya tatu kwa Rais Mstaafu kufika Muhimbili na kumjulia hali waziri huyo wa Mali ya asili na utalii.
Hongera sana Rais Mstaafu kwa upendo huo tunajua kabisa hiyo ni hulka na tabia yako kwenda Muhimbili kuwajulia hali wagonjwa bila kujali hali wala wadhifa wao na umefanya hivyo mara nyingi sana ulipokuwa madarakani.
Huu ni mfano wa kuigwa kwa viongozi mbalimbali huko walipo mikoani na wilayani si lazima tujue kama mnafanywa hivyo ila wanaowazunguka watajua upendo wenu na jinsi gani mnawajali wananchi wenu kwa kuwapa faraja wanapokuwa katika maswahibu ya kuuguwa na kulazwa katika hospitali mbalimbali nchini.