Rais, Majaji na wote wasiokatwa kodi kwenye mishahara yao ni muda muafaka nao waanze kulipa kodi

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
Kama kulipa kodi ni uzalendo, basi rais wa nchi ndiye anayepaswa kuwa mzalendo namba moja.

Kama Tanzania ni nchi ya Usawa, basi haiyumkiniki wawepo watu katika nchi hii wawe ni wavuja jasho, wanaokamuliwa kodi kwenye mishahara yao lakini kuna jingine la watanzania haohao mfano rais na Majaji ambao hawakatwi kodi kabisa kwenye mishahara yao

Majuzi hapa waziri wa fedha amesema bungeni kuwa katika mwaka huu wa fedha wameweka kodi kwenye laini ya Simu, kwamba watu watakuwa wakikatwa kuanzia shilingi 10 hadi 200 kila siku kulingana na uingizaji wao wa salio, wao wanaita eti kodi ya "Uzalendo".

Waziri wa fedha anasema eti pesa hizo zinatakiwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa mahospitalini. Ngoja nimkumbushe Waziri wa fedha Chanzo kizuri cha mapato ya serikali, Waziri ajue kuwa kuna wananchi nchi hii hawalipi kodi kwenye mishahara yao mfano ni RAIS na MAJAJI.

CCM huwa wanapenda kujitangaza kuwa nchi hii ni nchi ya kijamaa, Umewahi kuona ujamaa wa wapi wenye matabaka ya wazi ya namna hii ikiwemo ukosefu wa Usawa kwenye kulipa kodi?

Yaani sisi walalahoi kila siku tukamuliwe kodi ila top Class wao wale tu mishahara itokanayo na kodi zetu lakini wao wasilipe kodi, hii fairness ya wapi?

Tunataka sheria ibadilishwe, Kila anayepaswa kulipa kodi alipe kodi. Rais alipe kodi, Majaji walipe kodi na yeyote yule aliyepewa kinga ya kulipa kodi alipe.

Haiwezekani ionekane eti rais kulipa kodi ni kitu kibaya kwake lakini eti kiwe wajibu kwa raia wa kawaida!
 
Hao majaji si walikua raia wa kawaida kwanza? Maana yake walikua wanalipa kodi siyo? Acheni wivu, kwanza wako wangapi na impact ya kodi inayotazamiwa kutoka kwao ni ipi?
 
Tuliambiwa Jiwe alikua mzalendo halisi kuwahi kutokea.

Kwa transparency MATAGA wanaweza kutuambia makato yake kwenye mshahara yalikuawaje?

Ilhali aliwahi kusema analipwa millioni 9 na hazimtoshi. Huku akisahau kero za wafanyakazi na na tatizo la ajira alilolitengeneza..

Mwalimu aliwahi kujipunguzia 20% ya mshahara wake ili mambo yaende je nani mzalendo hapa?

Nchi za watu huku kila kiongozi mshahara wake uko wazi sababu maboss ni raia ila Africa kiujumla mishahara inafanywa siri sababu ni kufuru ikiwekwa wazi ni anasa zisizo na maana tena kwa nchi masikini.
 
Umeongea vizuri sana ndugu. Mimi kila nikiangalia Salary Slip upande wa kodi, roho inanisononeka sn. Kodi kwa mwaka nalipa kubwa kuliko Mfanya biashara mwenye maduka makubwa ya Hardware.

Kwa kweli, hamasa tunayopewa ya sisi kulipa kodi iwnzie kwa viongozi na wote wapokeao mishahara serikalini. Ukilipa kodi, ndio utaona uchungu au raha ya kushadadia iongrzwe au ipunguzwe. Huwezi ongea kitu usichokijua maumivu yake.
 
Hao majaji si walikua raia wa kawaida kwanza? Maana yake walikua wanalipa kodi siyo? Acheni wivu, kwanza wako wangapi na impact ya kodi inayotazamiwa kutoka kwao ni ipi?
Yaani watu wasilipe kodi halafu useme eti tunawaonea wivu?, Hatuwaonei wivu bali tunakasarishwa na wao kuwa wanyonyaji

Kodi inalipwa na mtu mmojammoja hatuangalii uchache wa watu au wingi wa watu katika fani husika.

KILA ANAYEPATA KIPATO HALALI HANA BUDI KULIPA KODI KWENYE KIPATO HICHO
 
Hao majaji si walikua raia wa kawaida kwanza? Maana yake walikua wanalipa kodi siyo? Acheni wivu, kwanza wako wangapi na impact ya kodi inayotazamiwa kutoka kwao ni ipi?
Kwa hiyo unashauri wengine walipe kodi, halafu wengine wawe ni wa kukutumia tu hiyo kodi? Unatumia kigezo gani kuwaondoa kwenye kundi la walipa kodi?

Maana kama kwa umuhimu, Waanze Walimu (wafundishajina walezi wa taaluma zote ), wasamehewe pia mafaktari(wanaookoa uhai wa watu), waje vyombo vya Usalama, ndio wafuate wajaji. Kiujumla, kila mtumishi kwenye sekta yake ni muhimu.

Kwa hiyo, suala la kulipa kodi sio la kuangalia idadi. Mfano, watu wanaoweka private number kwenyr magari yao ni wangapi? Sini wachache sn, mbona wameundikwa kifungu cha sheria kuwataka walipie kodi?
 
Back
Top Bottom