Rais Mbishi wa Kuelewa

jyfranca

JF-Expert Member
Oct 3, 2010
297
8
Rais ametangaza Baraza lake la Mawaziri, kama kawaida ya watu wengi wanachojua ni kumsifia tuu bila kumkosoa. Uchaguzi huu tumeona kura za Rais zimepungua zaidi ya asilimia 20 na bado Rais hajaelewa kuwa wananchi hawaridhiki na utendaji wake. Kaunda baraza kubwa kama kawaida yake. Baadhi ya Wizara hazina maana yoyote na zilipaswa ziunganishwe.
Mapendekezo yangu ni kama ifuatavyo;
1. Kuliko kuwa na mawaziri watatu Ofisi ya Rais angebaki mmoja
2.Pawe na waziri mmoja ofisi ya makamu wa Rais badala ya wawili
3.Ofisi ya waziri mkuu iwe na waziri mmoja badala ya watatu wa sasa, pabakiwe na waziri wa TAMISEMI tuu.
4.Wizara ya Uchukuzi na Ujenzi iwe moja
5.Wizara ya mahusiano ya Afrika Mashariki irudi ndania ya Wizara ya Mambo ya nje.
6.Wizara ya maji irudi kwenye wizara ya chakula

Hapo Rais angeweza kupunguza wizara 8 kwa haraka, pia wizara nyingi hazihitaji manaibu waziri.
Tusiogope kuikosoa serikali, mambo ya kupongezana kila siku yanawaumiza walipa kodi
 
Rais ametangaza Baraza lake la Mawaziri, kama kawaida ya watu wengi wanachojua ni kumsifia tuu bila kumkosoa. Uchaguzi huu tumeona kura za Rais zimepungua zaidi ya asilimia 20 na bado Rais hajaelewa kuwa wananchi hawaridhiki na utendaji wake. Kaunda baraza kubwa kama kawaida yake. Baadhi ya Wizara hazina maana yoyote na zilipaswa ziunganishwe.
Mapendekezo yangu ni kama ifuatavyo;
1. Kuliko kuwa na mawaziri watatu Ofisi ya Rais angebaki mmoja
2.Pawe na waziri mmoja ofisi ya makamu wa Rais badala ya wawili
3.Ofisi ya waziri mkuu iwe na waziri mmoja badala ya watatu wa sasa, pabakiwe na waziri wa TAMISEMI tuu.
4.Wizara ya Uchukuzi na Ujenzi iwe moja
5.Wizara ya mahusiano ya Afrika Mashariki irudi ndania ya Wizara ya Mambo ya nje.
6.Wizara ya maji irudi kwenye wizara ya chakula

Hapo Rais angeweza kupunguza wizara 8 kwa haraka, pia wizara nyingi hazihitaji manaibu waziri.
Tusiogope kuikosoa serikali, mambo ya kupongezana kila siku yanawaumiza walipa kodi

Bora ungeishia kukosa tu bila kutoa pendekezo lako. Kwa ufupi pendekezo lako la eti wizara ya maji ihamishiwe chakula linatokana na ufahamu wako mdogo. Sababu alizotoa jk kuhusu wizara ya maji kuendelea kujitegemea bila kuunganishwa na sekta nyingine ina mantiki kubwa na mimi ninamuunga mkono. Suala la maji hapa nchini bado ni tatizo. Hata takwimu tunazolishwa na ccm za upatikanaji wa maji mijini na vijiji naona kama ni za kisiasa tu kwa maana kwamba ni kama zimekarabatiwa tu ili kukidhi matakwa ya kisiasa. Maji ni tatizo haliwezi kuachwa liendelee kusumbua wananchi. Juzi nilikuwa tabora. Ukiangalia maji wanayohudumiwa wakazi wa tabora utawaonea huruma.
Ingekuwa ni nchi zilizoendelea labda yangefaa kwa shughuli za umwagiliaji tu na siyo kwa matumizi ya binadamu.
 
Gosbert,
Hivi unaelewa kazi za waziri. Zinazofanya kazi ni taasisi na mamlaka zinazo husika na maji. Kama hizo taasisi hazipo au hazina mwelekeo hata utengeneze wizara tatu za maji hakuta kuwa na maendeleo. Binafsi ningeunganisha Maji na Mazingira. Kwani vina uhusiano mkubwa sana na hata kiutaalamu vinaingiliana sana.
 
Usemalo ni mkweli mwana jamvi lakini je nani atalitekeleza.... Kama hakusikia awamu ya kwanza unadhani atafanya hivyo ndani ya miaka miwili... Na je akifanya hivyo itatusaidia kweli... Nadhani tuanze kumshauri rais ajae si huyu
 
Bora ungeishia kukosa tu bila kutoa pendekezo lako. Kwa ufupi pendekezo lako la eti wizara ya maji ihamishiwe chakula linatokana na ufahamu wako mdogo. Sababu alizotoa jk kuhusu wizara ya maji kuendelea kujitegemea bila kuunganishwa na sekta nyingine ina mantiki kubwa na mimi ninamuunga mkono. Suala la maji hapa nchini bado ni tatizo. Hata takwimu tunazolishwa na ccm za upatikanaji wa maji mijini na vijiji naona kama ni za kisiasa tu kwa maana kwamba ni kama zimekarabatiwa tu ili kukidhi matakwa ya kisiasa. Maji ni tatizo haliwezi kuachwa liendelee kusumbua wananchi. Juzi nilikuwa tabora. Ukiangalia maji wanayohudumiwa wakazi wa tabora utawaonea huruma.
Ingekuwa ni nchi zilizoendelea labda yangefaa kwa shughuli za umwagiliaji tu na siyo kwa matumizi ya binadamu.
Naogogopa kukuita mbumbumbu, jaribu kuwa unasoma kwa makini kabla hujajibu hoja, hakuna mtu amekataa kuna tatizo la maji. Je Tatizo la maji dawa yake ni wizara? Je tuunde wizara ya umeme kwa kuwa kuna tatizo la kukatika umeme kila mara? Vipi tuwe na wizara ya kuzuia wanafunzi kupata mimba kwa kuwa wanapata mimba sana? au tuunde wizara ya kusimamia ajali kwa kuwa kuna ajali nyingi za magari? Au tuunde wizara ya kuondoa misongamano ya magari barabarani? Jaribu kuwa kama umeelimika tatizo la maji dawa yake si wizara.Je unajua gharama ya wizara moja? Unajua kiasi gani tuu kumlipa waziri katibu naibu waziri na hao wafanyakazi. Hoja yako ya kipuuzi na unatakiwa uelimishwa, si kila tatizo linatakiwa wizara, je kama wizara imeundwa tatizo la maji limekwisha? We unaitaji elimu
 
Gosbert,
Hivi unaelewa kazi za waziri. Zinazofanya kazi ni taasisi na mamlaka zinazo husika na maji. Kama hizo taasisi hazipo au hazina mwelekeo hata utengeneze wizara tatu za maji hakuta kuwa na maendeleo. Binafsi ningeunganisha Maji na Mazingira. Kwani vina uhusiano mkubwa sana na hata kiutaalamu vinaingiliana sana.

Kwa kuunganisha maji na mazingira ninakubaliana nawe kabisa.
 
Even angeweka Wizara 1000 yaani kila kata, isingesaidia, jibu si wizara nyingiiiiiiii au hata angekuwa na wizara 15 bado si suluhisho, Suluhisho la nchi yetu ni LACK OF GOOD GOVERNANCE, mbona mnalielewa hili, tuna serikali ambayo si tendaji, usanii, we want responsible Government, mheshimiwa anajua huyu, yule, kaharibu, si mchapakazi, bado anamweka in cabinet, pili matumizi ya serikali mmmhhh out of touch, sina imani, hali itakuwa ngumu mnooooooooo, wait
 
Back
Top Bottom