Rais Magufuli: Waliouziwa Viwanda wakashindwa kuviendeleza, Wakamatwe wawekwe Korokoroni

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,483
54,850
Heshima kwenu wakuu,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli, amemuagiza Waziri wa Viwanda na Biashara Mwijage kuhakikisha Wote waliouziwa Viwanda halafu wakashindwa kuviendeleza, wakamatwe na wawekwe ndani.

Anasisitiza kwamba Tanzania ya Magufuli ni Tanzania ya Viwanda, anataka kuona Viwanda kama ambavyo pwani wamefanya. Sasa hivi pwani ina viwanda zaidi ya 371.

=====
Pwani. Rais John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, kuwanyang’anya viwanda wamiliki ambao wameshindwa kuviendeleza.

Ameyazungumza hayo leo (Alhamisi) akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambako amezindua viwanda saba.

“Kipindi cha nyuma tulipofanya makosa ni pale tulipouza viwanda kwa watu binafsi, sasa kuna viwanda 197 vimeshakufa waliouziwa hawajishughulishi na vingine vipo kama magofu,” amesema.

Kutokana na hilo, Rais amesema; "natoa wito kwa wote waliouziwa viwanda kipindi cha nyuma na sasa wameshindwa kuviendeleza , naagiza sasa basi mrudishe na wewe Waziri Mwijage tumia hata nguvu kama kuwaweka ndani weka tu siku akitoka huko atakuta kiwanda kimeanza kazi."

Chanzo: Mwananchi
 
Naona siku hizi umeshidnwa kumtetea tena amekuangusha sana mno au! Maana comments zako zinanitoa knock out
Ukiwapanga wanasiasa wote walio hai hapa nchini.
Magufuli is second to none.
hilo halihitaji kuandamana wala elimu ya juu mkuu.
hata wewe unajua sema kiburi tu...
Huyo jamaa hapo juu kaleta kipande cha habari badala ya habari utadhani alikuwa anakimbizwa...
naona umechelewa umekuta ameshafanya editing.
Kama umemikili kiwanda kwa makubaliano ya kukiendeleza na umevunja kwa sababu zisizoeleweka lazima uchukuliwe hatua hakuna namna...
 
Ukiwapanga wanasiasa wote walio hai hapa nchini.
Magufuli is second to none.
hilo halihitaji kuandamana wala elimu ya juu mkuu.
hata wewe unajua sema kiburi tu...
Huyo jamaa hapo juu kaleta kipande cha habari badala ya habari utadhani alikuwa anakimbizwa...
naona umechelewa umekuta ameshafanya editing.
Kama umemlikili kiwanda kwa makubaliano ya kukiendeleza na umevunja kwa sababu zisizoeleweka lazima uchukuliwe hatua hakuna namna...

Katika wanasiasa wote kwangu mimi JPM ni 'ZERO' sababu kubwa hayuko focused.Na ni mtu mwenye CHUKI,HASIRA na VISASI hafai kuwa kiongozi.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom