Rais Magufuli: Wakati wa mchakato wa uchaguzi tusiende na majina mfukoni. Tusikate majina ya wagombea kwasababu zetu binafsi

Chibudee

JF-Expert Member
Dec 28, 2016
1,775
2,397
Niwaombe Viongozi wenzangu ndani ya Wilaya na Mikoa wakati wa mchakato wa uchaguzi tusiende na majina mfukoni tuoneshe ukomavu mwaka huu, tuwaache wengine wakurupuke kuvunja taratibu wagombane, tusikate majina ya Wagombea kwasababu zetu binafsi

Mtu unajijua ni Mchezaji mzuri unaficha chenga zako kwanini?, tujiandae na uchaguzi, CCM hii sio ile ya nyuma na Wapinzani wetu sio wale wa nyuma, Wapinzani wamebadilisha mikakati yao, mingine wanaiweka hadharani na mingine ni ya kificho, tusibweteke

Sisi wasukuma ukiwa unaenda kutoa posa hasa Mwanamke awe mweupe huwezi kupeleka ng’ombe nusunusu utapeleka pesa yote ili mwingine asije kukuwahi, weupe oyee..aah mnamuangalia Mama Samia eeh?
Rais.jpg
 
Niwaombe Viongozi wenzangu ndani ya Wilaya na Mikoa wakati wa mchakato wa uchaguzi tusiende na majina mfukoni tuoneshe ukomavu mwaka huu, tuwaache wengine wakurupuke kuvunja taratibu wagombane, tusikate majina ya Wagombea kwasababu zetu binafsi

Mtu unajijua ni Mchezaji mzuri unaficha chenga zako kwanini?, tujiandae na uchaguzi, CCM hii sio ile ya nyuma na Wapinzani wetu sio wale wa nyuma, Wapinzani wamebadilisha mikakati yao, mingine wanaiweka hadharani na mingine ni ya kificho, tusibweteke

Sisi wasukuma ukiwa unaenda kutoa posa hasa Mwanamke awe mweupe huwezi kupeleka ng’ombe nusunusu utapeleka pesa yote ili mwingine asije kukuwahi, weupe oyee..aah mnamuangalia Mama Samia eeh?
yetu macho!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anayesema watu wasiende na majina mfukoni, yeye tayari ana majina yake!
 
Yeye mwenyewe jina lake lilikua la mfikoni october wanaleta jingine la mfukoni
 
Aruhusu fair play katika siasa. Pia asubutu kuwapa Watanzania tume huru ya uchaguzi.Atubu pia kushangilia ushindi wa 99.9% mitaa kwa kauli yake jana Na mara nyingi " Msema kweli ni mpenzi wa Mungu"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom