Rais Magufuli yupo sahihi: Tanzania ilikuwa inaenda kuwa kama Colombia au Zaire ya Mobutu

Alex Fredrick

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
680
1,338
Tanzania toka Mwl JK Nyerere alipoondoka madarakani Nchi ilianza kuseleleka pasi na wengine kuelewa tunapoelekea.

Rushwa ilianza kutamalaki kuanzia ngazi ya chini mpka magogoni huku Viongozi tuliowapa dhamana kujifanya hamnzo kwa kuinua mabega juu,Wale tuliohoji tunakoelekea tuliambiwa tuache wivu wa kike.

Wafanyabaishara wakajipenyeza kwa wakubwa ili wapate kandarasi nono,Tukashuhudia rushwa ikimea kila uchao wafanyabiashara wakashika Nchi na Viongozi ndio tuliwapa dhamana ndio wakawa visemeo cha wafanyabiashara rejea pesa za Escrow.

Nchi ikashikwa rasmi na matajiri na Kandarasi zote zikawa zao huko Mahakamani Majaji na baadhi ya Mahakimu Tukashuhudia wakigaiwa pesa kama njugu.

Wanyonge wakatupwa rasmi na wakakosa sauti ndani yao Nchi (Viongozi na wafanyabiashara tu wakifaidi keki ya Taifa).

Rais Magufuli alipoingia madarakani aliliona hilo kwa kwa jina la Tai,kwahiyo maamuzi mengine anayofanya Mh Rais Magufuli yupo sahihi kabisa na apaswa kuungwa mkono.

Hizi kesi za wafanyabiashara zingekuwa zinaendeshwa kwa mfumo ule tuliouzoea hawa majizi sasa hivi wangekuwa nje maana wangehonga Majaji na Mahakimu kama walivyozoea hapo awali.

Na Hii haipo kwa Rais Magufuli tu ipo Duniani kote pindi Nchi inapokuwa hovyo na kupata Kiongozi sampuli ya Magufuli.

Na tusiombe siku Rais Magufuli afukue makuburi ya Epa,Escrow na mengine.Angola sasa hvi Edouardo Dos Santos anatapika pesa za Nchi yeye na familia yake huku akitolewa kinga ya kutoshtakiwa.

Bado tunamhitaji sana Rais Magufuli kwenye Nchi hii ili tuweze kupiga hatua kama Rwanda ya Paul Kagame

Alex Fredrick
Dar es salaam


FB_IMG_1564060192380.jpeg
 
Sasa mbona inafanana na Colombia zaidi

maana mbunge anapigwa shaba live na hakuna uchunguzi
Watu wanatekwa wanapotezwa
watu wanabambikiziwa kesi kisha wanalazimishwa kununua uhuru wao
maiti zinaokotwa kwenye viloba kipindi cha awamu hii

sasa kama nchi hii haifanani na Colombia kipindi cha awamu hii basi haijawahi kufanana huko nyuma
 
"Rais Magufuli yupo sahihi,Tanzania ilikuwa inaenda kuwa kama Colombia au Zaire ya Mobutu"; hilo sawa, lakini je unaonaje kama sio tunaelekea kuwa kama zimbabwe ya Mugabe au Venezuela ya Maduro?!
 
je
1. hakuna rushwa?
2. wanyonge ni watu gani?
3. hao wanyonge wana sauti sasa?
4. unajua tunakoelekea?
1. Imepungua kwa 99%

2.Ni wale waliokua wananyonywa kwa awamu kadhaa zilizopita

3.kabisa wanyonge sasa tuna sauti ya kufa mtu kila ofisi tunayoingia matatizo yetu hisikilizwa na kutatuliwa kwa wakati kwani watumishi sasa ni waoga hasa pale wasipotimiza wajibu wao

4.Tunaelekea kua taifa linalojielewa na kujiendesha wenyewe bila kutegemea misaada ya mabeberu
 
je
1. hakuna rushwa?
2. wanyonge ni watu gani?
3. hao wanyonge wana sauti sasa?
4. unajua tunakoelekea?
1Rushwa ipo lakini woga umewaaja sio kama ilivyo kuwa.
2 wanyonge ambao walikua na haki ya kupata chao lakini hawakipati hata kama ni halali yao
3 sauti yao inasikika kwa sasa kama wataamua kuitoa mfano yule bibi wa arusha aliyetaka kudhulumia ardhi yake sauti ilisikika
4 kujua tunaoelekea kila mmoja na macho yake mweyekuona mbali au karibu inategemea na nguvu yake ya macho...
 
Sioni hoja zaidi ya kulalama hii inaonyesha wengi ni wale mliokuwa mnanufaika na uchafu huu kwa namna moja au nyingine
 
Utuambie na trioni 1.5 iko wapi maana katika awamu zote haijawai tokea kiasi kikubwa cha pesa namna hii ikatoweka tu
 
Baaada ya makundi ya kuteua wagombea tulikuwa tunaelekea kuwa majeshi ya kupigania wagombea
 
Aondolewe kinga, tumdai hela za mv Bagamoyo, meli ya samaki, mauzo ya nyumba za Serikali, mikataba ya ununuzi wa ndege, pesa tasilimu 1.5trilion, kukanyaga katiba, matumizi mabaya ya madaraka kwa upendeleo wa wazi kwa makonda.
 
Sasa mbona inafanana na Colombia zaidi

maana mbunge anapigwa shaba live na hakuna uchunguzi
Watu wanatekwa wanapotezwa
watu wanabambikiziwa kesi kisha wanalazimishwa kununua uhuru wao
maiti zinaokotwa kwenye viloba kipindi cha awamu hii

sasa kama nchi hii haifanani na Colombia kipindi cha awamu hii basi haijawahi kufanana huko nyuma
Ndio wanaosema wivu wa kike. Macho yako hayaoni vizuri. Ndiye aliyesema tusiwabuzi wachimba dhahabu. Yako wapi? Zitto na wezake wako kimyaa
 
1. Imepungua kwa 99%

2.Ni wale waliokua wananyonywa kwa awamu kadhaa zilizopita

3.kabisa wanyonge sasa tuna sauti ya kufa mtu kila ofisi tunayoingia matatizo yetu hisikilizwa na kutatuliwa kwa wakati kwani watumishi sasa ni waoga hasa pale wasipotimiza wajibu wao

4.Tunaelekea kua taifa linalojielewa na kujiendesha wenyewe bila kutegemea misaada ya mabeberu
sawa.....
 
1. Imepungua kwa 99%

2.Ni wale waliokua wananyonywa kwa awamu kadhaa zilizopita

3.kabisa wanyonge sasa tuna sauti ya kufa mtu kila ofisi tunayoingia matatizo yetu hisikilizwa na kutatuliwa kwa wakati kwani watumishi sasa ni waoga hasa pale wasipotimiza wajibu wao

4.Tunaelekea kua taifa linalojielewa na kujiendesha wenyewe bila kutegemea misaada ya mabeberu
sawa.....
 
1. Imepungua kwa 99%

2.Ni wale waliokua wananyonywa kwa awamu kadhaa zilizopita

3.kabisa wanyonge sasa tuna sauti ya kufa mtu kila ofisi tunayoingia matatizo yetu hisikilizwa na kutatuliwa kwa wakati kwani watumishi sasa ni waoga hasa pale wasipotimiza wajibu wao

4.Tunaelekea kua taifa linalojielewa na kujiendesha wenyewe bila kutegemea misaada ya mabeberu
Wajinga na wapumbavu hawana hoja za msingi kilichobaki ni kusema;-
1. Watu wanatekwa ovyo.
2. Watumishi hawapandishiwa mishahara wala madaraja.
3. Hakuna Democracy.
4. Wabunge wanapigwa risasi.
5. Nchi inaendeshwa kibabe.
6. Watu wanaokotwa kwenye viroba.
7. Hakuna uhuru wa vyombo vya habari.
Tusubir uchaguzi serikali za mitaa.
 
Back
Top Bottom