JOESKY
JF-Expert Member
- Mar 25, 2015
- 816
- 2,032
Asalaam Aleykum ndugu zangu...!
Natumaini ni siku nyingine tena tumeamka tukiwa na afya tele Asante nyingi kwake Mola muumba wa mbingu na ardhi.
Siku ya leo nina ushauri mfupi kwa Rais Mama Samia atakapolivunja baraza la mawaziri basi anatakiwa amfuatilie waziri mmoja baada ya mwingine katika wizara husika. Katika awamu iliyopita (5) Kuliibuka tabia ya waziri kupewa wizara hata kama hana vigezo vya kuongoza hiyo wizara ili mradi tu una urafiki na Magufuli au ni kada mwenye wingi wa mapambio mdomoni.
Hawa mawaziri waliweza kuwa ndio chanzo kikubwa cha upotevu wa mali za taifa letu ikiwamo ufisadi wa kodi za watanzania bila huruma kabisa kwa sababu tu wamepewa rungu la uongozo hekima iliwavuka walikuwa jeuri na wakati ( ukali wao ni kuwadhibiti wanaohoji)
Ilifikia kipindi mawaziri wanasema wapo kwa ajili ya matumbo yao na sio kusimamia na kuendeleza rasilimali za taifa letu kwa maendeleo endelevu ya wananchi wetu. Ikiumiza sana pale ilipofikia hatua hata waziri anadiriki kusema atakuua kwa risasi hadharani na hakemewi (Kigwangala) huyohuyo akatuhumiwa kwa upotevu wa bilioni moja mpaka leo yupo anadunda mtaani na hajachukuliwa hatua wala mbio.
Kwa leo niishie hapa huu ni ushauri wangu kwako. Tuna imani nawe kubwa sana kuwa umeletwa na Mungu utibu majeraha ya Watanzania wengi walioumizwa kwa namna moja ama nyingine.
Nakutakia majukumu mema na Mungu akulinde.
Natumaini ni siku nyingine tena tumeamka tukiwa na afya tele Asante nyingi kwake Mola muumba wa mbingu na ardhi.
Siku ya leo nina ushauri mfupi kwa Rais Mama Samia atakapolivunja baraza la mawaziri basi anatakiwa amfuatilie waziri mmoja baada ya mwingine katika wizara husika. Katika awamu iliyopita (5) Kuliibuka tabia ya waziri kupewa wizara hata kama hana vigezo vya kuongoza hiyo wizara ili mradi tu una urafiki na Magufuli au ni kada mwenye wingi wa mapambio mdomoni.
Hawa mawaziri waliweza kuwa ndio chanzo kikubwa cha upotevu wa mali za taifa letu ikiwamo ufisadi wa kodi za watanzania bila huruma kabisa kwa sababu tu wamepewa rungu la uongozo hekima iliwavuka walikuwa jeuri na wakati ( ukali wao ni kuwadhibiti wanaohoji)
Ilifikia kipindi mawaziri wanasema wapo kwa ajili ya matumbo yao na sio kusimamia na kuendeleza rasilimali za taifa letu kwa maendeleo endelevu ya wananchi wetu. Ikiumiza sana pale ilipofikia hatua hata waziri anadiriki kusema atakuua kwa risasi hadharani na hakemewi (Kigwangala) huyohuyo akatuhumiwa kwa upotevu wa bilioni moja mpaka leo yupo anadunda mtaani na hajachukuliwa hatua wala mbio.
Kwa leo niishie hapa huu ni ushauri wangu kwako. Tuna imani nawe kubwa sana kuwa umeletwa na Mungu utibu majeraha ya Watanzania wengi walioumizwa kwa namna moja ama nyingine.
Nakutakia majukumu mema na Mungu akulinde.